馬可福音 6
Chinese Union Version Modern Punctuation (Traditional)
拿撒勒人厭棄耶穌
6 耶穌離開那裡,來到自己的家鄉,門徒也跟從他。 2 到了安息日,他在會堂裡教訓人。眾人聽見就甚稀奇,說:「這人從哪裡有這些事呢?所賜給他的是什麼智慧?他手所做的是何等的異能呢? 3 這不是那木匠嗎?不是馬利亞的兒子雅各、約西、猶大、西門的長兄嗎?他妹妹們不也是在我們這裡嗎?」他們就厭棄他[a]。 4 耶穌對他們說:「大凡先知,除了本地、親屬、本家之外,沒有不被人尊敬的。」 5 耶穌就在那裡不得行什麼異能,不過按手在幾個病人身上,治好他們。 6 他也詫異他們不信,就往周圍鄉村教訓人去了。
耶穌差遣十二門徒
7 耶穌叫了十二個門徒來,差遣他們兩個兩個地出去,也賜給他們權柄制伏汙鬼, 8 並且囑咐他們:「行路的時候不要帶食物和口袋,腰袋裡也不要帶錢,除了拐杖以外,什麼都不要帶; 9 只要穿鞋,也不要穿兩件褂子。」 10 又對他們說:「你們無論到何處,進了人的家,就住在那裡,直到離開那地方。 11 何處的人不接待你們,不聽你們,你們離開那裡的時候,就把腳上的塵土跺下去,對他們作見證。」 12 門徒就出去,傳道叫人悔改, 13 又趕出許多的鬼,用油抹了許多病人,治好他們。
約翰責備希律被斬
14 耶穌的名聲傳揚出來。希律王聽見了,就說:「施洗的約翰從死裡復活了,所以這些異能由他裡面發出來。」 15 但別人說是以利亞,又有人說是先知,正像先知中的一位。 16 希律聽見卻說:「是我所斬的約翰,他復活了。」 17 先是希律為他兄弟腓力的妻子希羅底的緣故,差人去拿住約翰,鎖在監裡,因為希律已經娶了那婦人。 18 約翰曾對希律說:「你娶你兄弟的妻子是不合理的。」 19 於是希羅底懷恨他,想要殺他,只是不能。 20 因為希律知道約翰是義人,是聖人,所以敬畏他,保護他,聽他講論就多照著行[b],並且樂意聽他。 21 有一天,恰巧是希律的生日,希律擺設筵席,請了大臣和千夫長並加利利做首領的。 22 希羅底的女兒進來跳舞,使希律和同席的人都歡喜。王就對女子說:「你隨意向我求什麼,我必給你。」 23 又對她起誓說:「隨你向我求什麼,就是我國的一半,我也必給你!」 24 她就出去對她母親說:「我可以求什麼呢?」她母親說:「施洗約翰的頭!」 25 她就急忙進去見王,求他說:「我願王立時把施洗約翰的頭放在盤子裡給我。」 26 王就甚憂愁,但因他所起的誓,又因同席的人,就不肯推辭, 27 隨即差一個護衛兵,吩咐拿約翰的頭來。護衛兵就去,在監裡斬了約翰, 28 把頭放在盤子裡,拿來給女子,女子就給她母親。 29 約翰的門徒聽見了,就來把他的屍首領去,葬在墳墓裡。
無牧的羊
30 使徒聚集到耶穌那裡,將一切所做的事、所傳的道全告訴他。 31 他就說:「你們來,同我暗暗地到曠野地方去歇一歇。」這是因為來往的人多,他們連吃飯也沒有工夫。 32 他們就坐船,暗暗地往曠野地方去。 33 眾人看見他們去,有許多認識他們的,就從各城步行,一同跑到那裡,比他們先趕到了。 34 耶穌出來,見有許多的人,就憐憫他們,因為他們如同羊沒有牧人一般,於是開口教訓他們許多道理。 35 天已經晚了,門徒進前來說:「這是野地,天已經晚了, 36 請叫眾人散開,他們好往四面鄉村裡去自己買什麼吃。」
給五千人吃飽
37 耶穌回答說:「你們給他們吃吧!」門徒說:「我們可以去買二十兩銀子的餅給他們吃嗎?」 38 耶穌說:「你們有多少餅,可以去看看。」他們知道了,就說:「五個餅,兩條魚。」 39 耶穌吩咐他們,叫眾人一幫一幫地坐在青草地上。 40 眾人就一排一排地坐下,有一百一排的,有五十一排的。 41 耶穌拿著這五個餅、兩條魚,望著天祝福,掰開餅,遞給門徒,擺在眾人面前,也把那兩條魚分給眾人。 42 他們都吃,並且吃飽了。 43 門徒就把碎餅碎魚收拾起來,裝滿了十二個籃子。 44 吃餅的男人共有五千。
耶穌履海
45 耶穌隨即催門徒上船,先渡到那邊伯賽大去,等他叫眾人散開。 46 他既辭別了他們,就往山上去禱告。 47 到了晚上,船在海中,耶穌獨自在岸上, 48 看見門徒因風不順搖櫓甚苦。夜裡約有四更天,就在海面上走,往他們那裡去,意思要走過他們去。 49 但門徒看見他在海面上走,以為是鬼怪,就喊叫起來, 50 因為他們都看見了他,且甚驚慌。耶穌連忙對他們說:「你們放心!是我,不要怕!」 51 於是到他們那裡,上了船,風就住了。他們心裡十分驚奇, 52 這是因為他們不明白那分餅的事,心裡還是愚頑。
