Yohana 1:1-9
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yesu ni Neno la Mungu la Milele
1 Mwanzoni Kabla ulimwengu haujaumbwa
alikuwepo Neno.[a]
Huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu,
na Neno alikuwa Mungu.
2 Alikuwepo pamoja na Mungu
toka mwanzo.
3 Kila kitu kilifanyika kupitia kwake.
Hakuna chochote katika uumbaji wa Mungu
kilichofanyika bila yeye.
4 Ndani yake Neno kulikuwemo na uzima,
na uzima huo ulikuwa nuru
kwa ajili ya watu wa ulimwenguni.
5 Nuru[b] hiyo yamulika gizani,
na giza halikuishinda.[c]
6 Alikuwepo mtu aliyeitwa Yohana, aliyetumwa na Mungu. 7 Alikuja kuwaambia watu kuhusu nuru. Ili kupitia kwake watu wote waweze kusikia kuhusu yule aliye nuru na wamwamini. 8 Yohana mwenyewe hakuwa nuru. Lakini alikuja kuwaambia watu kuhusu nuru.
9 Nuru ya kweli,
anayeleta mwangaza kwa watu wote,
alikuwa tayari kuonekana kwa ulimwengu.
Footnotes
- 1:1 Neno Kwa Kiyunani neno hili ni logos, lenye maana mawasiliano ya aina yoyote. Linaweza kutafsiriwa “ujumbe”. Hapa lina maana ya Kristo; njia ambayo Mungu alitumia kuueleza ulimwengu kuhusu yeye. Pia katika mstari wa 10,14 na 16.
- 1:5 Nuru Lenye maana ya Kristo, Neno, aliyeleta ulimwenguni uelewa kuhusu Mungu. Pia katika mstari wa 7.
- 1:5 halikuishinda Au “kupotosha ukweli”.
© 2017 Bible League International