Previous Prev Day Next DayNext

Bible in 90 Days

An intensive Bible reading plan that walks through the entire Bible in 90 days.
Duration: 88 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Luka 2-9

Kuzaliwa Kwa Yesu

Siku zile Kaisari Augusto, mtawala wa milki ya Kirumi, aliamuru ya kwamba watu wote wa milki yake waandikishwe. Hii ilikuwa ni sensa ya kwanza kufanyika nayo ilitokea wakati Kirenio alipokuwa liwali wa Siria. Watu wote walikwenda katika sehemu walikozaliwa ili waandikishwe huko. Yusufu alitoka mji wa Nazareti uliopo Galilaya akaenda mpaka Bethlehemu mji wa Daudi kwa sababu yeye alikuwa wa ukoo wa Daudi. Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na mchumba wake Mariamu ambaye kwa wakati huu alikuwa mja mzito.

Walipokuwa Bethlehemu, wakati wa Mariamu kujifungua uli fika, naye akamzaa mtoto wa kiume, kifungua mimba. Akamfunika kwa vinguo na kumlaza horini, kwa sababu hapakuwa na nafasi katika nyumba ya wageni.

Wachungaji Wapata Habari

Usiku ule walikuwako wachungaji wakilinda kondoo zao nje ya mji. Ghafla malaika wa Bwana akawatokea, na utukufu wa Mungu ukawang’azia pande zote. Wakajawa na hofu kuu. 10 Lakini malaika akawatuliza akisema: “Msiogope! Nawaletea habari njema ya furaha kubwa, na habari hii ni kwa faida ya watu wote! 11 Kwa maana leo katika mji wa Bethlehemu, amezaliwa Mwokozi ambaye ndiye Kristo Bwana. 12 Na hivi ndivyo mtakavyomtambua: mtamkuta mtoto mchanga amefunikwa vinguo na kulazwa horini.”

13 Mara jeshi kubwa la malaika wa mbinguni likatokea na pamoja wakamsifu Mungu wakiimba: 14 “Atukuzwe Mungu juu mbin guni, na duniani iwepo amani kwa watu ambao amependezwa nao.”

15 Malaika hao waliporudi mbinguni wale wachungaji walish auriana: “Jamani, twendeni Bethlehemu tukaone mambo haya ya ajabu yaliyotokea, ambayo Bwana ametufahamisha.”

16 Kwa hiyo wakaenda haraka Bethlehemu, wakawakuta Mariamu na Yusufu; na yule mtoto mchanga alikuwa amelala mahali pa kulia ng’ombe. 17 Walipomwona mtoto, wakawaeleza yale waliyokuwa wameambiwa. 18 Na wote waliosikia habari hizi wakastaajabia yale waliyoambiwa na wachungaji. 19 Lakini Mariamu akayaweka mambo haya yote moyoni mwake, akayafikiria mara kwa mara.

20 Wale wachungaji wakarudi, huku wakimtukuza Mungu na kum sifu kwa yale waliyoyasikia na kuyaona.

21 Hata baada ya siku nane, ilipotimia siku ya kumtahiri mtoto, aliitwa Yesu; jina alilopewa na malaika kabla hata haja chukuliwa mimba.

