Add parallel Print Page Options

Mungu alituambia kwa Habari ya Mwanae

Yesu Kristo ndiye aliyekuja. Alikuja kwa maji na damu.[a] Hakuja kwa maji peke yake. Lahasha, Yesu alikuja kwa vyote maji na damu. Na Roho atuambia kuwa hili ni kweli. Roho ndiye Kweli. Kwa hiyo kuna mashahidi watatu wanao tuambia habari za Yesu: Roho, Maji, na Damu. Mashuhuda hawa watatu wanakubaliana.

Read full chapter

Footnotes

  1. 5:6 maji na damu Inaweza kumaanisha Maji ya ubatizo wa Yesu Kristo, na damu aliyo imwaga pale msalabani.