Add parallel Print Page Options

Salamu kutoka kwa mzee.[a]

Kwa mwanamke[b] aliyechaguliwa na Mungu na kwa wanawe.

Kweli kabisa, ninawapenda ninyi nyote. Na sio mimi peke yangu. Bali wote wanaoifahamu kweli[c] wanawapenda vile vile. Tunawapenda kwa sababu ya kweli, ile kweli iliyomo ndani yetu. Kweli inayoendelea kuwemo ndani yetu milele yote.

Neema, rehema, na amani itakuwa pamoja nasi kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa mwanaye, Yesu Kristo, kwa kadri tuishivyo katika kweli na upendo.

Read full chapter

Footnotes

  1. 1:1 mzee Huyu huenda alikuwa ni Mtume Yohana. “Mzee” ina maana ya mtu aliye mtu mzima au kiongozi maalumu katika kanisa (kama vile katika Tit 1:5).
  2. 1:1 mwanamke Inaweza kumaanisha mama. Au, katika barua hii, yaweza kumaanisha kanisa. Kama ni kanisa, basi watoto wake, wanaweza kuwa ndiyo wanakanisa. Pia katika mstari wa 5.
  3. 1:1 kweli Kweli au “habari njema” za Yesu Kristo zinazo waunganisha waamini wote pamoja.