Font Size
Yohana 20:11-13
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yohana 20:11-13
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
11 Lakini Mariamu akabaki amesimama nje ya kaburi, akilia. Aliinama na kuchungulia ndani ya kaburi alipokuwa akilia. 12 Mle ndani akawaona malaika wawili waliovaa nguo nyeupe na wameketi mahali ulipokuwa mwili wa Yesu. Mmoja amekaa sehemu kilipolazwa kichwa na mwingine aliketi sehemu miguu ilipokuwa imewekwa.
13 Malaika wakamwuliza Mariamu, “Mwanamke, kwa nini unalia?”
Mariamu akajibu, “Wameuondoa mwili wa Bwana wangu, na sijui wameuweka wapi.”
Read full chapter
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International