Previous Prev Day Next DayNext

Bible in 90 Days

An intensive Bible reading plan that walks through the entire Bible in 90 days.
Duration: 88 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Yuda - Ufunua wa Yohana 17

Mimi Yuda, mtumishi wa Yesu Kristo, na ndugu yake Yakobo. Nawaandikia wale walioitwa na kupendwa na Mungu Baba na kulindwa na Yesu Kristo. Ninawatakieni rehema, amani na upendo tele.

Hukumu Ya Watu Wasiomcha Mungu

Wapendwa, ingawa nilikuwa na hamu kubwa kuwaandikieni kuhusu wokovu wetu, nimeona ni muhimu niwaandikieni nikiwasihi mwendelee kuipigania kwa nguvu imani ambayo Mungu amewakabidhi watakatifu mara moja tu kwa wakati wote. Hii ni kwa sababu watu wasiomcha Mungu ambao tangu zamani wamekwisha kuandikiwa hukumu hii, wamejiingiza miongoni mwenu kwa siri. Hawa ni watu ambao wanapotosha neema ya Mungu wetu na kuitumia kama kisingizio cha kutenda maovu. Wao wanamkana Yesu Kristo ambaye pekee ndiye Mkuu na Bwana wetu.

Sasa nataka kuwakumbusha jambo ambalo tayari mnalijua: kwamba, Bwana aliwaokoa watu wake kutoka Misri, lakini baadaye akawaangamiza wale ambao hawakuamini. Na malaika ambao hawaku tunza madaraka yao wakaacha maskani yao halisi; hao amewafungia gizani kwa minyororo ya milele hadi wahukumiwe katika siku ile kuu. Vivyo hivyo watu wa Sodoma na Gomora na miji ya kando kando yake ambao hali kadhalika walifanya uasherati na kujifurah isha katika matendo yaliyo kinyume cha maumbile, waliadhibiwa kwa moto wa milele kama fundisho kwa watu wote.

Ndivyo walivyo hawa watu. Ndoto zao huwaongoza wachafue miili yao, wasitii mamlaka; na watukane viumbe watakatifu walioko mbinguni. Lakini hata Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na shetani kuhusu mwili wa Musa, hakuthubutu kutamka hukumu juu ya shetani, bali alisema, “Bwana akukemee!” 10 Lakini hawa watu hushutumu cho chote wasichokielewa; na yale mambo wanayotambua kwa asili, kama wanyama ambao hawawezi kujizuia kwa kutumia fikira, hayo ndio yanayowaangamiza. 11 Ole wao! Kwa maana watu hao wamefuata mfano wa Kaini, na kama Balaamu wako tayari kufanya lo lote kwa ajili ya fedha; na kama Kora wamejiangamiza wenyewe kwa kumwasi Mungu.

12 Watu hawa ni madoa katika karamu zenu za ushirika. Wanak ula nanyi bila kuwa na kiasi, wakicheka na kujishibisha na kunywa bila kujali wengine. Wao ni kama mawingu yanayochukuliwa na upepo huku na huku pasipo kuleta mvua; ni kama miti ya kiangazi iliy opukutika bila kuwa na matunda, ambayo imekufa kabisa na kung’olewa pamoja na mizizi yake. 13 Matendo yao ya aibu ni dha hiri kama vile mapovu ya mawimbi ya bahari. Wao ni kama nyota zinazotangatanga, na mahali pao ni katika lile giza kuu ambalo Mungu amewawekea milele. 14 Henoki, ambaye alikuwa wa kizazi cha saba baada ya Adamu, alitoa unabii kuhusu watu hawa akasema, “Sikilizeni! Nilimwona Bwana akija na watakatifu wake maelfu kwa maelfu 15 kutoa hukumu kwa wote na kuwaadhibu wasiomcha Mungu, kwa ajili ya matendo yao maovu waliyoyatenda na kwa ajili ya maneno makali ambayo hao waovu wasiomcha Mungu walisema juu yake.”

16 Watu hawa ni wanung’unikaji, wakaidi, wenye kufuata tamaa zao, wenye majivuno, wenye kujigamba na ambao huwasifu watu wen gine ili mambo yao yafanikiwe.

Maonyo Na Maagizo

17 Lakini ninyi wapendwa, kumbukeni yale mliyoambiwa na mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo kwamba yatatokea. 18 Waliwaam bieni kwamba, “Katika siku za mwisho, watatokea watu watakaowad hihaki , watu wafuatao tamaa zao mbaya.” 19 Watu hawa ndio wanaosababisha mafarakano, watu wafuatao tamaa za dunia, wasio na Roho wa Mungu. 20 Lakini ninyi wapendwa, jengeni maisha yenu juu ya imani yenu takatifu; ombeni katika nguvu na uweza wa Roho Mtakatifu. 21 Jitunzeni katika upendo wa Mungu; ngojeeni rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo itakayowafikisha kwenye uzima wa milele. 22 Wavuteni wale wenye mashaka. 23 Okoeni wengine kwa kuwany akua kutoka katika moto; wengine wahurumieni, lakini mwogope, mkichukia hata mavazi yao yaliyochafuliwa kwa tamaa zao za dhambi.

24 Basi, utukufu ni wake yeye awezaye kuwalinda msianguke na kuwafikisheni bila hatia mbele ya utukufu wake mkiwa na furaha.

Kuhusu Ufunuo Huu

Huu ni ufunuo wa Yesu Kristo aliopewa na Mungu ili apate kuwaonyesha watumishi wake mambo yatakayotokea karibuni. Kristo alimtuma malaika wake amjulishe mtumishi wake Yohana, ambaye ameandika yale yote aliyoyaona, yaani ujumbe wa neno la Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo. Amebarikiwa anayesoma maneno ya unabii huu na wale wanaosikiliza na kuzingatia yale yaliyoandikwa humu, maana wakati umekaribia.

Salamu Kwa Makanisa Saba

Kutoka kwa Yohana. Kwa Makanisa saba yaliyoko Asia: Ninawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu aliyeko, ambaye alikuwako na atakayekuja; na kutoka kwa wale roho saba walioko mbele ya kiti chake cha enzi;

na kutoka kwa Yesu Kristo ambaye ni shahidi mwaminifu, wa kwanza kufufuliwa kutoka kwa wafu, na ambaye ni mtawala wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda na ametuweka huru kutoka katika dhambi zetu kwa damu yake;

akatufanya sisi kuwa wafalme na makuhani, tum tumikie Mungu Baba yake. Utukufu na uwezo ni wake milele na milele! Amina.

Tazama! Anakuja katika mawingu! Na kila jicho litamwona. Hata na wale waliomchoma mkuki na makabila yote ulimwenguni wataomboleza kwa ajili yake. Naam. Amina. “Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu, “Aliyeko na aliyekuwako na ata kayekuja, Mwenyezi.”

Yohana Alivyopata Ufunuo

Mimi ni Yohana, ndugu yenu na mwenzenu katika mateso, na katika ufalme na subira kwa ajili ya Yesu Kristo. Niliwekwa katika kisiwa cha Patmo kwa ajili ya kutangaza neno la Mungu na kumshuhudia Yesu. 10 Basi, siku ya Bwana nilikuwa katika Roho, nikasikia sauti kubwa kama ya tarumbeta nyuma yangu 11 ikasema, “Andika haya yote unayoyaona kwenye kitabu, kisha ukipeleke kwe nye makanisa saba yafuatayo: Efeso, Smirna, Pergamo, Thiatira, Sardi, Filadelfia na Laodikia.”

Sardi, Filadelfia na Laodikia.”

12 Ndipo nikageuka ili nione ni sauti ya nani iliyokuwa ikisema nami. Na nilipogeuka, nikaona vinara saba vya taa vya dhahabu. 13 Katikati ya vile vinara, nikaona mtu kama mwana wa Adamu, amevaa kanzu ndefu na mkanda wa dhahabu kifuani. 14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu, nyeupe kama theluji; na macho yake yalikuwa kama moto uwakao. 15 Miguu yake ilikuwa kama shaba iliyosuguliwa sana, kama vile imesafishwa katika tanuru ya moto; na sauti yake ilikuwa kama sauti ya mapo romoko ya maji. 16 Katika mkono wake wa kulia alishika nyota saba, na kinywani mwake mlitoka upanga wenye makali kuwili. Uso wake uling’aa kama jua kali.

