Font Size
Marko 14:1-3
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Marko 14:1-3
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Mpango wa Kumwua Yesu
(Mt 26:1-5; Lk 22:1-2; Yh 11:45-53)
14 Ilikuwa yapata siku mbili kabla ya Sikukuu ya Pasaka na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Wakuu wa makuhani na walimu wa Sheria walikuwa wakitafuta njia, kwa ujanja fulani, ya kumkamata na kumuua Yesu. 2 Kwani walikuwa wakisema “tusifanye hivi wakati wa sherehe, ama sivyo watu watafanya fujo.”
Mwanamke Ampa Yesu Heshima
(Mt 26:6-13; Yh 12:1-8)
3 Yesu alikuwa Bethania, katika nyumba ya Simoni mwenye ugonjwa mbaya sana wa ngozi. Wakati ameketi mezani mwanamke mmoja alimwijia. Naye alikuwa na gudulia la mawe lililojaa manukato ya bei ghali yaliyotengenezwa kwa nardo safi. Mwanamke huyo alilifungua gudulia lile kwa kulivunja na kumwagia Yesu manukato kichwani mwake.
Read full chapter
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International