Font Size
Ufunuo 6:5-7
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Ufunuo 6:5-7
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
5 Mwanakondoo alipoufungua muhuri wa tatu. Nilisikia kiumbe mwenye uhai wa tatu akisema, “Njoo!” Nilipotazama nilimwona farasi mweusi mbele yangu. Aliyekuwa anamwendesha farasi huyu alikuwa na mizani mkononi mwake. 6 Kisha nilisikia kitu kilichosikika kama sauti ikitokea pale walipokuwa viumbe wenye uhai wanne. Kikisema, “Kilo moja[a] ya ngano au kilo tatu ya shayiri itagharimu mshahara wote wa siku moja. Lakini usiharibu upatikanaji wa mafuta ya mzeituni na divai!”
7 Mwanakondoo alipoufungua muhuri wa nne nilisikia sauti ya kiumbe wa nne mwenye uhai akisema, “Njoo!”
Read full chapterFootnotes
- 6:6 Kilo “Kibaba au posho,” kiasi cha gawio la nafaka kwa ajili ya askari. Ni kama kilo moja.
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International