17 Nilipomwona, nilianguka miguuni pake kama mfu. Lakini yeye akaweka mkono wake wa kulia juu yangu akasema, “Usiogope. Mimi ni wa kwanza na wa mwisho. 18 Mimi ni Yeye aliye hai; nili kufa na tazama, mimi ni hai milele na milele! Nami ninazo funguo za mauti na kuzimu. 19 Basi andika mambo uliyoyaona, yaliyopo na yatakayotokea baadaye. 20 Maana ya zile nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kulia na vile vinara saba vya taa vya dha habu ni hii: zile nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba; na vile vinara saba ni hayo makanisa saba.”

Ujumbe Kwa Kanisa La Efeso

“Kwa malaika wa kanisa la Efeso andika hivi: ‘Haya ni maneno ya yule aliyeshika nyota saba katika mkono wake wa kulia, na ambaye hutembea katikati ya vinara saba vya taa vya dhahabu. Najua matendo yako, bidii yako na uvumilivu wako. Najua kuwa huwezi kuvumilia watu waovu na kwamba umewapima wale wanaojiita mitume na kumbe sio, na umetambua ya kuwa wao ni waongo. Najua umevumilia na kustahimili mateso kwa ajili ya jina langu, wala hujachoka .

Lakini nina neno hili juu yako: kwamba umeacha upendo wako wa kwanza. Kumbuka pale ulipokuwa kabla ya kuanguka. Tubu, uache dhambi zako, ukafanye matendo ya mwanzo. Kama hukuacha dhambi zako, nitakuja kwako na kukiondoa kinara chako cha taa kutoka mahali pake. Lakini una jambo moja zuri: unayachukia matendo ya Wanikolai kama ninavyoyachukia mimi.

Mwenye nia ya kusikia na ayasikie yale ambayo Roho anawaam bia makanisa . Atakayeshinda, nitampa haki ya kula matunda ya mti wa uzima ambao uko katika bustani ya Mungu.”’

Ujumbe Kwa Kanisa La Smirna

“Kwa malaika wa kanisa la Smirna andika hivi: ‘Haya ni maneno yake yeye aliye wa kwanza na wa mwisho; aliyekufa kisha akawa hai tena.

Naijua dhiki yako na umaskini wako, ingawaje kwa kweli wewe ni tajiri! Najua matukano wanayokutukana wale wanaojiita Wayahudi lakini si Wayahudi; wao ni sinagogi la shetani. 10 Usiogope mateso yatakayokupata. Nakuhakikishia kuwa shetani atawatia baadhi yenu gerezani ili kuwajaribu. Nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.

11 Mwenye nia ya kusikia na asikie yale ambayo Roho anawaam bia makanisa. Atakayeshinda hatadhuriwa na kifo cha pili.’ ”

Ujumbe Kwa Kanisa La Pergamo

12 “Kwa malaika wa Kanisa la Pergamo andika hivi: ‘Haya ni maneno yake yeye aliye na upanga mkali wenye makali kuwili.

13 Ninajua unakoishi, kule ambako shetani ameweka kiti chake cha enzi. Hata hivyo umelishika jina langu, wala hukuikana imani yako kwangu hata katika siku za shahidi wangu mwaminifu Antipa, ambaye aliuawa katika mji wenu, ambao ni maskani ya shetani.

14 Lakini nina mambo machache juu yako: baadhi yenu ni wafu asi wa mafundisho ya Balaamu, yule aliyemfundisha Balaki awashaw ishi Waisraeli watende dhambi kwa kula vitu vilivyotolewa dhabihu kwa miungu na kufanya uasherati. 15 Na tena baadhi yenu wanafu ata mafundisho ya Wanikolai. 16 Basi tubuni mwache dhambi zenu: ama sivyo nitakuja hivi karibuni na kupigana na watu hao kwa upanga utokao kinywani mwangu.

17 Aliye na nia ya kusikia na asikie yale ambayo Roho ana waambia makanisa. Atakayeshinda nitampa sehemu ya ile mana iliy ofichwa, nami nitampa jiwe jeupe ambalo juu yake limeandikwa jina jipya asilolijua mtu, isipokuwa yule anayelipokea.’

Ujumbe Kwa Kanisa La Thiatira

18 “Kwa malaika wa kanisa la Thiatira andika hivi: ‘Haya ni maneno ya Mwana wa Mungu ambaye macho yake ni kama moto uwakao, na miguu yake inang’aa kama shaba iliyosuguliwa sana. 19 Nayajua matendo yako, upendo wako, imani yako, huduma na subira yako; na kwamba matendo yako ya sasa yamezidi yale ya mwanzo.

20 Hata hivyo ninalo jambo hili juu yako: unamvumilia yule mwanamke Yezebeli ambaye anajiita nabii, lakini anawafundisha na kuwapotosha watumishi wangu wafanye uasherati na kula vyakula vilivyotolewa kwa miungu. 21 Nimempa muda atubu, aache uasher ati, lakini hataki kutubu. 22 Kwa hiyo nitamtupa kitandani kwa ugonjwa, na atapata mateso makali pamoja na hao wanaozini naye wasipotubu matendo yake. 23 Tena nitawaua watoto wake. Ndipo makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo na akili za watu na kwamba nitamlipa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake. 24 Lakini ninawaambia ninyi wengine mlioko Thiatira, ninyi ambao hamfuati mafundisho ya Yezebeli, wala ham kujifunza hayo wengine wanayoyaita ‘siri za ndani’ za shetani, sitawaongezea mzigo mwingine. 25 Bali mshike sana hicho mlicho nacho mpaka nitakapokuja.

26 Atakayeshinda na kuendelea kutenda mapenzi yangu mpaka mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa. 27 ‘Atawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunja vipande vipande kama chombo cha udongo 28 Pia nitampa ile nyota ya asubuhi. 29 Aliye na nia ya kusikia na asikie yale ambayo Roho anawaambia makanisa.’ ”

Ujumbe Kwa Kanisa La Sardi

“Kwa malaika wa Kanisa la Sardi andika hivi: ‘Haya ni maneno yake yeye aliye na zile Roho saba za Mungu na zile nyota saba. Nayajua matendo yako; na kwamba una sifa ya kuwa hai, na kumbe umekufa. Amka! Imarisha kilichobakia kabla hakijaharibika kabisa, kwa maana nimeona kwamba kazi zako hazijakamilika mbele za Mungu wangu. Kumbuka basi yale uliyoyapokea na kuyasikia, yatii na kutubu. Lakini usipoamka, nitakuja kama mwizi wala huta jua saa nitakayokujia.

Bado wako watu wachache huko Sardi ambao hawajachafua mavazi yao. Wao watatembea pamoja nami wakiwa wamevaa mavazi yao meupe kwa maana wanastahili. Atakayeshinda atavikwa vazi jeupe kama wao, nami sitafuta jina lake katika kitabu cha uzima bali nitalikiri jina lake mbele ya Baba yangu na mbele za malaika wake.

Aliye na nia ya kusikia na asikie yale ambayo Roho anayaam bia makanisa.”’

Ujumbe Kwa Kanisa La Filadelfia

“Kwa malaika wa kanisa la Filadelfia andika hivi: ‘Haya ni maneno yake yeye aliye mtakatifu na wa kweli, ambaye anao ufunguo wa Daudi. Anachokifungua hakuna awezaye kukifunga, na anachoki funga hakuna awezaye kukifungua.