Yesu Apelekwa Hekaluni

22 Baada ya kutimia kwa muda wa utakaso wa Yusufu na Mar iamu, kwa mujibu wa sheria ya Musa, walimpeleka mtoto Yerusalemu, wakamtoa kwa Bwana 23 kama ilivyotakiwa na sheria ya Bwana -“Kila mtoto wa kiume wa kwanza atakabidhiwa kwa Bwana.” 24 Pia walitoa sadaka, kama ilivyotakiwa na sheria ya Bwana: “Hua wawili au makinda ya njiwa wawili.” 25 Na alikuwepo huko Yerusalemu mzee mmoja jina lake Simeoni ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu. Siku zote alikuwa akitarajia ukombozi wa Israeli na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake. 26 Pia Roho Mtaka tifu alikuwa amemhakikishia kuwa hangekufa kabla ya kumwona Kristo wa Bwana. 27 Kwa hiyo, akiwa ameongozwa na Roho Mtaka tifu, Simeoni alikwenda Hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria, 28 Simeoni alimpokea mtoto mikononi mwake akamshukuru Mungu akisema: 29 “Sasa Bwana, niruhusu mimi mtumishi wako niende kwa amani kama ulivyoniahidi, 30 kwa sababu macho yangu yameuona wokovu 31 ulioandaa mbele ya watu wote, 32 nuru itakayowaangazia watu wa mataifa na kuleta utukufu kwa watu wako Israeli.” 33 Wazazi wa mtoto walistaajabu kwa yale yaliyokuwa yakisemwa kumhusu mtoto wao. 34 Simeoni akawabariki. Kisha akamwambia Mariamu, mama yake, “Mtoto huyu amechaguliwa na Mungu kwa makusudi ya kuanga mizwa na kuokolewa kwa wengi katika Israeli. Atakuwa ishara ya onyo kutoka kwa Mungu ambayo watu wengi wataikataa 35 ili kudhi hirisha mawazo yao ya ndani. Na uchungu kama kisu kikali utaku choma moyoni.” 36-37 ,Tena, alikuwepo Hekaluni nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti wa Fanueli, wa kabila la Asheri. Nabii Ana alikuwa mjane wa miaka themanini na minne naye alikuwa ameolewa kwa miaka saba tu mumewe akafariki. Yeye aliishi humo Hekaluni daima, akimwabudu Mungu na kuomba na kufunga.

38 Wakati huo huo, Ana alikuja mbele akamshukuru Mungu na kueleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wakitarajia ukombozi wa Yerusalemu. 39 Yusufu na Mariamu walipokamilisha mambo yote yaliyotakiwa na sheria ya Mungu, walirudi nyumbani kwao Nazareti katika Wilaya ya Galilaya. 40 Yesu aliendelea kukua, akawa kijana mwenye nguvu na hekima, akijaa baraka za

Mtoto Yesu Adhihirisha Hekima Yake

41 kila mwaka wazazi wake walikwenda Yerusalemu kushiriki katika siku kuu ya Pasaka. 42 Yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama desturi ilivyokuwa. 43 Sikukuu ilipokwisha walianza safari ya kurudi nyumbani. Yesu akabaki Yerusalemu pasipo wazazi wake kujua. 44 Wao walidhani yupo nao kwenye msafara kwa hiyo wakaenda mwendo wa siku nzima. Walipotambua kwamba hawakuwa naye, walianza kumtafuta kati ya jamaa na marafiki. 45 Hawakumpata, kwa hiyo wakarudi Yerusalemu wakimtafuta. 46 Siku ya tatu wakamkuta Hek aluni ameketi kati ya walimu wa sheria, akiwasikiliza na kuwau liza maswali. 47 Wote waliomsikia walistaajabishwa na uwezo wake mkubwa wa kuelewa na majibu aliyoyatoa.

48 Wazazi wake walipomwona walishangaa. Mama yake akamwul iza: “Mwanangu, mbona umetufanyia hivi? Baba yako na mimi tume hangaika kukutafuta kila mahali kwa wasiwasi mkubwa.” 49 Lakini yeye akajibu: “Kwa nini mlihangaika kunitafuta? Hamkujua ninge kuwa hapa Hekaluni kwenye nyumba ya Baba yangu? 50 Lakini wao hawakuelewa maana ya jibu lake.

51 Akarudi pamoja na wazazi wake hadi Nazareti. Akawa aki watii, na mama yake akayaweka moyoni mambo haya yote. 52 Basi Yesu akaendelea kuongezeka katika kimo na hekima, akipendwa na

Yohana Mbatizaji Aanza Kuhubiri

Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Neno la Mungu lilimfikia Yohana mwana wa Zakaria alipokuwa nyikani. Wakati huo Pontio Pilato alikuwa mtawala wa Yudea; Her ode mtawala wa Galilaya, nduguye Filipo mtawala wa Iturea na Tra koniti; na Lisania alikuwa mtawala wa Abilene. Anasi na Kayafa walikuwa makuhani wakuu.

Yohana akazunguka sehemu zote za kando kando ya mto Yordani akihubiri kwamba watu watubu na kubatizwa ili wasamehewe dhambi zao. Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu aitae nyikani, ‘Mtayarishieni Bwana njia , nyoosheni sehemu zote atakazopita, jazeni kila bonde, sawazisheni milima yote. Na watu wote watamwona Mwokozi aliyetumwa na Mungu.’ ”

Yohana akawaambia wale waliokuja ili awabatize, “Enyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya muepuke hukumu ya Mungu ita kayokuja? Kama kweli mmetubu, basi onyesheni kwa matendo yenu. Wala msidhani kuwa mtasamehewa kwa kuwa ninyi ni uzao wa Ibra himu. Nawaambia wazi, Mungu anaweza kabisa kumpa Ibrahimu watoto kutoka katika haya mawe! Na hivi sasa hukumu ya Mungu, kama shoka kwenye shina la mti, iko juu yenu. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa katwa na kutupwa motoni.”

