Font Size
Ufunuo 18:20-22
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Ufunuo 18:20-22
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
20 Ufurahi kwa sababu ya hili, Ee mbingu!
Furahini, watakatifu wa Mungu, mitume na manabii!
Mungu amemhukumu kwa sababu ya kile alichowatendea ninyi.”
21 Kisha malaika mwenye nguvu akainua jiwe kubwa. Jiwe hili lilikuwa kubwa kama jiwe kubwa la kusagia. Malaika akalitupia jiwe baharini na kusema:
“Hivyo ndivyo mji mkuu Babeli utakavyotupwa chini.
Hautaonekana tena.
22 Ee Babeli, muziki wa wapigao vinanda na ala zingine waimbaji na tarumbeta,
hautasikika tena ndani yako.
Hakuna mfanyakazi afanyaye kazi atakayeonekana ndani yako tena.
Sauti ya jiwe la kusagia haitasikika ndani yako tena.
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International