53 既渡過去,來到革尼撒勒地方,就靠了岸。 54 一下船,眾人認得是耶穌, 55 就跑遍那一帶地方,聽見他在何處,便將有病的人用褥子抬到那裡。 56 凡耶穌所到的地方,或村中、或城裡、或鄉間,他們都將病人放在街市上,求耶穌只容他們摸他的衣裳穗子。凡摸著的人就都好了。
Marko 6
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yesu Aenda Kwenye Mji wa Kwao
(Mt 13:53-58; Lk 4:16-30)
6 Yesu akaondoka pale, na kwenda katika mji wa kwao; na wanafunzi wake wakamfuata. 2 Sabato ilipofika, alianza kufundisha katika sinagogi. Watu wengi walishangazwa walipomsikiliza. Wakasema, “Mtu huyu alipata wapi mambo haya? Alipata wapi hekima hii? Na anaifanyaje miujiza hii inayofanyika kwa mikono yake? 3 Je, yeye si yule seremala? Je, yeye si mwana wa Maria? Je, yeye si kaka yake Yakobo, Yusufu, Yuda, na Simoni? Je, dada zake hawaishi hapa katika mji wetu?” Kulikuwa na vikwazo vilivyowazuia wasimkubali.
4 Yesu akawaambia, “kila mtu humheshimu nabii isipokuwa watu wa mji wa kwao mwenyewe, jamaa zake mwenyewe na wale wa nyumbani mwake mwenyewe.” 5 Yesu hakuweza kufanya miujiza ya aina yoyote pale, isipokuwa aliweka mikono juu ya wagonjwa wachache na kuwaponya. 6 Naye akashangazwa na jinsi watu wa mji wa kwao mwenyewe walivyokosa kuwa na imani. Kisha Yesu alizunguka vijijini akiwafundisha watu.
Yesu Awatuma Kazi Mitume Wake
(Mt 10:1,5-15; Lk 9:1-6)
7 Akawaita kwake wanafunzi wake kumi na wawili, na akaanza kuwatuma wawili wawili. Akawapa uwezo wa kuwaweka huru watu kutoka pepo wachafu. 8 Akawapa amri kuwa wasichukue kitu chochote kwa ajili ya safari yao isipokuwa fimbo; hawakupaswa kuchukua mkate, mfuko, hata kubeba fedha kwenye mikanda yao. 9 Aliwaruhusu kuvaa makobazi lakini wasichukue kanzu ya pili. 10 Naye akawambia, “ikiwa mtu atawapa mahali pa kuishi mkae katika nyumba hiyo kwa muda wote mtakapokuwa katika mji ule msihamehame kutoka nyumba moja hadi nyingine. 11 Ikiwa hamtakaribishwa ama kusikilizwa katika mji wowote au mahali popote, kwa kuwaonya kunguteni mavumbi toka miguuni mwenu.”
12 Kwa hiyo mitume wakatoka na kuhubiri ili watu watubu. 13 Mitume wakafukuza mashetani wengi na kuwapaka mafuta ya mizeituni[a] wagonjwa wengi na kuwaponya.
