Font Size
2 Yohana 1-3
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
2 Yohana 1-3
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
1 Salamu kutoka kwa mzee.[a]
Kwa mwanamke[b] aliyechaguliwa na Mungu na kwa wanawe.
Kweli kabisa, ninawapenda ninyi nyote. Na sio mimi peke yangu. Bali wote wanaoifahamu kweli[c] wanawapenda vile vile. 2 Tunawapenda kwa sababu ya kweli, ile kweli iliyomo ndani yetu. Kweli inayoendelea kuwemo ndani yetu milele yote.
3 Neema, rehema, na amani itakuwa pamoja nasi kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa mwanaye, Yesu Kristo, kwa kadri tuishivyo katika kweli na upendo.
Read full chapterFootnotes
- 1:1 mzee Huyu huenda alikuwa ni Mtume Yohana. “Mzee” ina maana ya mtu aliye mtu mzima au kiongozi maalumu katika kanisa (kama vile katika Tit 1:5).
- 1:1 mwanamke Inaweza kumaanisha mama. Au, katika barua hii, yaweza kumaanisha kanisa. Kama ni kanisa, basi watoto wake, wanaweza kuwa ndiyo wanakanisa. Pia katika mstari wa 5.
- 1:1 kweli Kweli au “habari njema” za Yesu Kristo zinazo waunganisha waamini wote pamoja.
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International