10 Watu wakamwuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?” 11 Aka waambia: “Aliye na nguo mbili amgawie asiye na nguo; kama una chakula wape wenye njaa.”

12 Watoza kodi nao pia walikuja ili wabatizwe; wakamwuliza, “Bwana, na sisi inatupasa tufanyeje?”

13 Akawajibu: “ Msimdhulumu mtu kwa kudai kodi zaidi ya ile iliyoamriwa.”

14 Na baadhi ya askari wakamwuliza, “Na sisi je, tufanye nini?” Akawajibu: “Msichukue fedha za watu kwa kutumia nguvu; msiwashtaki watu kwa kuwasingizia makosa; bali mtosheke na misha hara yenu!”

15 Siku hizo watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wakijiuliza mioyoni mwao kama Yohana ndiye Kristo.

16 Yohana aliwajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji. Lakini anayekuja ni mkuu kuliko mimi, sistahili hata kuwa mtumwa wake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.

17 “Yuko tayari na pepeto lake mkononi, tayari kusafisha mahali pake pa kukusanyia mazao. Nafaka safi ataiweka ghalani lakini makapi atayachoma kwa moto usiozimika.”

18 Yohana alitumia mifano mingine mingi kuwaonya watu na kuwatangazia Habari Njema. 19 Lakini Yohana alipomkanya Herode kuhusu uhusiano wake na Herodia mke wa kaka yake, na maovu men gine aliyofanya, 20 Herode aliongezea uovu huo kwa kumfunga

Kubatizwa Kwa Bwana Yesu

21 Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye alibatizwa. Na alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka. 22 Roho Mtakatifu akash uka juu yake kama hua; na sauti ikasikika kutoka mbinguni ikisema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, ninapendezwa nawe.”

Ukoo Wa Bwana Yesu

23 Yesu alikuwa na umri wa miaka kama thelathini hivi ali poanza kazi ya kuhubiri. Yesu alijulikana kama mtoto wa Yusufu. Yusufu alikuwa mwana wa Eli, 24 Eli alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi, Lawi alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Yanai, Yanai alikuwa mwana wa Yusufu 25 Yusufu alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Amosi, Amosi alikuwa mwana wa Nahumu, Nahumu alikuwa mwana wa Esli, Esli ali kuwa mwana wa Nagai, 26 Nagai alikuwa mwana wa Maathi, Maathi alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Semeini, Semeini alikuwa mwana wa Yoseki, Yoseki alikuwa mwana wa Yoda, 27 Yoda alikuwa mwana wa Yoanani, Yoanani alikuwa mwana wa Resa, Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli, Zerubabeli alikuwa mwana wa Shealtieli, Shealtieli alikuwa mwana wa Neri, 28 Neri alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Adi, Adi alikuwa mwana wa Kosamu, Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu, Elmadamu alikuwa mwana wa Eri, 29 Eri alikuwa mwana wa Yoshua, Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri, Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu, Yorimu alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi, 30 1Lawi alikuwa mwana wa Simeoni, Simeoni alikuwa mwana wa Yuda, Yuda alikuwa mwana wa Yusufu, Yusufu alikuwa mwana wa Yonamu, Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu, Eliakimu alikuwa mwana wa Melea, 31 Melea alikuwa mwana wa Mena, Mena alikuwa mwana wa Matatha, Matatha alikuwa mwana wa Nathani, Nathani alikuwa mwana wa Daudi, 32 Daudi alikuwa mwana wa Yese, Yese alikuwa mwana wa Obedi, Obedi alikuwa mwana wa Boazi, Boazi alikuwa mwana wa Salmoni, Salmoni alikuwa mwana wa Nashoni, 33 Nashoni alikuwa mwana wa Aminadabu, Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu, Aramu alikuwa mwana wa Hesroni, Hesroni alikuwa mwana wa Peresi, Peresi alikuwa mwana wa Yuda, 34 Yuda alikuwa mwana wa Yakobo, Yakobo alikuwa mwana wa Isaki, Isaki alikuwa mwana wa Abrahamu, Abrahamu alikuwa mwana wa Tera, Tera alikuwa mwana wa Nahori, 35 Nahori alikuwa mwana wa Serugi, Serugi alikuwa mwana wa Ragau, Ragau alikuwa mwana wa Pelegi, Pelegi alikuwa mwana wa Eberi, Eberi alikuwa mwana wa Sala, 36 Sala alikuwa mwana wa Kenani, Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi, Arfaksadi alikuwa mwana wa Shemu, Shemu alikuwa mwana wa Nuhu, Nuhu alikuwa mwana wa Lameki, 37 Lameki alikuwa mwana wa Methusela, Methusela alikuwa mwana wa Henoko, Henoko alikuwa mwana wa Yaredi, Yaredi alikuwa mwana wa Mahalaleli, Mahalaleli alikuwa mwana wa Kenani, 38 Kenani alikuwa mwana wa Enoshi, Enoshi alikuwa mwana wa Sethi, Sethi alikuwa mwana wa Adamu,

