Add parallel Print Page Options

Upendo Uwe Dira Yenu

13 Ninaweza kusema kwa lugha zingine, za wanadamu au za malaika. Lakini ikiwa sina upendo, mimi ni kengele yenye kelele na tuazi linalolia. Ninaweza kuwa na karama ya unabii, ninaweza kuzielewa siri zote na kujua kila kitu kinachopaswa kujulikana, na ninaweza kuwa na imani kuu kiasi cha kuhamisha milima. Lakini pamoja na haya yote, ikiwa sina upendo, mimi ni bure. Ninaweza kutoa kila kitu nilichonacho ili niwasaidie wengine na ninaweza hata kuutoa mwili wangu ili niweze kujisifu.[a] Lakini siwezi kupata chochote kwa kufanya haya yote ikiwa sina upendo.

Read full chapter

Footnotes

  1. 13:3 kuutoa mwili wangu ili niweze kujisifu Kwa maana ya kawaida, “ili nichomwe moto”, ambayo inapatikana katika nakala za kale na bora zaidi za Kiyunani. Baadhi ya nakala za kale za Kiyunani zimetumia hapa maneno “hata nikichomwa moto”, kwa maana hii ya “Kujisifu”, tazama 2 Kor 12:9-10.