Yesu Ajaribiwa Na Shetani

Kisha Yesu akaongozwa na Roho Mtakatifu mpaka nyikani ili akajaribiwe na shetani. Akakaa huko siku arobaini akifunga, pasipo kula kitu cho chote mchana na usiku, hatimaye akaona njaa. Ndipo shetani akamjia akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.”

Read full chapter