Font Size
Yohana 4:9-11
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yohana 4:9-11
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
9 Mwanamke yule akajibu, “Nimeshangazwa wewe kuniomba maji unywe! Wewe ni Myahudi nami ni mwanamke Msamaria!” (Wayahudi hawana uhusiano na Wasamaria.[a])
10 Yesu akajibu, “Hujui kile Mungu anachoweza kukukirimu. Na hunijui mimi ni nani, niliyekuomba maji ninywe. Kama ungejua, nawe ungekuwa umeniomba tayari, nami ningekupa maji yaletayo uzima.”
11 Mwanamke akasema, “Bwana, utayapata wapi maji yaliyo hai? Kisima hiki kina chake ni kirefu sana, nawe huna kitu cha kuchotea.
Read full chapterFootnotes
- 4:9 Wayahudi … Wasamaria Au “Wayahudi hawatumii vitu ambavyo Wasamaria wametumia.”
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International