Font Size
Yohana 20:17-19
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yohana 20:17-19
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
17 Yesu akamwambia, “Hupaswi kunishika! Kwani bado sijapaa kwenda huko juu kwa Baba yangu. Lakini nenda ukawaambie wafuasi wangu[a] maneno haya: ‘Ninarudi kwa Baba yangu ambaye pia ni Baba yenu. Ninarudi kwa Mungu wangu ambaye pia ni Mungu wenu.’”
18 Mariamu Magdalena akaenda kwa wafuasi na kuwaambia, “Nimemwona Bwana!” Naye akawaeleza yale Yesu aliyomwambia.
Yesu Awatokea Wafuasi Wake
(Mt 28:16-20; Mk 16:14-18; Lk 24:36-49)
19 Ilikuwa siku ya Jumapili, na jioni ile wafuasi walikuwa pamoja. Nao walikuwa wamefunga milango kwa kuwa waliwaogopa viongozi wa Wayahudi. Ghafla, Yesu akawa amesimama pale katikati yao. Akasema, “Amani iwe nanyi!”
Read full chapterFootnotes
- 20:17 wafuasi wangu Yaani, “ndugu zangu”.
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International