Mimi Yuda, mtumishi wa Yesu Kristo, na ndugu yake Yakobo. Nawaandikia wale walioitwa na kupendwa na Mungu Baba na kulindwa na Yesu Kristo. Ninawatakieni rehema, amani na upendo tele.

Hukumu Ya Watu Wasiomcha Mungu

Wapendwa, ingawa nilikuwa na hamu kubwa kuwaandikieni kuhusu wokovu wetu, nimeona ni muhimu niwaandikieni nikiwasihi mwendelee kuipigania kwa nguvu imani ambayo Mungu amewakabidhi watakatifu mara moja tu kwa wakati wote.

Read full chapter