Add parallel Print Page Options

Tushangilie na kufurahi na
    kumpa Mungu utukufu!
Mpeni Mungu utukufu, kwa sababu arusi ya Mwanakondoo imewadia.
    Na bibi arusi wa Mwanakondoo amekwisha jiandaa.
Nguo ya kitani safi ilitolewa kwa bibi arusi ili avae.
    Kitani ilikuwa safi na angavu.”

(Kitani safi inamaanisha mambo mazuri ambayo watakatifu wa Mungu waliyatenda.)

Kisha malaika akaniambia, “Andika hili: Heri ni kwa wale walioalikwa kwenye karamu ya arusi ya Mwanakondoo!” Kisha malaika akasema, “Haya ni maneno ya Mungu mwenyewe.”

Read full chapter