Font Size
Yohana 20:15-17
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yohana 20:15-17
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
15 Akamwuliza, “Mwanamke, kwa nini unalia? Je, unamtafuta nani?”
Yeye alifikiri kuwa huyu alikuwa ni mtunzaji wa bustani. Hivyo akamwambia, “Je, ulimwondoa Bwana? Niambie umemweka wapi. Nami nitaenda kumchukua.” 16 Yesu akamwita, “Mariamu.”
Mariamu akamgeukia na kumwambia kwa Kiaramu, “Raboni”, (hii ikiwa na maana “Mwalimu”).
17 Yesu akamwambia, “Hupaswi kunishika! Kwani bado sijapaa kwenda huko juu kwa Baba yangu. Lakini nenda ukawaambie wafuasi wangu[a] maneno haya: ‘Ninarudi kwa Baba yangu ambaye pia ni Baba yenu. Ninarudi kwa Mungu wangu ambaye pia ni Mungu wenu.’”
Read full chapterFootnotes
- 20:17 wafuasi wangu Yaani, “ndugu zangu”.
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International