Add parallel Print Page Options

15 Viongozi wa Kiyahudi wakawaambia mitume watoke nje ya chumba cha mkutano wa baraza. Kisha viongozi wakajadiliana wao wenyewe juu ya nini wanachopaswa kufanya. 16 Wakaulizana, “Tuwafanye nini watu hawa? Kila mtu katika Yerusalemu anajua kuhusu muujiza walioufanya kama ishara kutoka kwa Mungu. Ni dhahiri, hatuwezi kusema muujiza huo haukufanyika. 17 Lakini ni lazima tuwatishe ili wasiendelee kuwaambia watu kutumia jina lile.[a] Ili tatizo hili lisisambae miongoni mwa watu.”

Read full chapter

Footnotes

  1. 4:17 jina lile Yaani, jina la Yesu. Viongozi wa Kiyahudi walikwepa kutamka jina lake. Tazama Lk 15:2 na Mdo 5:28.