Font Size
Yohana 10:16-18
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yohana 10:16-18
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
16 Nina kondoo wengine ambao hawamo kwenye kundi hili hapa. Hao nao napaswa kuwaongoza. Kwani wataisikia sauti yangu. Baadaye kutakuwa na kundi moja na mchungaji mmoja.[a] 17 Baba ananipenda kwa sababu nautoa uhai wangu. Nautoa uhai wangu ili niweze kuuchukua tena. 18 Hakuna anayeweza kuuchukua uhai wangu kutoka kwangu. Nautoa uhai wangu kwa hiari yangu. Ninayo haki ya kuutoa, na ninayo haki ya kuuchukua tena. Haya ndiyo aliyoniambia Baba yangu.”
Read full chapterFootnotes
- 10:16 Yesu ana maana kuwa anao wafuasi ambao si Wayahudi. Tazama Yh 11:52.
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International