Font Size
Tito 3:8-10
Neno: Bibilia Takatifu
Tito 3:8-10
Neno: Bibilia Takatifu
8 Neno hili ni kweli kabisa. Ninataka uyatilie mkazo mambo haya ili wale waliomwamini Mungu waone umuhimu wa kutenda mema wakati wote, maana mambo haya ni mazuri na tena ni ya manufaa kwa watu.
9 Lakini jiepushe na ubishi wa kipuuzi: mambo kama orodha ndefu za vizazi na ubishi na ugomvi juu ya sheria; haya hayana maana wala hayamsaidii mtu ye yote. 10 Mtu anayesababisha mafarakano, muonye mara ya kwanza na mara ya pili. Baada ya hapo, usijishughulishe naye tena.
Read full chapter
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Copyright © 1989 by Biblica