Font Size
Luka 22:33-35
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Luka 22:33-35
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
33 Lakini Petro akamwambia Yesu, “Bwana, niko tayari kufungwa gerezani pamoja nawe. Hata kufa pamoja nawe!”
34 Lakini Yesu akasema, “Petro, asubuhi kabla jogoo hajawika, utakuwa umenikana mara tatu.”
Iweni Tayari kwa Matatizo
35 Kisha Yesu akawaambia mitume, “Kumbukeni nilipowatuma bila pesa, mkoba, wala viatu. Je, mlipungukiwa chochote?”
Mitume wakajibu, “Hapana.”
Read full chapter
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International