Nayajua matendo yako. Tazama, nimeweka mbele yako mlango ulio wazi ambao hakuna awezaye kuufunga. Ninajua kwamba ingawa nguvu yako ni ndogo lakini umelishika neno langu na hujalikana jina langu. Sikiliza, wale watu ambao ni wa sinagogi la she tani, wale wajiitao Wayahudi kumbe sio, bali ni waongo; nitawafa nya waje wapige magoti mbele yako na wakiri kwamba nimekupenda. 10 Kwa kuwa umeshika agizo langu la kustahimili kwa subira, nitakulinda wakati wa ile dhiki itakayokuja duniani pote kuwajar ibu waishio ulimwenguni.

11 Ninakuja upesi. Shika sana kile ulicho nacho asije mtu akachukua taji yako. 12 Atakayeshinda nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu wala hatatoka humo kamwe. Na nitaan dika juu yake jina la Mungu wangu na jina la mji wake Mungu wangu, Yerusalemu mpya, ambao unakuja kutoka mbinguni kwa Mungu wangu. Pia nitaandika juu yake jina langu jipya.

13 Aliye na nia ya kusikia na asikie yale ambayo Roho anay aambia makanisa.’ ”

Ujumbe Kwa Kanisa La Laodikia

14 “Kwa malaika wa kanisa la Laodikia andika hivi: ‘Haya ni maneno yake yeye aitwaye Amina, shahidi mwaminifu na wa kweli, mtawala wa vyote alivyoumba Mungu.

15 Nayajua matendo yako; kwamba wewe si baridi wala si moto. Afadhali kama ungalikuwa baridi au moto. 16 Basi, kwa kuwa wewe ni vuguvugu, si baridi wala si moto, nitakutapika utoke kinywani mwangu. 17 Unajigamba ukisema, ‘Mimi ni tajiri , nimefanikiwa wala sihitaji kitu cho chote.’ Lakini hutambui kwamba wewe ni mnyonge, mtu wa kuhurumiwa, maskini, kipofu; tena wewe ni uchi. 18 Kwa hiyo ninakushauri ununue kutoka kwangu dhahabu iliyosaf ishwa kwa moto ili upate kuwa tajiri; na mavazi meupe ili upate kuvaa, ufiche aibu ya uchi wako. Ujinunulie pia mafuta uyapake macho yako ili upate kuona.

19 Wote niwapendao, ninawakaripia na kuwarudi. Kwa hiyo fanya bidii, utubu na kuziacha dhambi zako. 20 Tazama, nasimama mlangoni napiga hodi. Mtu ye yote akisikia sauti yangu na kufun gua mlango, nitaingia ndani na kula pamoja naye, naye pamoja nami. 21 Atakayeshinda nitampa haki ya kuketi pamoja nami kwenye kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu kwenye kiti chake cha enzi. 22 Aliye na nia ya kusikia na asikie yale ambayo Roho anay aambia makanisa.’ ”

Kiti Cha Enzi Kilichoko Mbinguni

Baada ya hayo nilitazama, nikaona mlango ulio wazi mbin guni. Na ile sauti niliyokuwa nimeisikia ikisema nami kama tar umbeta ikasema, “Njoo huku juu nami nitakuonyesha yatakayotokea baada ya haya. ” Ghafla nilikuwa katika Roho, na mbele yangu kilikuwapo kiti cha enzi mbinguni, kikiwa kimekaliwa. Aliyeketi kwenye kiti hicho cha enzi alionekana kama jiwe zuri jekundu na akiki, na upinde wa mvua ulizunguka kile kiti cha enzi, ukione kana kama zumaridi. Kiti hicho kilizungukwa na viti vingine ishirini na vinne vya enzi ambavyo juu yake walikaa wazee ishi rini na wanne waliokuwa wamevalia mavazi meupe na taji za dhahabu vichwani. Na katika kile kiti cha enzi kulitoka umeme, ngurumo na sauti. Taa saba za moto zilikuwa zinawaka mbele ya kile kiti cha enzi, ambazo ni zile roho saba za Mungu. Mbele ya kile kiti cha enzi kulikuwa na kitu kinachofanana na bahari ya kioo iking’aa kama jiwe la kioo. Katikati, kuzunguka kile kiti cha enzi, walikuwapo viumbe hai wanne, wenye macho kila mahali, mbele na nyuma.

Kiumbe hai wa kwanza alifanana na simba, wa pili alifanana na ng’ombe dume, wa tatu alikuwa na uso kama wa mwanadamu, wa nne alifanana na tai arukaye. Na hawa viumbe hai wanne, kila mmoja alikuwa na mabawa sita na macho kila mahali, hata chini ya mabawa. Usiku na mchana hawakuacha kuimba, “Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni Bwana Mungu Mwenyezi, aliyekuwako, aliyeko na atakayekuja.”

Kila mara viumbe hao wanne walipomtukuza na kumheshimu na kumshukuru yeye aliyeketi kwenye kiti cha enzi na aishie milele na milele, 10 wale wazee ishirini na wanne walianguka mbele zake yeye aliyeketi kwenye kiti cha enzi na kumwabudu yeye aliye hai milele na milele. Wakaziweka taji zao mbele ya kile kiti cha enzi wakisema, 11 “Bwana wetu na Mungu wetu, wewe umestahili kupokea utukufu na heshima na uweza, kwa maana ni wewe uliyeviumba vitu vyote, na kwa mapenzi yako vitu vyote viliumbwa na vinapata kuwapo.”

Hati Na Mwana-Kondoo

Kisha nikaona katika mkono wa kulia wa yule aliyeketi kwe nye kile kiti cha enzi hati iliyoandikwa ndani na nje, ambayo ilikuwa imefungwa na mihuri saba. Tena nikamwona malaika mwenye nguvu akitangaza kwa sauti kuu, “Ni nani anayestahili kufungua hati hii na kuvunja mihuri yake?” Lakini hakupatikana mtu mbinguni, juu ya nchi, wala chini ya nchi aliyeweza kufungua hati hiyo, wala kuitazama. Nililia sana kwa sababu hakupatikana mtu aliyestahili kuifungua hati hiyo wala kuitazama. Kisha, mmoja wapo wa wale wazee akaniambia, “Usilie! Tazama, yule simba wa kabila la Yuda, wa ukoo wa Daudi, ameshinda. Yeye anaweza kufun gua hati hiyo na kuvunja mihuri yake saba.” Katikati ya kile kiti cha enzi na wale viumbe wanne na wale wazee, nikaona Mwana- Kondoo amesimama, akionekana kama amechinjwa. Alikuwa na pembe saba, na macho saba, ambayo ni wale roho saba wa Mungu waliotumwa ulimwenguni kote . Huyo Mwana-Kondoo akaenda, akaichukua ile hati kutoka kwenye mkono wa kulia wa yule aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi. Alipokwisha kuichukua ile hati, wale viumbe wanne pamoja na wale wazee ishirini na wanne walianguka mbele ya yule Mwana-Kondoo. Kila mmoja wao alikuwa na kinubi, nao walikuwa wameshika mabakuli ya dhahabu yaliyojaa ubani , ambao ni maombi ya watu wa Mungu. Nao wakaimba wimbo mpya: “Wewe unastahili kuichukua hati na kuifungua mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa na kwa damu yako ukamnunulia Mungu watu kutoka katika kila kabila na kila lugha; watu wa kila jamaa na kila taifa. 10 Umewafanya hawa wawe ufalme na makuhani wa kumtumikia Mungu wetu, na watata wala ulimwenguni.” 11 Kisha nikatazama, nikasikia sauti za mal aika wengi sana wakizunguka kile kiti cha enzi, pamoja na wale viumbe wanne na wale wazee ishirini na wanne. Idadi ya hao mal aika ilikuwa ni maelfu na maelfu na kumi elfu mara kumi elfu. 12 Nao waliimba kwa sauti kuu, “Mwana -Kondoo aliyeuawa anasta hili kupewa uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima, na utukufu na sifa!” 13 Kisha nikasikia kila kiumbe mbinguni na duniani, juu ya nchi na chini ya nchi, baharini na vyote vilivy omo baharini wakiimba, “Baraka na heshima na utukufu na uweza ni wake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi; na kwa Mwana-Kondoo, hata milele na milele! 14 Na wale viumbe wenye uhai wanne wakasema, “Amina!” Na wale wazee wakaanguka kifudifudi wakaabudu.