Yesu Ajaribiwa Na Shetani

Kisha Yesu, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akarudi kutoka Yordani akaongozwa hadi jangwani. Alikaa huko jangwani siku arobaini akijaribiwa na shetani. Siku zote hizo hakula cho chote , kwa hiyo baada ya muda huo aliona njaa.

Shetani akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”

Yesu akamjibu, “Imeandikwa katika maandiko, ‘mtu haishi kwa chakula tu.’ ”

Kisha shetani akamchukua hadi juu ya mlima mrefu akamwo nyesha kwa mara moja milki zote za dunia. 6-7 Akamwambia, “Uki piga magoti na kuniabudu, nitakupa uwezo juu ya milki zote hizi na fahari yake; maana ni zangu na ninaweza kumpa ye yote nita kaye.” Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na kumtumikia yeye peke yake.’ ”

9-11 Ndipo shetani akamfikisha Yerusalemu, akampand isha juu ya mnara wa Hekalu, akamwambia: “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kwani imeandikwa, ‘Mungu ataamrisha mal aika wake wakulinde

12 Yesu akamwambia, “Pia imeandikwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’ ”

Mungu wako.’ ”

13 Basi Shetani alipomaliza majaribu yote, akamwacha Yesu kwa muda.

Yesu Ahubiri Galilaya

14 Kisha Yesu akarudi Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu. Habari zake zikaenea katika sehemu zote za wilaya ile. 15 Alifundisha katika masinagogi yao na wote wakamsifu.

Yesu Akataliwa Na Watu Wa Nazareti

16 Baadaye Yesu akaenda Nazareti, mahali alipokulia. Siku ya sabato alikwenda katika sinagogi kama kawaida yake. Akasimama ili asome Maandiko. 17 Akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifun gua mahali palipoandikwa: 18-19 “Roho wa Bwana yu juu yangu. Amenichagua kuwahubiria maskini Habari Njema. Amenituma kuwatan gazia wafungwa kuwa wako huru, kuwaambia vipofu kuwa wanaweza kuona tena; na kuwaweka huru wanaoonewa, na nitangaze mwaka ambao Bwana atawabariki watu wake.” 20 Akakifunga kitabu, akamrud ishia mtumishi, akaketi; na watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho. 21 Ndipo akasema: “Maandiko haya mliyosikia nikisoma, leo yametimia.”

22 Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake mazuri, wakaulizana, “Je, huyu si yule mtoto wa Yusufu?” 23 Lakini akawajibu, “Bila shaka mtaniambia, ‘Daktari, jiponye! Mbona hutendi hapa kijijini kwako miujiza tuliyosikia kuwa umeifanya kule Kapernaumu?’ 24 Ningependa mfahamu ya kwamba hakuna nabii anayekubaliwa na watu kijijini kwake. 25 Nawahakik ishieni kwamba walikuwepo wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mvua ilipoacha kunyesha kwa miaka mitatu na nusu, pakawepo na njaa kuu nchi nzima. 26 Lakini Eliya hakutumwa kumwokoa hata mmojawapo wa hawa wajane, isipokuwa alitumwa kwa mjane mmoja wa kijiji cha Sarepta katika nchi ya Sidoni. 27 Na pia wakati wa nabii Elisha, walikuwepo wakoma wengi katika Israeli; lakini hakumtakasa hata mmoja wao, ila Naamani ambaye alikuwa raia wa Siria.”

