Font Size
Ufunuo 19:5-7
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Ufunuo 19:5-7
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
5 Sauti ikatoka kwenye kiti cha enzi na kusema:
“Msifuni Mungu wetu,
ninyi nyote mnaomtumikia!
Msifuni Mungu wetu,
ninyi nyote mlio wadogo na wakubwa mnaomheshimu!”
6 Kisha nikasikia kitu kilichosikika kama kundi kubwa la watu. Kilikuwa na kelele kama mawimbi ya bahari au radi. Watu walikuwa wakisema:
“Haleluya!
Bwana Mungu wetu anatawala.
Ndiye Mwenye Nguvu, Mungu Mwenyezi.
7 Tushangilie na kufurahi na
kumpa Mungu utukufu!
Mpeni Mungu utukufu, kwa sababu arusi ya Mwanakondoo imewadia.
Na bibi arusi wa Mwanakondoo amekwisha jiandaa.
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International