Add parallel Print Page Options

Na,

“jiwe linalowafanya watu wajikwae
    na mwamba unaowafanya watu waanguke.”(A)

Walijikwaa kwa sababu hawakuutii ujumbe wa Mungu, na Mungu alisema hilo litatokea wasipotii.

Lakini ninyi ni watu mlioteuliwa, ni Ukuhani unaomtumikia Mfalme. Ninyi ni taifa takatifu nanyi ni watu wa Mungu. Yeye aliwaita Ili muweze kutangaza matendo yake yenye nguvu. Naye aliwaita mtoke gizani na mwingie katika nuru yake ya ajabu.

10 Kuna wakati hamkuwa watu,
    lakini sasa mmekuwa watu wa Mungu.
Kuna wakati hamkuoneshwa rehema,
    lakini sasa mmeoneshwa rehema za Mungu.

Read full chapter