Herode Adhani Yesu ndiye Yohana Mbatizaji
(Mt 14:1-12; Lk 9:7-9)
14 Mfalme Herode alisikia habari hii kwani umaarufu wa Yesu ulikuwa umeenea mahali pote. Watu wengine walisema, “Yohana Mbatizaji amefufuka kutoka wafu, ndiyo maana ana uwezo wa kufanya miujiza.”
15 Wengine wakasema, “Yeye ni Eliya.”
Wengine walisema, “Yeye ni nabii kama mmoja wa manabii wa zamani.”
16 Lakini Herode aliyasikia haya na kusema, “Yohana, yule mtu niliyemkata kichwa, amefufuka kutoka kifo.”
Yohana Mbatizaji Alivyouawa
17 Kwa kuwa Herode mwenyewe alikuwa ametoa amri ya kumkamata Yohana na kumweka gerezani. Alifanya hivi kwa sababu ya Herodia, mkewe Filipo kaka yake ambaye Herode alikuwa amemwoa. 18 Kwani Yohana alizidi kumwambia Herode, “Si halali kwako kisheria kumwoa mke wa kaka yako.” 19 Herodia alikuwa na kisa na Yohana. Hivyo alitaka auwawe, lakini hakuweza kumshawishi Herode kumuua Yohana. 20 Hii ni kwa sababu Herode alimhofu Yohana. Herode pia alifahamu ya kuwa Yohana alikuwa ni mtu mtakatifu na mwenye haki, hivyo akamlinda. Herode alimpomsikia Yohana, alisumbuka sana; lakini alifurahia kumsikiliza.
21 Lakini muda maalumu ukafika; katika siku ya kuzaliwa kwake. Herode aliandaa sherehe ya chakula cha jioni kwa maafisa mashuhuri wa baraza lake, maafisa wake wa kijeshi, na watu maarufu wa Galilaya. 22 Binti ya Herodia alipowasili ndani ya ukumbi alicheza na kumpendeza Herode na wageni aliowaalika katika sherehe hiyo.
Mfalme Herode akamwambia yule msichana, “Uniombe chochote unachotaka, nami nitakupa.” 23 Akamuahidi: “Nitakupa chochote utakachoniomba, hata nusu ya ufalme wangu!”
24 Naye akatoka na kumwambia mama yake, “Niombe kitu gani?”
Mama yake akasema, “Omba kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
25 Yule msichana mara moja aliharakisha kuingia ndani kwa mfalme na kuomba: “Nataka unipe sasa hivi kichwa cha Yohana Mbatizaji katika sinia.”
26 Mfalme alisikitika sana. Lakini kwa sababu ya viapo vyake alivyovifanya mbele ya wageni wake chakulani hakutaka kumkatalia ombi lake. 27 Kwa hiyo mfalme mara moja akamtuma mwenye kutekeleza hukumu za kifo akiwa na amri ya kukileta kichwa cha Yohana. Kisha akaenda kukikata kichwa cha Yohana, 28 na kukileta katika sinia na kumpa yule msichana, na msichana akampa mama yake. 29 Wanafunzi wa Yohana waliposikia haya walikuja na kuchukua mwili na kuuweka ndani ya kaburi.
Yesu Awalisha Watu Zaidi ya 5,000
(Mt 14:13-21; Lk 9:10-17; Yh 6:1-14)
30 Mitume walikusanyika kumzunguka Yesu, na wakamweleza yote waliyofanya na kufundisha. 31 Kisha Yesu akawaambia, “Njooni mnifuate peke yenu hadi mahali patulivu na palipo mbali na watu wengine ili mpumzike kidogo”, kwani pale walikuwepo watu wengi wakija na kutoka, nao hawakuwa na nafasi ya kula.
32 Kwa hiyo wakaondoka na mtumbwi kuelekea mahali patulivu na mbali na watu wakiwa peke yao. 33 Lakini watu wengi waliwaona wakiondoka na waliwafahamu wao ni kina nani; kwa hiyo walikimbilia pale kwa njia ya nchi kavu kutoka vitongoji vyote vilivyolizunguka eneo hilo wakafika kabla ya Yesu na wanafunzi wake. 34 Alipotoka katika mashua, Yesu aliona kundi kubwa, na akawahurumia, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasiokuwa na mchungaji, Kwa hiyo akaanza kuwafundisha mambo mengi.