Mwana- Kondoo Avunja Mihuri Saba

Kisha nikamwona Mwana -Kondoo akifungua mhuri wa kwanza kati ya ile mihuri saba. Nikasikia mmoja wa wale viumbe wanne akisema kwa sauti kama ya ngurumo: “Njoo!” Nikaangalia, na hapo mbele yangu nikaona farasi mweupe na aliyempanda alikuwa na upinde, na alipewa taji akatoka kama mshindi akaendelee kushinda.

Mwana-Kondoo alipofungua muhuri wa pili, nikamsikia yule kiumbe hai wa pili akisema, “Njoo!” Akatoka farasi mwingine mwekundu sana na aliyempanda alipewa uwezo wa kuondoa amani duniani na kuwafanya watu wauane. Yeye alipewa upanga mkubwa.

Mwana-Kondoo alipofungua muhuri wa tatu, nilimsikia yule kiumbe hai wa tatu akisema, “Njoo!” Nikaangalia na mbele yangu nikaona farasi mweusi, na aliyempanda alikuwa na mizani mkononi mwake. Nikasikia kitu kama sauti kati ya hao viumbe wanne hai, ikisema, “Kibaba kimoja cha ngano kwa mshahara wa siku moja! na vibaba vitatu vya shayiri kwa mshahara wa siku moja! Lakini usi haribu mafuta wala divai!”

Mwana-Kondoo alipofungua muhuri wa nne, nilisikia sauti ya yule kiumbe hai wa nne ikisema, “Njoo!” Nikaangalia na mbele yangu nikamwona farasi mwenye rangi ya kijivu. Aliyempanda huyo farasi aliitwa mauti, naye alikuwa akifuatana na kuzimu. Nao wal ipewa mamlaka juu ya robo ya dunia, kuua kwa upanga, njaa, tauni na kwa wanyama wakali wa dunia.

Mwana-Kondoo alipofungua muhuri wa tano, niliona chini ya madhabahu, roho za watu waliouawa kwa ajili ya neno la Mungu na kwa ushuhuda wao. 10 Wakalia kwa sauti kuu wakisema, “Bwana Mwenyezi, uliye mtakatifu na mwaminifu, utakawia mpaka lini kuwa hukumu na kulipiza kisasi juu ya watu wote waishio duniani kwa ajili ya damu yetu?” 11 Kisha kila mmoja wao akapewa kanzu nyeupe. Wakaambiwa wasubiri kidogo zaidi mpaka idadi ya ndugu zao na watumishi wenzao wanaopaswa kuuawa kama wao walivyouawa, ita kapotimia.

12 Nilitazama Mwana-Kondoo alipokuwa akifungua muhuri wa sita. Pakatokea tetemeko kuu la nchi na jua likawa jeusi kama gunia lililotengenezwa kwa manyoya ya mbuzi. Mwezi wote ukawa mwekundu kama damu. 13 Nyota zikaanguka ardhini kama vile mat unda ya mtini yasiyokomaa yaangukavyo wakati mti wake unapoti kiswa na upepo mkali. 14 Anga ikatoweka kama vile karatasi inav yosokotwa; na kila mlima na kila kisiwa vikaondolewa mahali pake.

15 Ndipo wafalme wa duniani, wakuu wote, majemadari, mata jiri , wenye nguvu; na kila mtu, mtumwa na aliye huru, wakajifi cha mapangoni na kwenye miamba ya milima. 16 Wakaisihi milima na miamba wakisema, “Tuangukieni, mkatufiche tusionwe na uso wake yeye aketiye kwenye kiti cha enzi na mtuepushe na ghadhabu ya Mwana-Kondoo. 17 Kwa maana siku ile kuu ya ghadhabu yao imekuja, na ni nani awezaye kusalimika?”

Watu 144,000 Wawekewa Muhuri

Baada ya haya nikaona malaika wanne wamesimama katika pembe zote nne za dunia wakizuia pepo nne za dunia, ili upepo usivume nchi kavu wala baharini wala kwenye mti wo wote. Kisha nikaona malaika mwingine akija kutoka mashariki akiwa na muhuri wa Mungu aliye hai. Akawaita kwa sauti kuu wale malaika waliokuwa wamepewa mamlaka kuidhuru nchi na bahari, akisema, “Msiidhuru nchi wala bahari, wala miti, mpaka tutakapoweka mihuri kwenye vipaji vya nyuso za watumishi wa Mungu wetu.”

Ndipo nikasikia idadi ya wale waliowekewa mihuri, watu 144,000 kutoka katika kila kabila la Waisraeli. Kabila la Yuda, 12,000, kabila la Rubeni 12,000, kabila la Gadi 12,000, kabila la Asheri 12,000, kabila la Naftali 12,000, kabila la Manase 12,000, kabila la Simioni 12,000, kabila la Lawi 12,000, kabila la Isakari 12,000, kabila la Zabuloni 12,000, kabila la Yusufu 12,000, kabila la Benyamini 12,000.

Umati Wa Watu Waliokombolewa

Kisha nikatazama, nikaona umati mkubwa wa watu ambao hakuna mtu awezaye kuwahesabu: watu wa kila taifa, kila kabila, kila jamaa na kila lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi na mbele ya Mwana-Kondoo. Walikuwa wamevaa mavazi meupe na wameshika matawi ya mitende mikononi mwao. 10 Nao walikuwa wakisema kwa sauti kuu, “Ukombozi hutoka kwa Mungu wetu aketiye katika kiti cha enzi, na kwa Mwana-Kondoo!” 11 Na wale malaika wote wakasi mama kuzunguka kile kiti cha enzi na wale wazee na wale viumbe hai wanne, wakaanguka chini mbele ya kile kiti cha enzi wakamwab udu Mungu, 12 wakisema, “ Amina! Sifa na utukufu na hekima na shukrani na heshima na nguvu na uweza ni za Mungu wetu milele na milele! Amina”. 13 Kisha mmoja wa wale wazee akaniuliza, “Hawa watu waliovaa mavazi meupe, ni kina nani? Nao wametoka wapi?” 14 Nikamjibu, “Bwana, wewe ndiye unayefahamu.” Naye akasema, “Hawa ni wale waliotoka katika ile dhiki kuu; wameosha mavazi yao katika damu ya Mwana-Kondoo yakawa meupe kabisa. 15 Kwa hiyo, wanakaa mbele ya kiti cha enzi cha Mungu na kumtumikia katika Hekalu lake usiku na mchana; naye aketiye katika kile kiti cha enzi atakuwa pamoja nao na kuwalinda. 16 Kamwe hawataona njaa wala kiu tena; jua wala joto kali halitawachoma tena. Kwa maana Mwana-Kondoo aliye katikati ya kiti cha enzi atakuwa mchun gaji wao. Naye atawaongoza kwenye chemchemi za maji ya uzima; na

Muhuri Wa Saba

Mwana-Kondoo alipofungua muhuri wa saba, mbinguni palikuwa kimya kwa muda upatao nusu saa hivi. Kisha nikawaona wale mal aika saba wanaosimama mbele za Mungu, nao wakapewa tarumbeta saba.

Malaika mwingine aliyekuwa na chetezo cha dhahabu, alikuja akasimama mbele ya madhabahu. Akapewa ubani mwingi auchanganye pamoja na sala za watu wote wa Mungu, kwenye madhabahu ya dhahabu iliyo mbele ya kile kiti cha enzi. Ule moshi wa ubani ukapanda juu mbele za Mungu, pamoja na maombi ya watu wa Mungu , kutoka mkononi mwa huyo malaika. Halafu yule malaika akachukua kile chetezo akakijaza moto kutoka kwenye ile madhabahu akautupa juu ya nchi. Pakatokea radi, ngurumo, umeme na tetemeko la nchi.

