Font Size
Mathayo 6:6-8
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Mathayo 6:6-8
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
6 Lakini unapoomba, unapaswa kuingia katika chumba chako cha ndani na ufunge mlango. Kisha mwombe Baba yako aliye mahali pa siri. Yeye anayaona mambo yanayofanyika katika siri na hivyo atakupa thawabu.
7 Na unapoomba usiwe kama watu wasiomjua Mungu. Wao kila wanapoomba wanarudia maneno yale yale, tena na tena, wakidhani kuwa wanapoyarudia maneno hayo mara nyingi watasikiwa na Mungu na kujibiwa maombi yao. 8 Msiwe kama wao. Baba yenu anajua yale mnayohitaji kabla hamjamwomba.
Read full chapter
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International