Add parallel Print Page Options

14 Lakini Pilato akawauliza, “Kwa nini? Je, amefanya kosa gani?”

Lakini wote wakapiga kelele zaidi, “Muue kwenye msalaba!”

15 Pilato alitaka kuwaridhisha watu, kwa hiyo alimweka huru Baraba kwa ajili yao. Akaamuru maaskari wampige Yesu viboko na kisha akamtoa kwao ili akauawe kwenye msalaba.

16 Maaskari wakamwongoza Yesu hadi ndani ya baraza la jumba la gavana (lililojulikana kama Praitorio). Huko wakakiita pamoja kikosi cha maaskari.

Read full chapter