Luka 23
Neno: Bibilia Takatifu
23 Wote waliokuwepo katika Baraza wakasimama, wakampeleka Yesu kwa Pilato. 2 Wakafungua mashtaka yao kwa kusema: “Tumem wona huyu mtu akipotosha taifa letu. Yeye anawaambia watu wasi lipe kodi kwa Kaisari na kujiita kuwa yeye ni Kristo, mfalme.” 3 Basi Pilato akamwuliza Yesu, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Yesu akamjibu, “Ni kama ulivyosema.” 4 Pilato akawaambia maku hani wakuu na watu wote waliokuwapo, “Sioni sababu ya kutosha kumshtaki huyu mtu!” 5 Lakini wao wakakazana kusema, “Anawa chochea watu kwa mafundisho yake katika Yudea yote. Alianzia huko
Yesu Apelekwa Kwa Herode
6 Pilato aliposikia hayo akauliza, ‘Huyu mtu ni Mgalilaya?” 7 Alipofahamu kwamba Yesu alitoka katika mkoa unaotawaliwa na Herode, akampeleka kwa Herode ambaye wakati huo alikuwa Yerus alemu. 8 Herode alifurahi sana kumwona Yesu. Alikuwa amesikia habari zake na kwa muda mrefu akatamani sana kumwona; na pia alitegemea kumwona Yesu akifanya mwujiza. 9 Kwa hiyo akamwuliza Yesu maswali mengi, lakini yeye hakumjibu neno. 10 Wakati huo, makuhani wakuu na walimu wa sheria walikuwepo wakitoa mashtaka yao kwa nguvu sana. 11 Herode na maaskari wake wakamkashifu Yesu na kumzomea. Wakamvika vazi la kifahari, wakamrudisha kwa Pilato. 12 Siku hiyo, Herode na Pilato, ambao kabla ya hapo walikuwa maadui, wakawa marafiki.
Yesu Ahukumiwa Kifo
13 Pilato akawaita makuhani wakuu, viongozi na watu 14 aka waambia, “Mmemleta huyu mtu kwangu mkamshtaki kuwa anataka kuwa potosha watu. Nimemhoji mbele yenu, na sikuona kuwa ana hatia kutokana na mashtaka mliyoleta. 15 Hata Herode hakumwona na kosa lo lote; ndio sababu amemrudisha kwetu. Kama mnavyoona, mtu huyu hakufanya jambo lo lote linalostahili adhabu ya kifo. 16 Kwa hiyo nitaamuru apigwe viboko, kisha nimwachilie.” [ 17 Kwa kawaida, kila sikukuu ya Pasaka ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja].
18 Watu wote wakapiga kelele kwa pamoja, “ Auawe huyo! Tufungulie Baraba!” 19 Baraba alikuwa amefungwa gerezani kwa kuhusika katika fujo na mauaji yaliyotokea mjini. 20 Pilato ali taka sana kumwachilia Yesu kwa hiyo akasema nao tena. 21 Lakini wao wakazidi kupiga kelele, “Msulubishe! Msulubishe!” 22 Kwa mara ya tatu Pilato akasema nao tena, “Amefanya kosa gani huyu mtu? Sioni sababu yo yote ya kutosha kumhukumu adhabu ya kifo. Kwa hiyo nitaamuru apigwe viboko kisha nimwachilie .”
23 Lakini watu wakazidi kupiga kelele kwa nguvu na kusisi tiza kwamba Yesu asulubiwe. Hatimaye, kelele zao zikashinda. 24 Pilato akaamua kutoa hukumu waliyoitaka. 25 Akamwachia huru yule mtu aliyekuwa amefungwa gerezani kwa kuhusika katika fujo na mauaji yaliyotokea mjini; akamkabidhi Yesu mikononi mwao, wamfa nyie watakavyo. Yesu Asulubiwa Msalabani
26 Na walipokuwa wakienda naye, wakamkamata mtu mmoja ait waye Simoni wa Kirene aliyekuwa anatoka mashambani. Wakambebesha msalaba, wakamlazimisha atembee nyuma ya Yesu. 27 Umati mkubwa wa watu wakamfuata Yesu ikiwa ni pamoja na wanawake waliokuwa wakimlilia na kuomboleza. 28 Lakini Yesu akawageukia, akawaam bia, “Enyi akina mama wa Yerusalemu, msinililie mimi bali jilil ieni ninyi wenyewe na watoto wenu. 29 Kwa maana wakati utafika ambapo mtasema, ‘Wamebarikiwa akina mama tasa, ambao hawakuzaa na matiti yao hayakunyonyesha.’ 30 Na watu wataiambia milima, ‘Tuangukieni’ na vilima, ‘Tufunikeni’. 31 Kwa maana kama watu wanafanya mambo haya wakati mti ni mbichi, itakuwaje utakapo kauka?”
