19 Wakaja watu kutoka Antiokia na Ikonio wakawashawishi wale watu, wakampiga Paulo kwa mawe, wakamkokota hadi nje ya mji, wakidhani amekufa. 20 Lakini waamini walipokusanyika kumzunguka, aliamka, akarudi nao mjini. Kesho yake akaondoka na Barnaba wakaenda mpaka Derbe.

Paulo Na Barnaba Warudi Antiokia

21 Walipokwisha hubiri Habari Njema katika mji ule na watu wengi wakaamini wakawa wanafunzi, walirudi Listra na Ikonio na Antiokia.

Read full chapter