Add parallel Print Page Options

22 Ee Babeli, muziki wa wapigao vinanda na ala zingine waimbaji na tarumbeta,
    hautasikika tena ndani yako.
Hakuna mfanyakazi afanyaye kazi atakayeonekana ndani yako tena.
    Sauti ya jiwe la kusagia haitasikika ndani yako tena.
23 Mwanga wa taa hautang'aa ndani yako tena.
    Sauti za maarusi hazitasikika ndani yako tena.
Wafanyabiashara wako walikuwa watu wakuu wa ulimwengu.
    Mataifa yote yalidanganyika kwa uchawi wako.
24 Una hatia ya vifo vya manabii, na watakatifu wa Mungu,
    na vya wote waliouawa duniani.”

Read full chapter