Font Size
Matayo 6:5-7
Neno: Bibilia Takatifu
Matayo 6:5-7
Neno: Bibilia Takatifu
Mafundisho Kuhusu Sala
5 “Na mnaposali, msiwe kama wanafiki; maana wao wanapenda kusimama na kusali katika masinagogi na kando ya barabara ili waonekane na watu. Nawaambieni kweli, wao wamekwisha kupata tuzo yao. 6 Unaposali, nenda chumbani kwako ufunge mlango na umwombe Baba yako aliye sirini. Na Baba yako aonaye sirini atakupa tha wabu.
7 “Mnaposali msirudie maneno yale yale kama wafanyavyo watu wa mataifa wasiomjua Mungu. Kwa maana wao hudhani kwamba watasi kilizwa kwa sababu ya wingi wa maneno yao.
Read full chapter
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Copyright © 1989 by Biblica