20 Lakini waamini walipokusanyika kumzunguka, aliamka, akarudi nao mjini. Kesho yake akaondoka na Barnaba wakaenda mpaka Derbe.

Paulo Na Barnaba Warudi Antiokia

21 Walipokwisha hubiri Habari Njema katika mji ule na watu wengi wakaamini wakawa wanafunzi, walirudi Listra na Ikonio na Antiokia. 22 Huko waliwatia nguvu wanafunzi na kuwashauri waendelee kukua katika imani. Wakawaonya wakisema, “Tunalazimika kuingia katika Ufalme wa Mungu kwa kupitia katika mateso mengi.”

Read full chapter