Add parallel Print Page Options

26 Hivyo ikiwa Shetani anayafukuza mashetani[a] yake mwenyewe, anapigana kinyume chake yeye mwenyewe, na ufalme wake hautaishi. 27 Mnasema kuwa ninatumia nguvu za Shetani kuyatoa mashetani. Ikiwa hiyo ni kweli, sasa ni nguvu gani watu wenu hutumia wanapoyafukuza mashetani? Hivyo watu wenu wenyewe watathibitisha kuwa mmekosea. 28 Lakini ninatumia nguvu ya Roho wa Mungu kuyafukuza mashetani, na hili linaonesha kuwa Ufalme wa Mungu umekuja kwenu.

Read full chapter

Footnotes

  1. 12:26 ikiwa Shetani … mashetani Kwa maana ya kawaida, “ikiwa Shetani atamfukuza Shetani.”