Font Size
Luka 11:1-3
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Luka 11:1-3
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yesu Afundisha Kuhusu Maombi
(Mt 6:9-15)
11 Siku moja Yesu alitoka akaenda mahali fulani kuomba. Alipomaliza, mmoja wa wafuasi wake akamwambia, “Yohana aliwafundisha wafuasi wake namna ya kuomba. Bwana, tufundishe nasi pia.”
2 Yesu akawaambia wafuasi wake, “Hivi ndivyo mnapaswa kuomba:
‘Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe daima.
Tunaomba Ufalme wako uje.
3 Utupe chakula tunachohitaji kila siku.
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International