18 Watakapoona moshi wake wakati mji ukiteketezwa watalia wakisema, ‘Kuna mji gani ambao umepata kuwa kama mji huu mkuu?’ 19 Nao watajimwagia vumbi vichwani na kulia na kuomboleza wakisema, ‘Ole wako, Ole wako mji mkuu, mji ambapo wote wenye meli baharini walitajirika kwa mali yake! Maana katika saa moja tu umeteketezwa. 20 Fura hini juu yake, enyi mbingu, watakatifu na mitume na manabii; Kwa kuwa Mungu ameuhukumu kwa ajili yenu!”’

Read full chapter