Tarumbeta Za Kwanza Nne

Kisha wale malaika saba waliokuwa na tarumbeta saba waka jiandaa kuzipiga. Malaika wa kwanza akapiga tarumbeta yake, pakatokea mvua ya mawe na moto uliochanganyika na damu, ikanyesha kwa nguvu juu ya nchi; na theluthi moja ya nchi ikateketea, na theluthi moja ya miti ikateketea na majani yote mabichi yakateke tea.

Malaika wa pili akapiga tarumbeta yake na kitu kama mlima mkubwa unaowaka moto kikatupwa baharini. Theluthi moja ya bahari ikageuka kuwa damu, theluthi moja ya viumbe hai waishio bahar ini wakafa na theluthi moja ya meli zikaharibiwa.

10 Malaika wa tatu akapiga tarumbeta yake, na nyota kubwa iliyokuwa ikiwaka kama taa ilianguka kutoka angani, ikaangukia theluthi moja ya mito na chemchemi za maji. 11 Nyota hiyo inaitwa “Uchungu”. Theluthi moja ya maji yakawa machungu, na watu wengi walikufa kutokana na maji hayo kwa maana yalikuwa machungu.

12 Kisha malaika wa nne akapiga tarumbeta, na theluthi moja ya jua, theluthi moja ya mwezi na theluthi moja ya nyota, zika pigwa. Kwa hiyo theluthi moja ya mwanga wao ukawa giza. Theluthi moja ya mchana ilikuwa haina mwanga na pia theluthi moja ya usiku.

13 Halafu tena nikatazama, nikasikia tai mmoja akipiga kelele kwa sauti kuu wakati akiruka katikati ya mbingu, “Ole wao! Ole wao! Ole wao watu waishio duniani wakati itakaposikika milio ya tarumbeta ambazo karibuni zitapigwa na malaika watatu waliobakia.”

Tarumbeta Ya Tano

Kisha malaika wa tano akapiga tarumbeta yake, nikaona nyota iliyokuwa imeanguka kutoka angani hadi ardhini. Nyota hiyo ili pewa ufunguo wa shimo la kuzimu. Alipolifungua hilo shimo, moshi ulitoka ndani yake kama moshi wa tanuru kubwa sana. Jua na anga vilitiwa giza kwa ajili ya ule moshi uliotoka katika shimo hilo. Kisha, katika ule moshi wakatoka nzige wakatua ardhini. Nao wakapewa nguvu kama nguvu ya nge wa duniani. Waliambiwa wasidhuru nyasi za nchi, wala majani, wala mmea au mti wo wote. Bali wawadhuru wale watu wasiokuwa na muhuri wa Mungu kwenye vipaji vya nyuso zao. Waliruhusiwa kuwatesa kwa muda wa miezi mitano lakini wasiwaue. Na uchungu wa kuuma kwao ulikuwa kama uchungu wa mtu anapoumwa na nge. Katika siku hizo watu watata futa kifo lakini hawatakiona; watatamani kufa, lakini kifo kita wakimbia.

Wale nzige walionekana kama farasi waliotayarishwa kwa vita; vichwani mwao kulikuwa na kitu kama taji za dhahabu; na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu. Manyoya yao yalifanana kama nywele za wanawake; na meno yao yalikuwa kama meno ya simba. Walikuwa na magamba yaliyofanana na ngao za chuma; na kelele za mabawa yao zilikuwa kama kelele za magari ya farasi yenye farasi wanaokimbia kwenda vitani. 10 Walikuwa na mikia ya kuuma kama nge; nguvu yao ya kutesa watu kwa muda wa miezi mitano ilikuwa katika mikia yao. 11 Walikuwa na mfalme wa kuwatawala, naye ni malaika wa shimo la kuzimu ambaye jina lake kwa Kiebrania ni Aba doni na kwa Kigiriki ni Apolioni.

12 Maafa ya kwanza yamepita; bado mengine mawili yanakuja.

Tarumbeta Ya Sita

13 Malaika wa sita akapiga tarumbeta yake, nami nikasikia sauti ikitoka katika zile pembe nne za madhabahu iliyoko mbele ya Mungu. 14 Sauti hiyo ikamwambia yule malaika wa sita mwenye tar umbeta, “Wafungulie wale malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa wa Efrati.” 15 Basi wakafunguliwa wale malaika wanne waliokuwa wamewekwa tayari kwa ajili ya saa hiyo, na siku hiyo na mwezi huo na mwaka huo, wawaue theluthi moja ya wanadamu. 16 Idadi ya majeshi wapandao farasi ilikuwa milioni mia mbili. 17 Na hivi ndivyo nilivyowaona hao farasi na wapanda farasi katika maono yangu: wapanda farasi walivaa ngao vifuani zenye rangi ya moto na samawati na kiberiti. Na vichwa vya farasi hao vilikuwa kama vichwa vya simba; na moto, moshi na kiberiti vili kuwa vinatoka vinywani mwao. 18 Theluthi moja ya wanadamu waliu awa kwa maafa hayo matatu, yaani, moto, moshi na kiberiti, yaliy otoka vinywani mwa hao farasi. 19 Nguvu ya hao farasi ilikuwa vinywani mwao na mikiani mwao; kwa sababu mikia yao ilikuwa kama nyoka wenye vichwa ambavyo vilitumika kuwadhuru watu.

20 Wanadamu waliosalia, ambao hawakuuawa katika maafa hayo, bado walikataa kutubu na kuacha kuabudu vitu walivyotengeneza kwa mikono yao wenyewe. Waliendelea kuabudu pepo, sanamu za dhahabu na za fedha na za shaba na za mawe na za miti, sanamu zisizoweza kuona, kusikia wala kutembea. 21 Wala hawakutubu na kuacha matendo yao ya uuaji, uchawi, uasherati na wizi.

Malaika Mwenye Hati Ndogo

10 Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa amevaa wingu, na upinde wa mvua kich wani. Uso wake uling’aa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto. Mkononi mwake alikuwa ameshika hati ndogo iliyokuwa imefunguliwa. Mguu wake wa kulia aliuweka juu ya bahari na mguu wake wa kushoto aliuweka juu ya nchi kavu. Naye akaita kwa sauti kuu kama simba anayenguruma. Alipopaza sauti, ngurumo saba ziliitikia kwa kishindo. Na zile ngurumo saba zilipokwisha kuitikia, nilitaka kuanza kuandika, lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Funga hayo yaliyosemwa na ngurumo hizo saba, ni siri; usiyaandike.”

Kisha yule malaika aliyekuwa amesimama juu ya bahari na nchi kavu akainua mkono wake wa kulia juu mbinguni, akaapa kwa jina la Mungu aishiye milele na milele, aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote vilivyomo, na bahari na vyote vilivy omo, akasema, “Wakati wa kungoja umekwisha. Lakini katika siku ambazo yule malaika wa saba atakaribia kupiga tarumbeta yake, siri ya Mungu itatimizwa kama alivyowatangazia watumishi wake manabii.”

Ndipo ile sauti niliyokuwa nimeisikia pale mwanzoni ikasema nami tena, “Nenda, kachukue ile hati iliyoko mkononi mwa yule malaika aliyesimama juu ya bahari na nchi kavu.”

Basi nikaenda, nikamwomba yule malaika anipe ile hati ndogo. Akaniambia, “Ichukue uile. Itakuwa chungu tumboni mwako, lakini mdomoni mwako itakuwa tamu kama asali.” 10 Basi nikaichukua ile hati ndogo kutoka mkononi mwa yule malaika nikaila. Ilikuwa tamu kama asali mdomoni mwangu lakini nili poimeza, ikawa chungu tumboni mwangu. 11 Kisha nikaambiwa, “Inakubidi kutoa unabii tena kuhusu watu wengi, na mataifa, lugha na wafalme.”