Siria.”

28 Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, waka kasirika sana. 29 Wakasimama wote wakamtoa nje ya mji hadi kwe nye kilele cha mlima ambapo mji huo ulijengwa ili wamtupe chini kwenye mteremko mkali. 30 Lakini yeye akapita katikati yao akaenda zake. Yesu Afukuza Pepo Mchafu

31 Kisha akaenda Kapernaumu, mji ulioko wilaya ya Galilaya, na siku ya sabato akawafundisha watu katika sinagogi. 32 Walis taajabishwa na mafundisho yake, maana maneno yake yalikuwa na mamlaka. 33 Alikuwepo mtu mmoja katika sinagogi aliyekuwa ame pagawa na pepo mchafu, naye alianza kupiga kelele kwa nguvu akisema, 34 “Unataka kutufanya nini, Wewe Yesu wa Nazareti? Ume kuja kutuangamiza? Nakufahamu wewe ni nani. Wewe ni Mtakatifu wa Mungu.” 35 Yesu akamwamuru yule pepo: “Nyamaza! Mtoke!” Yule pepo akamwangusha chini yule mtu mbele yao, akamtoka pasipo kumd huru. 36 Watu wote wakashangaa wakaambiana, “Mafundisho ya mtu huyu ni ya ajabu. Anawaamuru pepo wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka! 37 Habari zake zikaenea pote katika mkoa ule.

Yesu Awaponya Wengi

38 Alipotoka katika sinagogi Yesu alikwenda nyumbani kwa Simoni na alipofika huko alimkuta mama mkwe wa Simoni ana homa kali. Wakamwomba sana amponye. 39 Basi Yesu akasimama kando ya kitanda chake akaiamuru ile homa imtoke. Homa ikamtoka yule mama. Akaamka mara moja akaanza kuwahudumia. 40 Jua lilipokuwa likichwa, wote waliokuwa na wagonjwa wenye maradhi mbalimbali waliwaleta kwa Yesu. Akamgusa kila mgonjwa, akawaponya wote. 41 Pepo wachafu pia waliwatoka watu wengi, nao walipokuwa wakitoka wakapiga kelele wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea na kuwazuia wasiseme, kwa maana walifahamu kuwa yeye ni Kristo.

42 Kesho yake, kulipopambazuka, Yesu alikwenda mahali pa faragha. Watu wengi wakawa wanamtafuta kila mahali, na walipom wona wakajaribu kumzuia asiondoke. 43 Lakini yeye akawaambia, “Ninao wajibu wa kuhubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu sehemu nyingine pia. Hii ndio sababu nilitumwa.” 44 Kwa hiyo akaende lea kuhubiri katika masinagogi ya Yudea. Yesu Awachagua Wanafunzi Wa Kwanza

Siku moja Yesu alipokuwa amesimama akihubiri karibu na ziwa la Genesareti, watu wengi walimsonga ili wapate kusikia neno la Mungu. Akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa, lakini wenye mashua walikuwa wakiosha nyavu zao. Akaingia katika mashua moja, akamwomba mwenye mashua, ambaye jina lake lilikuwa Simoni, aisogeze zaidi katika maji. Kisha akakaa kwenye mashua, akaanza kuwafundisha.

Alipokwisha zungumza na watu akamwambia Simoni, “Sasa ipe leke mashua hadi mahali penye kina kirefu, kisha mshushe nyavu zenu nanyi mtapata samaki.”

Simoni akamjibu, “Bwana, tumekesha usiku kucha tukivua na hatukuambulia kitu cho chote. Lakini, kwa kuwa wewe umesema, tutazishusha nyavu.” Nao walipofanya kama Yesu alivyowaagiza, nyavu zao zikajaa samaki, zikaanza kuchanika! Wakawaashiria wavuvi wa ile mashua nyingine waje kuwasaidia. Mashua zote mbili zikajaa samaki hata karibu kuzama.

Simoni Petro alipoona yaliyotokea alipiga magoti mbele ya Yesu akamwambia, “Bwana,tafadhali uniache kwa maana mimi ni mwe nye dhambi.” Kwa kuwa yeye na wavuvi wenzake walikuwa wamesh angazwa sana na wingi wa samaki waliopata. 10 Hali kadhalika wavuvi wa ile mashua nyingine, Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo walishangazwa pia. Ndipo Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope; tangu sasa utakuwa mvuvi wa watu.”

