Font Size
Yohana 8:11-13
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yohana 8:11-13
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
11 Mwanamke akajibu, “Hakuna hata mmoja aliyenihukumu, Bwana.”[a]
Kisha Yesu akasema, “Hata mimi sikuhukumu. Unaweza kwenda sasa, lakini usifanye dhambi tena.”
Yesu ni Nuru ya Ulimwengu
12 Baadaye Yesu akazungumza tena na watu. Akasema, “Mimi ndiye nuru ya ulimwengu. Yeyote atakayenifuata mimi hataishi gizani kamwe. Atakuwa na nuru inayoleta uzima.”
13 Lakini Mafarisayo wakamwambia Yesu, “Unapojishuhudia mwenyewe, unakuwa ni wewe peke yako unayethibitisha kuwa mambo haya ni kweli. Hivyo hatuwezi kuyaamini unayosema.”
Read full chapterFootnotes
- 8:11 Nakala za kale na bora za Kiyunani hazina mistari 7:53-8:11. Nakala zingine zina sehemu hii katika maeneo mbalimbali kitabuni.
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International