Add parallel Print Page Options

14 “Ee Babeli, mambo mazuri uliyoyataka yamekuacha.
Utajiri wako wote na vitu vya fahari vimetoweka.
    Hautakuwa navyo tena.”

15 Wafanya biashara wataogopa mateso yake na watakaa mbali naye. Hawa ni wale waliotajirika kwa kumwuzia vitu hivyo. Watalia na kuhuzunika. 16 Watasema:

“Inatisha! Inatisha kwa mji mkuu!
    Alivalishwa kitani safi;
    alivaa zambarau na nguo nyekundu.
    Alikuwa anang'aa kwa sababu ya dhahabu, vito na lulu!

Read full chapter