Font Size
Warumi 15:7-9
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Warumi 15:7-9
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
7 Kristo aliwakaribisha ninyi, hivyo nanyi mkaribishane ninyi kwa ninyi. Hili litaleta heshima[a] kwa Mungu. 8 Ndiyo, haya ndiyo maneno yangu kwenu kwamba Kristo alifanyika mtumishi wa Wayahudi ili kuonesha kuwa Mungu amefanya yale aliyowaahidi baba zao wakuu. 9 Na pia alifanya hivi ili wale wasio Wayahudi waweze kumsifu Mungu kwa rehema anazowapa. Maandiko yanasema,
“Hivyo nitakushukuru wewe katikati ya watu wa mataifa mengine;
Nitaliimbia sifa jina lako.”(A)
Footnotes
- 15:7 heshima Au “utukufu”. Tazama Utukufu katika Orodha ya Maneno.
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International