Mashahidi Wawili

11 Ndipo nikapewa kipimo kama fimbo, nikaambiwa, “Nenda kapime Hekalu la Mungu pamoja na madhabahu na uwahesabu watu waabuduo humo. Lakini usipime uwanja wa nje ya Hekalu, uache, kwa sababu uwanja huo wamepewa mataifa wasiomjua Mungu. Wao wataukanyagakanyaga mji mtakatifu kwa muda wa miezi arobaini na miwili. Nami nitawapa uwezo mashahidi wangu wawili watoe unabii kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na sitini na mbili, wakiwa wamevaa magunia.”

Manabii hao wawili ni ile mizeituni miwili na vile vinara viwili visimamavyo mbele za Bwana na mbele ya nchi yote. Na mtu akitaka kuwadhuru, moto hutoka vinywani mwao na kuwateketeza adui zao. Na hivyo ndivyo atakavyokufa mtu ye yote atakayetaka kuwad huru. Watu hawa wanayo mamlaka ya kuyafunga mawingu ili mvua isinyeshe wakati wote watakapokuwa wanatoa unabii wao. Watakuwa na mamlaka juu ya maji kuyageuza kuwa damu, na kuleta maafa ya kila aina ulimwenguni, kama wapendavyo. Lakini wakishamaliza kutoa unabii huo, yule mnyama atokaye katika shimo la kuzimu ata wapiga vita na kuwashinda na kuwaua. Maiti zao zitabaki katika barabara ya mji mkuu ambao kwa fumbo unaitwa Sodoma na Misri, ambapo Bwana wao alisulubiwa. Kwa muda wa siku tatu na nusu, watu wa kila kabila, lugha, taifa na rangi wataziangalia maiti zao, na hawataruhusu wazikwe. 10 Watu waishio duniani watafura hia kifo cha manabii hao wawili na kushangilia kwa kupeana zawadi kwa sababu manabii hao waliwatesa watu waishio ulimwenguni.

11 Lakini baada ya zile siku tatu na nusu, pumzi ya uhai kutoka kwa Mungu iliwaingia, nao wakasimama; wote waliowaona wakaingiwa na hofu kuu. 12 Kisha wale manabii wawili wakasikia sauti kuu kutoka mbinguni ikiwaambia, “Njooni huku juu!” Nao wakapaa mbinguni katika wingu, wakati maadui zao wakiwatazama. 13 Wakati huo huo, kukatokea tetemeko kuu la nchi, na sehemu moja ya kumi ya mji ikaanguka. Watu elfu saba wakauawa katika tetemeko hilo na waliosalimika wakaogopa sana, wakamtukuza Mungu wa mbinguni.

14 Maafa ya pili yamekwisha kupita. Lakini maafa ya tatu yanakuja upesi.

Tarumbeta Ya Saba

15 Kisha malaika wa saba akapiga tarumbeta yake. Na sauti kuu zikasikika mbinguni zikisema, “Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana wetu na Kristo wake, naye atatawala milele na milele.” 16 Na wale wazee ishirini na wanne waketio mbele za Mungu katika viti vyao vya enzi wakaanguka kifudifudi wakamwabudu Mungu, 17 wakisema, “Tunakushukuru, Bwana Mungu Mwenyezi uli yeko na uliyekuwako; kwa kuwa umeuchukua uweza wako mkuu na ukaanza kutawala. 18 Watu wa mataifa walikasirika kwa kuwa wakati wa ghadhabu yako umefika. Wakati umefika wa kuwahukumu wafu na kuwapa tuzo watumishi wako manabii na watakatifu walioli tukuza jina lako, wakubwa kwa wadogo; na wakati umefika wa kuwaangamiza wale wanaoiangamiza dunia.”

19 Kisha Hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa na sanduku la agano lake likaonekana Hekaluni mwake. Kukatokea umeme, sauti, ngurumo na tetemeko la nchi na mvua kubwa ya mawe.

Mwanamke Na Joka

12 Ndipo ishara kuu ikaonekana mbinguni: palikuwa na mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na taji ya nyota kumi na mbili ilikuwa juu ya kichwa chake. Alikuwa mjam zito,akilia kwa uchungu kwa kuwa alikuwa anakaribia kujifungua. Kisha ishara nyingine ikaonekana mbinguni: likaonekana joka kubwa jekundu lenye vichwa saba na pembe kumi na taji saba katika vichwa vyake. Mkia wake ulifagia theluthi moja ya nyota zote angani na kuziangusha ardhini. Joka hili likasimama mbele ya yule mwanamke aliyekuwa karibu kujifungua, likiwa tayari kumla huyo mtoto mara tu atakapozaliwa. Mama huyo akajifungua mtoto wa kiume, ambaye atayatawala mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Lakini mtoto huyo akanyakuliwa na kupelekwa kwa Mungu, kwenye kiti chake cha enzi. Yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambako Mungu alik wisha kumtengenezea mahali pa kumtunza kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na sitini.

Vita Mbinguni

Kisha kukazuka vita mbinguni: Mikaeli na malaika wake waki pigana na hilo joka. Joka nalo pamoja na malaika wake likapigana nao. Lakini joka na malaika wake wakashindwa na hapakuwa tena na nafasi kwa ajili yao mbinguni. Basi joka hilo kuu likatupwa nje, yule nyoka wa kale aitwaye Ibilisi na Shetani, adanganyaye watu wote ulimwenguni. Alitupwa chini ardhini, yeye pamoja na malaika wake.

Ushindi Mbinguni Watangazwa

10 Kisha nikasikia sauti kuu mbinguni ikisema, “Sasa umeti mia wokovu na uweza na Ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake yamefika. Kwa kuwa mshtaki wa ndugu zetu anayewashtaki mbele za Mungu usiku na mchana ametupwa chini. 11 Nao wamemshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo na kwa neno la ushuhuda wao, kwa kuwa wao hawakuyapenda maisha yao kiasi cha kuogopa kifo. 12 Kwa hiyo furahini ninyi mbingu, na wote wakaao mbinguni! Bali ole wenu nchi na bahari maana shetani amekuja kwenu akiwa amejaa ghadhabu, kwa maana anajua kuwa muda wake ni mfupi!”

13 Lile joka lilipoona kuwa limetupwa chini duniani, lilim winda yule mwanamke aliyekuwa amejifungua mtoto wa kiume. 14 Lakini huyo mama akapewa mabawa mawili ya yule tai mkubwa kusudi aruke hadi mahali ambapo atatunzwa kwa muda na nyakati na nusu ya wakati. 15 Lile joka likamwaga maji kama mto kutoka kinywani mwake, mafuriko yakamfuata huyo mama ili yamchukue. 16 Lakini ardhi ikamsaidia huyo mama; ikafunua kinywa chake na kuumeza ule mto uliotoka kinywani mwa joka. 17 Kisha lile joka likashikwa na ghadhabu kwa ajili ya huyo mama, likaondoka kwenda kupigana vita na watoto wake waliobakia, wale wanaozitii amri za Mungu na kumshuhudia Yesu. Lile joka likasimama kwenye mchanga wa bahari.

Mnyama Kutoka Baharini

13 Kisha nikaona mnyama akitoka baharini. Alikuwa na pembe kumi na vichwa saba na taji kumi kwenye pembe zake. Na kila kichwa kiliandikwa jina la kufuru. Huyo mnyama alifanana kama chui lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kinywa chake kama cha simba. Lile joka lilimpa mnyama huyo nguvu zake, kiti chake cha enzi na uwezo mkuu. Kichwa kimoja cha huyo mnyama kilione kana kama kilikwisha kuwa na jeraha lisiloweza kupona, lakini jeraha hilo lilikuwa limepona na dunia nzima ilimstaajabia huyo mnyama na kumfuata. Watu waliliabudu lile joka kwa sababu lili kuwa limempa huyo mnyama uwezo wake. Pia walimwabudu huyo mnyama wakisema, “Ni nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana naye?”

Kisha huyo mnyama akaruhusiwa kusema maneno ya kujisifu na ya kufuru na akapewa haki ya kutawala kwa muda wa miezi arobaini na miwili. Alisema maneno ya kumkufuru Mungu, akilitukana jina lake na mahali aishipo, yaani, aliwatukana wale waishio mbinguni. Pia aliruhusiwa kuwapiga vita watu wa Mungu na kuwashinda. Alipewa uwezo juu ya watu wa kila kabila, kila ukoo, kila lugha na taifa. Na watu wote waishio duniani watamwabudu, yaani kila mmoja ambaye tangu kabla ya ulimwengu kuumbwa, jina lake haliku andikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa.