11 Nao walipokwisha fikisha mashua yao nchi kavu, wakaacha vyote, wakamfuata Yesu. Yesu Amponya Mwenye Ukoma

12 Siku moja Yesu alipokuwa katika mji fulani alitokea mtu mwenye ukoma mwili mzima. Alipomwona Yesu alijitupa chini kwa kunyenyekea akamsihi akisema, “Bwana, ukitaka unaweza kunita kasa!” 13 Yesu akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Ndio, nataka upone; takasika!” Wakati huo huo, ukoma wote ukamtoka . 14 Yesu akamwambia, “Usimweleze mtu ye yote jinsi ulivyopata kupona bali nenda moja kwa moja hadi kwa kuhani ili aone kuwa kweli umepona. Kisha utoe sadaka ya shukrani, kama she ria ya Musa inavyoagiza, ili kuthibitisha kuwa umetakasika.”

15 Lakini sifa za Yesu zikazidi sana kuenea. Watu wakamimi nika kwa wingi kutoka kila upande kuja kumsikiliza na kuponywa maradhi yao. 16 Ila mara kwa mara alitoka peke yake akaenda pasipo na watu akaomba.

Yesu Amponya Mwenye Kupooza

17 Siku moja Yesu alipokuwa akifundisha, Mafarisayo na wal imu wa sheria kutoka katika kila mji wa wilaya za Galilaya, Yudea na Yerusalemu walikuwepo. Na Yesu alikuwa amejaa nguvu ya Mungu ya kuponya wagonjwa.

18-19 Kisha wakaja watu wamembeba mgonjwa aliyepooza kwe nye kitanda. Wakajaribu kumpitisha ndani wamfikishe alipokuwa Yesu, lakini wakashindwa kwa sababu ya msongamano wa watu. Basi wakampandisha juu ya paa, wakaondoa baadhi ya vigae, wakapata nafasi ya kumteremsha yule mgonjwa pamoja na kitanda chake kwa kamba, hadi mbele ya Yesu. 20 Alipoona imani yao, Yesu alimwam bia yule mgonjwa, “Rafiki yangu, umesamehewa dhambi zako.” 21 Wale walimu wa sheria na Mafarisayo wakaanza kusemezana, “Mbona huyu anakufuru! Anadhani yeye ni nani? Hakuna awezae kusamehe dhambi ila Mungu peke yake.”

22 Yesu alifahamu mawazo yao kwa hiyo akawauliza, “Kwa nini mnafikiri mimi ninakufuru? 23 Je, ni lipi lililo rahisi zaidi, kumwambia huyu, ‘Umesamehewa dhambi zako’; au kusema, ‘Simama utembee?’ 24 Sasa nitawahakikishia kuwa mimi Mwana wa Adamu ninao uwezo wa kusamehe dhambi duniani.” Akamgeukia yule mgonjwa aliyepooza, akasema, “Nakuambia: Simama! Chukua kitanda chako uende nyumbani.” 25 Mara yule mtu aliyekuwa amepooza akasimama mbele yao wote, akachukua kitanda chake akaenda zake nyumbani, huku akimtukuza Mungu. 26 Wote waliokuwepo wakastaajabu sana. Wakajaa hofu. Wakamtukuza Mungu, wakasema, “Tumeona maajabu leo.”

Yesu Amwita Lawi

27 Baada ya haya Yesu alimwona afisa mmoja mtoza kodi jina lake Lawi akiwa ofisini mwake, akamwambia, “Njoo uwe mmoja wa wanafunzi wangu.” 28 Lawi akaacha vyote, akaondoka, akamfuata Yesu. 29 Baadaye Lawi akafanya karamu kubwa kumkaribisha Yesu nyumbani kwake. Watoza kodi wengi walikuwa miongoni mwa watu wal ioalikwa. 30 Basi baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria ambao walikuwa kundi moja wakawalalamikia wanafunzi wa Yesu wakisema, “Mbona mnakula na kunywa na wenye dhambi?” 31 Yesu akawajibu, “Wenye afya hawahitaji daktari, lakini wagonjwa wanamhitaji. 32 Sikuja kwa ajili ya wenye haki bali nimekuja kuwaita wenye dhambi ili watubu.”

