Font Size
Yuda 1-3
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yuda 1-3
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
1 Salamu kutoka kwa Yuda, mtumwa wa Yesu Kristo na ndugu yake Yakobo. Kwa wale waliochaguliwa na kupendwa na Mungu Baba na kulindwa ndani ya Yesu Kristo.
2 Rehema, amani na upendo viwe pamoja nanyi zaidi na zaidi.
Mungu Atawaadhibu Watendao Mabaya
3 Rafiki wapendwa, nilitaka sana kuwaandikia kuhusu wokovu tunaoshiriki pamoja. Lakini nimejisikia kuwa ni muhimu niwaandikie kuhusu kitu kingine: Ninataka kuwatia moyo kuipigania kwa nguvu imani ambayo Mungu aliwapa watakatifu wake. Mungu alitoa imani hii mara moja na ni nzuri wakati wote.
Read full chapter
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International