32 Wahalifu wengine wawili pia walipelekwa wakasulubiwe pamoja na Yesu. 33 Walipofika mahali paitwapo “Fuvu la kichwa,” wakamsulubisha Yesu hapo pamoja na hao wahalifu; mmoja upande wa kulia na mwingine upande wa kushoto.
34 Yesu akasema, “Baba, uwasamehe, kwa maana hawajui wali tendalo!” Wakagawana nguo zake kwa kupiga kura. 35 Watu wakasi mama pale wakimwangalia. Viongozi wa Wayahudi wakamdhihaki wakisema, “Si aliokoa wengine! Ajiokoe mwenyewe basi, kama kweli yeye ndiye Kristo wa Mungu, Mteule wake.” 36 Askari nao wakam wendea, wakamdhihaki. Wakamletea siki anywe, 37 wakamwambia, “Kama wewe ni mfalme wa Wayahudi, jiokoe tuone.”
38 Na maandishi haya yaliwekwa kwenye msalaba juu ya kichwa chake: “HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI.” 39 Mmoja kati ya wale wahalifu waliosulubiwa naye akamtu kana, akasema: “Wewe si ndiye Kristo? Jiokoe na utuokoe na sisi.”
40 Yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake, akisema, “Wewe humwogopi hata Mungu! Wote tumehukumiwa adhabu sawa. 41 Adhabu yetu ni ya haki kwa sababu tunaadhibiwa kwa makosa tuliyofanya. Lakini huyu hakufanya kosa lo lote.” 42 Kisha akasema, “Bwana Yesu unikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.” 43 Yesu akam jibu, “Nakuambia kweli, leo hii utakuwa pamoja nami peponi.”
Yesu Afa Msalabani
44 Ilikuwa kama saa sita mchana. Kukawa na giza nchi nzima mpaka saa tisa, 45 kwa maana jua liliacha kutoa nuru. Pazia la Hekalu likapasuka katikati kukawa na vipande viwili. 46 Yesu akapaza sauti akasema, “Baba, mikononi mwako ninaikabidhi roho yangu.” Baada ya kusema haya, akakata roho.
47 Mkuu wa maaskari alipoona yaliyotokea, akamsifu Mungu akasema, “Hakika, mtu huyu alikuwa mwenye haki.” 48 Na watu wote waliokuwa wamekusanyika hapo kushuhudia tukio hilo walipoy aona hayo, walirudi makwao wakijipiga vifua kwa huzuni.
49 Lakini wale wote waliomfahamu, pamoja na wanawake wal iokuwa wamemfuata kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiyata zama mambo haya. Yesu Azikwa Kaburini
50 Kulikuwa na mtu mmoja jina lake Yusufu mwenyeji wa mji wa Arimathaya, ambaye alikuwa anautazamia Ufalme wa Mungu. Yeye ali kuwa mjumbe wa Baraza na pia alikuwa mtu mwema na mwenye kuheshi mika. 51 Lakini yeye hakukubaliana na wajumbe wenzake katika uamuzi wao na kitendo cha kumsulubisha Yesu. 52 Basi, Yusufu alikwenda kwa Pilato akaomba apewe mwili wa Yesu. 53 Akaushusha kutoka msalabani, akauzungushia sanda, akauhifadhi katika kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kaburi hilo lilikuwa halijatumika bado. 54 Siku hiyo ilikuwa Ijumaa, Siku ya Maandalizi, na sabato ilikuwa karibu ianze. 55 Wale wanawake waliokuwa wamefuatana na Yesu kutoka Galilaya wakamfuata Yusufu, wakaliona kaburi na jinsi mwili wa Yesu ulivyolazwa humo. 56 Kisha wakarudi nyumbani wakaandaa marashi na manukato ya kuupaka huo mwili. Lakini waka pumzika siku ya sabato kama ilivyoamriwa.
Luke 23
New Century Version
Pilate Questions Jesus
23 Then the whole group stood up and led Jesus to Pilate.[a] 2 They began to accuse Jesus, saying, “We caught this man telling things that mislead our people. He says that we should not pay taxes to Caesar, and he calls himself the Christ, a king.”
3 Pilate asked Jesus, “Are you the king of the Jews?”
Jesus answered, “Those are your words.”
4 Pilate said to the leading priests and the people, “I find nothing against this man.”
5 They were insisting, saying, “But Jesus makes trouble with the people, teaching all around Judea. He began in Galilee, and now he is here.”
Pilate Sends Jesus to Herod
6 Pilate heard this and asked if Jesus was from Galilee. 7 Since Jesus was under Herod’s authority, Pilate sent Jesus to Herod, who was in Jerusalem at that time. 8 When Herod saw Jesus, he was very glad, because he had heard about Jesus and had wanted to meet him for a long time. He was hoping to see Jesus work a miracle. 9 Herod asked Jesus many questions, but Jesus said nothing. 10 The leading priests and teachers of the law were standing there, strongly accusing Jesus. 11 After Herod and his soldiers had made fun of Jesus, they dressed him in a kingly robe and sent him back to Pilate. 12 In the past, Pilate and Herod had always been enemies, but on that day they became friends.
Jesus Must Die
13 Pilate called the people together with the leading priests and the rulers. 14 He said to them, “You brought this man to me, saying he makes trouble among the people. But I have questioned him before you all, and I have not found him guilty of what you say. 15 Also, Herod found nothing wrong with him; he sent him back to us. Look, he has done nothing for which he should die. 16 So, after I punish him, I will let him go free.” [17 Every year at the Passover Feast, Pilate had to release one prisoner to the people.][b]
18 But the people shouted together, “Take this man away! Let Barabbas go free!” 19 (Barabbas was a man who was in prison for his part in a riot in the city and for murder.)
20 Pilate wanted to let Jesus go free and told this to the crowd. 21 But they shouted again, “Crucify him! Crucify him!”
22 A third time Pilate said to them, “Why? What wrong has he done? I can find no reason to kill him. So I will have him punished and set him free.”
23 But they continued to shout, demanding that Jesus be crucified. Their yelling became so loud that 24 Pilate decided to give them what they wanted. 25 He set free the man who was in jail for rioting and murder, and he handed Jesus over to them to do with him as they wished.
Jesus Is Crucified
26 As they led Jesus away, Simon, a man from Cyrene, was coming in from the fields. They forced him to carry Jesus’ cross and to walk behind him.
27 A large crowd of people was following Jesus, including some women who were sad and crying for him. 28 But Jesus turned and said to them, “Women of Jerusalem, don’t cry for me. Cry for yourselves and for your children. 29 The time is coming when people will say, ‘Blessed are the women who cannot have children and who have no babies to nurse.’ 30 Then people will say to the mountains, ‘Fall on us!’ And they will say to the hills, ‘Cover us!’ 31 If they act like this now when life is good, what will happen when bad times come?”[c]
32 There were also two criminals led out with Jesus to be put to death. 33 When they came to a place called the Skull, the soldiers crucified Jesus and the criminals—one on his right and the other on his left. 34 Jesus said, “Father, forgive them, because they don’t know what they are doing.”[d]
The soldiers threw lots to decide who would get his clothes. 35 The people stood there watching. And the leaders made fun of Jesus, saying, “He saved others. Let him save himself if he is God’s Chosen One, the Christ.”
36 The soldiers also made fun of him, coming to Jesus and offering him some vinegar. 37 They said, “If you are the king of the Jews, save yourself!” 38 At the top of the cross these words were written: this is the king of the jews.
39 One of the criminals on a cross began to shout insults at Jesus: “Aren’t you the Christ? Then save yourself and us.”
40 But the other criminal stopped him and said, “You should fear God! You are getting the same punishment he is. 41 We are punished justly, getting what we deserve for what we did. But this man has done nothing wrong.” 42 Then he said, “Jesus, remember me when you come into your kingdom.”
43 Jesus said to him, “I tell you the truth, today you will be with me in paradise.”[e]
Jesus Dies
44 It was about noon, and the whole land became dark until three o’clock in the afternoon, 45 because the sun did not shine. The curtain in the Temple[f] was torn in two. 46 Jesus cried out in a loud voice, “Father, I give you my life.” After Jesus said this, he died.
47 When the army officer there saw what happened, he praised God, saying, “Surely this was a good man!”
48 When all the people who had gathered there to watch saw what happened, they returned home, beating their chests because they were so sad. 49 But those who were close friends of Jesus, including the women who had followed him from Galilee, stood at a distance and watched.
Joseph Takes Jesus’ Body
50 There was a good and religious man named Joseph who was a member of the council. 51 But he had not agreed to the other leaders’ plans and actions against Jesus. He was from the town of Arimathea and was waiting for the kingdom of God to come. 52 Joseph went to Pilate to ask for the body of Jesus. 53 He took the body down from the cross, wrapped it in cloth, and put it in a tomb that was cut out of a wall of rock. This tomb had never been used before. 54 This was late on Preparation Day, and when the sun went down, the Sabbath day would begin.
55 The women who had come from Galilee with Jesus followed Joseph and saw the tomb and how Jesus’ body was laid. 56 Then the women left to prepare spices and perfumes.
On the Sabbath day they rested, as the law of Moses commanded.
Footnotes
- 23:1 Pilate Pontius Pilate was the Roman governor of Judea from a.d. 26 to a.d. 36.
- 23:17 Every . . . people. Some Greek copies do not contain the bracketed text.
- 23:31 If . . . come? Literally, “If they do these things in the green tree, what will happen in the dry?”
- 23:34 Jesus . . . doing.” Some Greek copies do not have this first part of verse 34.
- 23:43 paradise Another word for heaven.
- 23:45 curtain in the Temple A curtain divided the Most Holy Place from the other part of the Temple, the special building in Jerusalem where God commanded the Jewish people to worship him.
Copyright © 1989 by Biblica
The Holy Bible, New Century Version®. Copyright © 2005 by Thomas Nelson, Inc.