35 Kwa sasa ilikuwa imekwisha kuwa jioni sana. Kwa hiyo wanafunzi wake walimwijia na kusema, “Hapa ni mahali palipojitenga na sasa hivi saa zimeenda. 36 Uruhusu watu waende zao, ili kwamba waende kwenye mashamba na vijiji vinavyozunguka na waweze kujinunulia kitu cha kula.”
37 Lakini kwa kujibu aliwaambia, “Ninyi wenyewe wapeni kitu cha kula.”
Wao Wakamwambia, “Je, twende kununua mikate yenye thamani ya mshahara wa mtu mmoja[b] wa miezi minane na kuwapa wale?”
38 Yesu akawambia, “Ni mikate mingapi mliyonayo? Nendeni mkaone.”
Walienda kuhesabu, wakarudi kwa Yesu na kusema, “Tunayo mikate mitano na samaki wawili.”
39 Kisha akawaagiza wakae chini kila mmoja kwenye majani mabichi kwa vikundi. 40 Nao wakakaa kwa vikundi vya watu mia na mmoja na vya watu hamsini.
41 Akachukua ile mikate mitano na samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akashukuru na akaimega. Akawapa wanafunzi wake ili wawape watu. Pia aligawanya samaki wawili miongoni mwao wote.
42 Wakala na wote wakatosheka. 43 Wakachukua mabaki ya vipande vya mikate na samaki na kujaza vikapu kumi na viwili. 44 Na idadi ya wanaume waliokula ile mikate ilikuwa 5,000.
Yesu Atembea Juu ya Maji
(Mt 14:22-33; Yh 6:16-21)
45 Mara Yesu akawafanya wafuasi wake wapande kwenye mashua na wamtangulie kwenda Bethsaida upande wa pili wa ziwa, wakati yeye akiliacha lile kundi liondoke. 46 Baada ya Yesu kuwaaga wale watu, alienda kwenye vilima kuomba.
47 Ilipotimia jioni, mashua ilikuwa katikati ya ziwa, na Yesu alikuwa peke yake katika nchi kavu. 48 Naye akawaona wanafunzi wake wakihangaika kupiga makasia, kwani upepo uliwapinga. Kati ya saa tisa na saa kumi na mbili asubuhi Yesu aliwaendea akitembea juu ya ziwa. Yeye akiwa karibu kuwapita, 49 wanafunzi wake wakamwona akitembea juu ya ziwa,[c] na wakafikiri kuwa alikuwa ni mzimu, ndipo walipopiga kelele. 50 Kwa kuwa wote walimwona, na wakaogopa. Mara tu alizungumza nao na kuwaambia, “Jipeni moyo! Ni mimi. Usiogope.” 51 Kisha alipanda kwenye mtumbwi pamoja nao, na upepo ukatulia. Wakashangaa kabisa, 52 kwa kuwa walikuwa bado hawajauelewa ule muujiza wa mikate. Kwani fahamu zao zilikuwa zimezibwa.
Yesu Awaponya Watu Wengi Wagonjwa
(Mt 14:34-36)
53 Walipolivuka ziwa, walifika Genesareti na wakaifunga mashua. 54 Walipotoka katika mashua, watu wakamtambua Yesu, 55 Wakakimbia katika lile jimbo lote na kuanza kuwabeba wagonjwa katika machela na kuwapeleka pale waliposikia kuwa Yesu yupo. 56 Na kila alipoenda vijijini, mijini na mashambani, waliwaweka wagonjwa kwenye masoko, na wakamsihi awaache waguse pindo la koti lake. Na wote walioligusa walipona.
Footnotes
- 6:13 kuwapaka mafuta ya mizeituni Mafuta ya mizeituni yalitumika kama dawa. Ilikuwa pia ni alama ya uponyaji wa Mungu aliopewa Yesu na baadaye wanafunzi wake na Roho Mtakatifu.
- 6:37 thamani ya mshahara wa mtu mmoja Kwa Kiyunani vipande 200 vya fedha vimelinganishwa na TKU kama kiasi cha mshahara wa mtu mmoja kwa miezi minane.
- 6:49 akitembea juu ya ziwa Watu zama za Marko waliamini kwamba mizimu isingeweza kutembea juu ya maji, lakini waliamini miungu wangeweza kutembea juu ya maji. Watu hao wangeshangaa kuona mitume wa Yesu wakiwa tayari kuamini kitu potovu kabla ya kuamini kuwa Yesu alisimama mbele yao ni Mungu kwani ametembea majini.
Copyright © 2011 by Global Bible Initiative
© 2017 Bible League International