Add parallel Print Page Options

Hivyo, Maandiko yanasema,

“Tazameni, naweka katika Sayuni Jiwe la msingi katika jengo,
    lililoteuliwa na kuheshimika,
na yeyote anayeamini hataaibishwa.”(A)

Inamaanisha heshima kwenu mnaoamini, bali kwa wasioamini,

“jiwe walilolikataa wajenzi
    limekuwa jiwe la muhimu kuliko yote.”(B)

Na,

“jiwe linalowafanya watu wajikwae
    na mwamba unaowafanya watu waanguke.”(C)

Walijikwaa kwa sababu hawakuutii ujumbe wa Mungu, na Mungu alisema hilo litatokea wasipotii.

Read full chapter