Font Size
Ufunuo 21:6-8
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Ufunuo 21:6-8
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
6 Akaniambia, “Imekwisha! Mimi ni Alfa na Omega,[a] Mwanzo na Mwisho. Kila mwenye kiu nitampa bure maji kutoka kwenye chemichemi ya maji ya uzima. 7 Wale wote watakaoshinda watapokea yote haya. Na nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watoto wangu. 8 Lakini waoga, wanaokataa kuniamini, wafanyao mambo ya kuchukiza, wauaji, wazinzi, wachawi, waabuduo sanamu na waongo, nitawatupa katika ziwa linalowaka moto. Hii ni mauti ya pili.”
Read full chapterFootnotes
- 21:6 Alfa na Omega Herufi ya kwanza na ya mwisho katika mfumo wa herufi wa Kiyunani, hapa inamaanisha “wa Kwanza na wa Mwisho”. Pia katika 22:13.
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International