“Aliye na nia ya kusikia, asikilize kwa makini: 10 Ye yote aliyepangiwa kuchukuliwa mateka atatekwa. Mtu ye yote akiua kwa upanga atauawa kwa upanga. Na hii ndio nafasi ya watu wa

Mnyama Kutoka Ardhini

11 Kisha nikamwona mnyama mwingine akipanda juu kutoka katika ardhi. Alikuwa na pembe mbili kama za mwana kondoo lakini aliongea kama joka. 12 Naye alitumia uwezo wote wa yule mnyama wa kwanza aliyemtangulia. Akalazimisha dunia yote na wote waliomo duniani wamwabudu huyo mnyama wa kwanza aliyekuwa na jeraha la kifo lililokuwa limepona. 13 Huyu mnyama wa pili akafanya miu jiza ya ajabu hata kufanya moto utoke mbinguni na kushuka duniani mbele ya watu. 14 Kwa njia ya miujiza aliyowezeshwa kufanya kwa niaba ya yule mnyama wa kwanza, aliwadanganya watu waishio duniani. Aliwaamuru watengeneze sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi. 15 Kisha akawe zeshwa kuipatia pumzi ile sanamu ya mnyama wa kwanza hata ikaweza kuongea na kufanya wale wote ambao hawakuiabudu wauawe. 16 Pia aliwalazimisha watu wote, wakubwa kwa wadogo, matajiri na mas kini, watu huru na watumwa, watiwe alama kwenye mikono yao ya kulia au kwenye vipaji vya nyuso zao. 17 Hakuna mtu ye yote ambaye angeweza kununua au kuuza kitu kama hana alama ile, yaani jina la huyo mnyama au namba ya jina lake.

18 Jambo hili linahitaji hekima. Mwenye akili ya kutambua apige hesabu ya mnyama huyo kwa sababu ni namba ya mtu. Namba yake ni mia sita sitini na sita.

Mwana-Kondoo Na Waliokombolewa Wa Kwanza

14 Kisha nikatazama na mbele yangu nikamwona Mwana-Kondoo amesimama juu ya Mlima Sioni akiwa pamoja na watu 144,000 ambao kwenye vipaji vya nyuso zao waliandikwa jina la Mwana-Kondoo na jina la Baba yake. Basi nikasikia sauti kutoka mbinguni kama sauti ya maporomoko ya maji mengi na kama sauti ya ngurumo ya radi kubwa. Na sauti hiyo niliyoisikia, ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi wakipiga vinubi vyao. Walikuwa wanaimba wimbo mpya mbele ya kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe hai wanne na wale wazee. Hakuna mtu aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao watu 144,000 waliokombolewa kutoka duniani. Hao ndio wale ambao hawakujitia unajisi kwa kuhusiana na wanawake, kwa kuwa wao ni bikira. Hao ndio wanaomfuata Mwana-Kondoo kila aendako. Wame nunuliwa kutoka miongoni mwa wanadamu wakawa matunda ya kwanza kutolewa kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo. Hawajapata kusema uongo kamwe; hawana hatia yo yote.

Malaika Watatu

Kisha nikamwona malaika mwingine akiruka juu angani akiwa na Injili ya milele ya kuwatangazia watu wote waishio duniani: kwa mataifa yote, makabila yote, kwa watu wa lugha zote na watu wa aina zote. Akasema kwa sauti kuu, “Mcheni Mungu na kumtu kuza kwa maana saa ya kutoa hukumu yake imefika. Mwabuduni yeye aliyeumba mbingu, dunia, bahari na chemchemi za maji.”

Malaika wa pili akafuata akisema, “Babiloni umeanguka! Babiloni mkuu umeanguka, ule mji mkuu ambao uliwanywesha mataifa yote divai yake, divai kali ya uzinzi wake.”

Malaika wa tatu aliwafuata hao wawili akisema kwa sauti kuu, “Kama mtu ye yote anamwabudu yule mnyama na sanamu yake na kukubali kutiwa alama yake kwenye kipaji cha uso wake au kwenye mkono wake, 10 yeye naye atakunywa divai ya ghadhabu ya Mungu ambayo imemiminiwa katika kikombe cha ghadhabu yake bila kuchan ganywa na maji. Naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya mal aika watakatifu na mbele za Mwana-Kondoo. 11 Moshi wa mateso yao hupanda juu milele na milele; wala hakuna nafuu, mchana au usiku, kwa wale wamwabuduo huyo mnyama na sanamu yake au kwa ye yote anayepokea alama ya jina lake.” 12 Jambo hili linahitaji watu wa Mungu, wale ambao wanazishika amri zake, wawe wavumilivu na kumwamini Yesu.

13 Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika haya: Wamebarikiwa watu ambao tangu sasa wanakufa wakiwa ndani ya Bwana.” “Naam,” asema Roho, “watapumzika baada ya taabu zao, kwa kuwa matendo yao yatawafuata.”

Mavuno

14 Nikatazama, na mbele yangu nikaona wingu jeupe na mtu anayeonekana kama ‘mwana wa mtu’ akiwa ameketi juu yake. Alikuwa na taji ya dhahabu kichwani mwake na mundu mkali mkononi mwake. 15 Na malaika mwingine akaja kutoka Hekaluni na kwa sauti kubwa akamwita yule aliyekuwa ameketi juu ya wingu akasema, “Chukua mundu wako ukavune kwa kuwa saa ya kuvuna imefika, maana mavuno ya dunia yamekomaa.” 16 Basi yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu akauzungusha mundu wake duniani, na mavuno ya dunia yakavunwa.

17 Kisha malaika mwingine akatoka Hekaluni mbinguni, naye pia akiwa na mundu mkali.

18 Na malaika mwingine, ambaye alikuwa na mamlaka juu ya moto, akatoka kwenye madhabahu akamwita yule malaika mwenye mundu mkali kwa sauti kuu, akasema, “Chukua mundu wako mkali ukayakate matawi ya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva.”

19 Basi malaika huyo akauzungusha mundu wake duniani akakata zabibu za dunia, akazitia ndani ya mtambo mkubwa wa kusindika zabibu wa ghadhabu ya Mungu. 20 Zabibu zikakamuliwa ndani ya mtambo huo wa kusindika zabibu uliokuwa nje ya mji, na damu ika tiririka kama mafuriko kutoka katika mtambo huo na urefu wa mafu riko hayo ulikuwa kama kilometa mia tatu, na kina chake kiasi cha meta moja na nusu.

Wimbo Wa Musa Na Mwana-Kondoo

15 Ndipo nikaona ishara nyingine mbinguni, ishara kubwa na ya ajabu: malaika saba wenye maafa saba ya mwisho, kwa maana, maafa hayo yanakamilisha ghadhabu ya Mungu.

Na nikaona kitu kama bahari ya kioo imechanganyika na moto. Na kando ya hiyo bahari, walikuwa wamesimama wale watu waliom shinda yule mnyama na sanamu yake pamoja na namba ya jina lake. Walikuwa wameshika vinubi walivyopewa na Mungu. Nao waliimba wimbo wa Musa, mtumishi wa Mungu na wimbo wa Mwana-Kondoo wakisema, ‘ ‘Matendo yako Bwana Mungu Mwenyezi, ni makuu na ya ajabu! Njia zako wewe Mfalme wa Mataifa ni za haki na za kweli! Ni nani asiyekucha wewe Bwana na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako ni mtakatifu. Mataifa yote yatakuja na kukuabudu kwa kuwa matendo yako ya haki yamekwisha dhihirishwa.”

