Font Size
Luka 17:2-4
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Luka 17:2-4
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
2 Ingekuwa vizuri kwa mtu huyo kama jiwe la kusagia lingefungwa shingoni mwake, na akatupwa baharini, kuliko kusababisha mmojawapo wa wanyenyekevu hawa kutenda dhambi. 3 Hivyo iweni waangalifu!
Ikiwa ndugu au dada yako katika familia ya Mungu akikukosea, umwonye. Akitubu, msamehe. 4 Hata kama akikukosea mara saba katika siku moja, lakini akakuomba msamaha kila anapokukosea, msamehe.”
Read full chapter
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International