15 Wale wafanya biashara wa bidhaa hizo waliopata utajiri wao kwake watasimama mbali kabisa kwa kuogopa mateso yake, nao watalia na kuomboleza kwa nguvu wakisema, 16 ‘Ole wako! Ole wako! mji mkuu, ulikuwa umevikwa mavazi ya kitani safi, rangi ya zambarau na nyekundu, uking’aa kwa dhahabu na vito vya thamani na lulu! 17 Katika muda wa saa moja utajiri wote huu umeharibiwa!’ Manahodha wote, mabaharia na wote wasafirio baharini na wote wafanyao kazi melini watasimama mbali kabisa.

Read full chapter