Font Size
Yohana 8:9-11
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yohana 8:9-11
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
9 Waliposikia hayo, wale watu walianza kuondoka mmoja baada ya mwingine. Wanaume wazee wakitangulia kwanza, na kisha wengine wakifuata. Wakamwacha Yesu peke yake na yule mwanamke akiwa amesimama mbele yake. 10 Kisha Yesu akainua uso wake tena na kumwambia, “Wameenda wapi hao wote? Je, hakuna aliyekuhukumu kuwa una hatia?” 11 Mwanamke akajibu, “Hakuna hata mmoja aliyenihukumu, Bwana.”[a]
Kisha Yesu akasema, “Hata mimi sikuhukumu. Unaweza kwenda sasa, lakini usifanye dhambi tena.”
Read full chapterFootnotes
- 8:11 Nakala za kale na bora za Kiyunani hazina mistari 7:53-8:11. Nakala zingine zina sehemu hii katika maeneo mbalimbali kitabuni.
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International