Add parallel Print Page Options

13 Kisha malaika pamoja na jeshi kubwa la mbinguni wakaanza kumsifu Mungu, wakisema:

14 “Atukuzwe Mungu juu mbinguni,
    na amani iwepo duniani
    kwa watu wote wanaompendeza.”

15 Malaika walipoondoka kurudi mbinguni, wale wachungaji wakaambiana wakisema, “Twendeni Bethlehemu, tukalione jambo hili lililotokea, ambalo Bwana ametujulisha.”

Read full chapter