Yesu Aulizwa Habari Za Kufunga

33 Baadhi ya watu wakamwuliza Yesu, “Wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo hufunga na kusali mara kwa mara. Mbona wanafunzi wako wanakula na kunywa tu?”

34 Yesu akawajibu, “Je, inawezekana wageni walioalikwa har usini kufunga wakati wakiwa na Bwana Harusi? 35 Lakini wakati utafika ambapo Bwana Harusi ataondolewa. Wakati huo ndipo wataka pofunga.

36 Yesu akawapa mfano akawaambia: “Hakuna mtu anayechana nguo mpya ili apate kiraka cha kuweka kwenye nguo kuu kuu. Akifa nya hivyo ataharibu ile nguo mpya na ile kuu kuu itaonekana mbaya zaidi ikiwa na kiraka kipya. 37 Wala watu hawaweki divai mpya katika viriba vilivyochakaa; ukifanya hivyo, hivyo viriba vitapa suka na divai yote itamwagika. 38 Divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya. 39 Na pia hakuna mtu anayependelea divai mpya baada ya kunywa divai iliyoiva vizuri. Kwa maana husema, ‘Hii divai iliyoiva siku nyingi ni bora zaidi.’ ”

Bwana Wa Sabato

Siku moja ya sabato Yesu alikuwa akipita katika mashamba ya ngano. Wanafunzi wake wakawa wakivunja masuke ya ngano, wakayafi kicha na kula punje zake. Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnavunja sheria kwa kuvuna ngano siku ya sabato?”

Yesu akawajibu, “Ninyi hamsomi Maandiko? Hamjasoma alicho fanya Mfalme Daudi wakati yeye na wafuasi wake walipokuwa na njaa? Aliingia Hekaluni, akachukua ile mikate ya madhabahuni -ambayo huliwa na makuhani peke yao -akala, kisha akawapa na wafuasi wake wakala!” Akaongezea kusema, “Mimi Mwana wa Adamu ni Bwana wa sabato.”

Ikawa siku nyingine ya sabato Yesu alikuwa akifundisha katika sinagogi, na alikuwepo mtu ambaye mkono wake wa kuume uli kuwa umepooza. Walimu wa sheria na Mafarisayo wakawa wanangoja waone kama atamponya mtu siku ya sabato ili wapate sababu ya kumshtaki. Lakini Yesu alifahamu mawazo yao. Kwa hiyo akamwam bia yule aliyepooza mkono, ’Njoo usimame hapa mbele ili kila mtu akuone.” Yule mtu akaja mbele. Kisha Yesu akawageukia wale walimu wa sheria na Mafarisayo akasema, “Nawauliza ninyi, ni lipi lililo halali siku ya sabato - kutenda mema au kutenda mabaya? Kuokoa maisha au kuyaangamiza?” 10 Akawatazama watu wote waliokuwepo. Kisha akamwambia yule aliyepooza mkono, “Nyoosha mkono wako!” Akaunyoosha na mkono wake ukapona kabisa! 11 Wale wakuu wakakasirika sana. Wakaanza kushauriana, “Tumfa nye nini huyu Yesu?’ ’

Kuchaguliwa Kwa Mitume Kumi Na Wawili

12 Siku moja Yesu alikwenda milimani kuomba, akakesha usiku kucha akimwomba Mungu. 13 Asubuhi akawaita wanafunzi wake, na kati yao akachagua kumi na wawili akawapa cheo cha “mitume.” Majina yao ni haya: 14 Simoni, aliyemwita Petro; Andrea, nduguye Simoni; Yakobo; Yohana; Filipo; Bartholomayo; 15 Mathayo; Tomaso; Yakobo, mwana wa Alfayo; Simoni, aliyeitwa Mzalendo; 16 Yuda, mwana wa Yakobo; na Yuda Iskariote, ambaye baadaye alimsaliti Yesu.

Yesu Aponya Wengi

17 Akashuka pamoja nao akasimama mahali penye uwanja tambar are. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati mkubwa wa watu waliotoka sehemu zote za Yudea na Yerusalemu na kutoka pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walikuwa wamekuja kumsiki liza na kuponywa magonjwa yao. 18 Hata wale waliokuwa wakiteswa na pepo wachafu nao walimjia akawaponya. 19 Na watu wote wali kuwa wanajitahidi kumgusa kwa maana walipofanya hivyo, nguvu zil ikuwa zikimtoka na kuwaponya wote.

