Font Size
Marko 9:2-4
Neno: Bibilia Takatifu
Marko 9:2-4
Neno: Bibilia Takatifu
Yesu Ageuka Sura
2 Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohana akawapeleka juu ya mlima mrefu ambapo walikuwa faraghani, peke yao. Na huko, wakiwa wanamtazama, Yesu akageuka sura. 3 Mavazi yake yakametameta kwa weupe, yakang’aa, yakawa meupe kuliko ambavyo dobi ye yote duniani angaliweza kuyang’aarisha. 4 Musa na Eliya wakawatokea nao walikuwa wakizungumza na Yesu.
Read full chapter
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Copyright © 1989 by Biblica