Font Size
Yohana 8:6-8
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yohana 8:6-8
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
6 Watu hao waliyasema haya ili kumtega Yesu. Walitaka kumkamata akisema mambo tofauti ili wapate mashtaka ya kumshitaki. Lakini Yesu akainama chini na kuanza kuandika kwenye udongo kwa kidole chake. 7 Viongozi wa Kiyahudi waliendelea kumuuliza swali lao hilo. Naye akainuka na kusema, “Yeyote hapa ambaye hajawahi kutenda dhambi awe wa kwanza kumponda jiwe mwanamke huyu.” 8 Kisha Yesu akainama chini tena na kuendelea kuandika katika udongo.
Read full chapter
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International