Baada ya hapo nikatazama, nikaona mbinguni Hekalu, yaani hema ya ushuhuda, imefunguliwa. Basi wale malaika saba wenye maafa saba wakatoka humo Hekaluni wakiwa wamevaa nguo za kitani safi zing’aazo na vifuani mwao walivaa mikanda ya dhahabu. Kisha mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai, akawapa wale mal aika saba mabakuli saba ya dhahabu yalizojaa ghadhabu ya Mungu aishiye milele na milele. Na Hekalu ilijaa moshi uliotokana na utukufu na uweza wake, wala hakuna mtu aliyeweza kuingia Hekaluni mpaka yale maafa saba ya wale malaika saba yakamilike.

Mabakuli Saba Ya Ghadhabu Ya Mungu

16 Kisha nikasikia sauti kuu kutoka Hekaluni ikiwaambia wale malaika saba, “Nendeni mkamwage duniani yale mabakuli saba ya ghadhabu ya Mungu.”

Malaika wa kwanza akaenda akalimimina bakuli lake ardhini na madonda mabaya yenye maumivu makali yakawapata wote waliokuwa na alama ya yule mnyama na walioabudu sanamu yake.

Malaika wa pili akamimina bakuli lake baharini , ikawa kama damu ya mtu aliyekufa na kila kiumbe hai kilichokuwa ndani ya bahari kikafa.

Malaika wa tatu akamimina bakuli lake katika mito na chemchemi za maji, nazo zikageuka kuwa damu. Nami nikamsikia malaika wa maji akisema, “Umefanya haki katika hukumu hizi uli zotoa, wewe uliyeko na uliyekuwako, Mtakatifu. Maana walimwaga damu ya watakatifu na manabii, na wewe umewapa damu wanywe, kama walivyostahili.” Nikasikia madhabahu ikiitikia, “Naam, Bwana Mungu Mwenyezi, hukumu zako ni za kweli na haki.!”

Mungu Mwenyezi, hukumu zako ni za kweli na haki.!”

Malaika wa nne akamimina bakuli lake kwenye jua nalo lika pewa nguvu za kuwachoma watu kwa moto wake mkali. Watu wakaun guzwa na moto huo nao wakalaani jina la Mungu aliyekuwa na uwezo juu ya maafa haya, wala hawakutubu na kumtukuza.

10 Malaika wa tano akamimina bakuli lake kwenye kiti cha enzi cha yule mnyama, na ufalme wake ukawa gizani. Watu wakauma ndimi zao kwa uchungu 11 wakamlaani Mungu wa mbinguni kwa mau mivu yao na madonda yao, wala hawakutubu kwa ajili ya matendo yao maovu.

12 Malaika wa sita akamimina bakuli lake kwenye mto mkubwa wa Efrati, maji yake yakakauka ili kuwatayarishia njia wafalme kutoka mashariki. 13 Nikaona roho wachafu waliofanana na chura wakitoka katika kinywa cha lile joka na katika kinywa cha yule mnyama, na katika kinywa cha yule nabii wa uongo. 14 Hizo ni roho za pepo zitendazo miujiza. Nazo huwaendea wafalme wa ulim wengu wote na kuwakusanya tayari kwa vita, siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi. 15 “Sikiliza! Ninakuja kama mwizi! Amebarikiwa aliye macho, akiziweka tayari nguo zake ili asiende bila nguo na watu wakam wona uchi!” 16 Kisha wakawakusanya wafalme pamoja mahali ambapo huitwa “Armageddoni” kwa Kiebrania.

17 Malaika wa saba akamimina bakuli lake angani na sauti kuu ikatoka Hekaluni katika kile kiti cha enzi ikisema, “Imekwisha timia!” 18 Kukawa na miali ya umeme, sauti, ngurumo za radi na tetemeko kuu la ardhi. Hapajawahi kuwa na tetemeko la ardhi kama hilo tangu mwanadamu kuwapo, kwani lilikuwa tetemeko kubwa ajabu.

19 Ule mji mkuu uligawanywa katika sehemu tatu na miji yote ya mataifa ikaanguka. Mungu akakumbuka Babiloni kuu akainywesha kikombe cha divai ya hasira na ghadhabu yake. 20 Kila kisiwa kikatoweka wala milima haikuonekana. 21 Mvua kubwa ya mawe, mawe mazito karibu kilo hamsini, ikanyesha kutoka mbinguni ikawaangu kia wanadamu. Wanadamu wakamlaani Mungu kwa ajili ya maafa ya mvua ya mawe. Kwa maana lilikuwa ni pigo kuu la kutisha.

Adhabu Ya Babiloni

17 Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na yale mabakuli saba akaja akaniambia, “Njoo, nitakuonyesha hukumu ya yule kahaba mkuu aliyeketi juu ya maji mengi. Wafalme wa dunia wamezini naye, na watu waishio duniani walilewa divai yake ya uzinzi.” Kisha nikiwa katika Roho malaika akanipeleka nyikani, nikamwona mwanamke mmoja ameketi juu ya mnyama mwekundu aliyejaa majina ya kumtukana Mungu mwili mzima. Mnyama huyo alikuwa na vichwa saba na pembe kumi. Huyo mwanamke alikuwa amevaa mavazi ya rangi ya zambarau na nyekundu na kujipamba kwa dhahabu, vito vya thamani na lulu. Mkononi mwake alishika kikombe cha dhahabu kilichojaa mambo ya kuchukiza na uchafu wa uasherati wake. Na kwenye kipaji cha uso wake yaliandikwa maneno yenye maana iliyofichika: “Babiloni Mkuu, Mama wa Makahaba na wa Machukizo yote ya Duniani.” Nikaona kuwa huyo mwanamke alikuwa amelewa damu ya watu wa Mungu na damu ya watu waliouawa kwa kumshuhudia Yesu. Nilipomwona, nilistaajabu sana. Lakini yule malaika akaniambia, “Kwa nini unastaajabu? Nitakufunulia siri ya huyo mwanamke na huyo mnyama aliyembeba, mwenye vichwa saba na pembe kumi. Huyo mnyama uliyemwona alikuwapo lakini sasa hayupo , naye atapanda kutoka katika shimo la kuzimu kwenda maangamizoni. Na watu waishio duniani ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima tangu ulimwengu kuumbwa, watashangaa kumwona huyo mnyama, kwa maana alikuwapo, na hayupo, na kwamba atakuwapo.

Jambo hili linahitaji hekima na maarifa. Vile vichwa saba ni milima saba ambapo huyo mwanamke ameketi. 10 Pia hivyo vichwa saba ni wafalme saba ambao kati yao watano wamekwisha kuanguka, mmoja yupo na mmoja hajaja bado, naye akija, atalazimika kukaa kwa muda mfupi tu. 11 Na huyo mnyama aliyekuwapo ambaye hayupo, yeye ni wa nane, lakini ni wa kundi la wale saba naye pia ataan gamizwa.

12 Zile pembe kumi ulizoziona ni wafalme kumi ambao hawaja tawazwa bado, lakini watatawazwa kwa muda wa saa moja tu pamoja na yule mnyama. 13 Hawa wana nia moja nao watampa yule mnyama nguvu zao na mamlaka yao. 14 Watampiga vita Mwana-Kondoo na Mwa na-Kondoo atawashinda kwa kuwa yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme, na wale walio pamoja naye wanaitwa wateule na waami nifu.”

15 Kisha akaniambia, “Yale maji uliyoyaona alipokuwa amekaa yule kahaba, ni watu na umati wa watu na mataifa na lugha. 16 Na zile pembe kumi ulizoziona, pamoja na huyo mnyama watamchukia huyo kahaba; watamfanya kuwa mkiwa na uchi, watamla nyama yake na kumteketeza kabisa kwa moto. 17 Maana Mungu amefanya mioyo yao kutimiza mapenzi yake, kwa kuwafanya wawe na nia moja ya kumpa mamlaka yao ya kifalme huyo mnyama, mpaka maneno ya Mungu yataka potimizwa. 18 Na yule mwanamke uliyemwona ni ule mji mkuu wenye mamlaka juu ya wafalme wa dunia.”

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica