Mfano Wa Taa

16 “Ni nani anayewasha taa kisha akaifunika, au akaiweka uvunguni, badala ya kuiweka mahali ambapo mwanga wake utaonekana? 17 Hakuna siri ambayo haitafichuliwa, wala hakuna jambo lililo fichika ambalo halitajulikana na kuwekwa wazi. 18 Kwa hiyo muwe waangalifu mnaposikiliza, kwa sababu, yeye aliye na kitu ataonge zewa, naye ambaye hana, atanyang’anywa hata kile anachodhania anacho.”

Read full chapter