20 Kisha akawatazama wanafunzi wake akasema, “Mmebarikiwa ninyi mlio maskini kwa sababu Ufalme wa mbinguni ni wenu! 21 Mmebarikiwa ninyi mlio na njaa sasa, kwa sababu mtashibishwa! Mmebarikiwa ninyi mnaolia sasa, kwa sababu mtacheka. 22 Mmebari kiwa ninyi watu watakapowachukia na kuwakataa na kuwatukana na kuharibu sifa yenu kwa ajili yangu. 23 Yatakapotokea haya fura hini na kuruka ruka kwa furaha kwa sababu zawadi kubwa imewekwa mbinguni kwa ajili yenu. Hata baba zao waliwatendea manabii wa zamani vivyo hivyo.

24 “Lakini ole wenu ninyi matajiri, kwa sababu mmekwisha pata furaha yenu! Ole wenu ninyi mlioshiba, maana mtaona njaa! 25 Ole wenu ninyi mnaocheka sasa, maana mtalia na kuomboleza! 26 Ole wenu mtakaposifiwa na watu, kwani ndivyo baba zao walivy owasifu manabii wa uongo.”

Wapendeni Adui Zenu

27 “Sikieni niwaambie, wapendeni adui zenu. Watendeeni mema wanaowachukia. 28 Wabarikini wanaowalaani, waombeeni mema wanaowaumiza. 29 Mtu akikupiga kofi, mgeuzie na shavu la pili. Mtu akikunyang’anya koti lako, usimzuie kuchukua na shati lako pia. 30 Aombae mpe, na mtu akichukua mali yako usidai urudishiwe. 31 Watendee wengine unavyopenda nao wakutendee. 32 Je, kuna sifa gani mnapowapenda watu wawapendao? Hata wasiomjua Mungu huwapenda wawapendao. 33 Tena kuna sifa gani mnapowatendea mema wale wanaowatendea mema? Hata wasiomjua Mungu hufanyiana hivyo. 34 Tena mnapowakopesha wale tu ambao mnategemea kuwa watawalipa, kuna sifa gani? Hata watu wasiomjua Mungu huwakopesha wenye dhambi wenzao wakiwa na hakika ya kurudishiwa mali yao yote. 35 Bali, wapendeni adui zenu, watendeeni mema. Wakopesheni bila kutegemea kurudishiwa mlichokopesha. Ndipo mtapata zawadi kubwa nanyi mtakuwa wana wa Mungu Aliye Juu. Yeye ni mwema kwa watu wasio na shukrani na watu waovu. 36 Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.”

Msiwahukumu Wengine

37 “Msiwahukumu wengine nanyi hamtahukumiwa. Msilaani, nanyi hamtalaaniwa. Wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa. 38 Muwe wepesi wa kutoa nanyi mtapokea. Kipimo mtakachotoa mtar udishiwa kikiwa kimejaa na kushindiliwa na kutikiswa na kufurika. Kwa kuwa jinsi mtakavyotoa, ndivyo mtakavyopata.”

Kwa kuwa jinsi mtakavyotoa, ndivyo mtakavyopata.”

39 Pia akawapa mfano akasema, “Je, kipofu anaweza kumwon goza kipofu mwenzake? Si wote wawili watatumbukia shimoni? 40 Mwanafunzi hawezi kuwa mjuzi kuliko mwalimu wake, ila akihi timu, anaweza kuwa bingwa kama mwalimu wake. 41 Mbona unatazama sana kipande kilichoko katika jicho la mwenzako nawe huoni pande lililoko ndani ya jicho lako? 42 Utawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Ndugu yangu, hebu, nikusaidie kutoa kipande hicho ndani ya jicho lako,’ wakati wewe mwenyewe huoni pande hilo lililoko ndani ya jicho lako? Mnafiki wewe! Ondoa kwanza pande hilo ndani ya jicho lako, na ndipo utakapoweza kuona vizuri na kuondoa kipande kili choko ndani ya jicho la ndugu yako.

43 “Hakuna mti bora uzaao matunda hafifu wala hakuna mti hafifu uzaao matunda bora. 44 Kila mti hutambuliwa kwa matunda yake. Tini hazichumwi kwenye michongoma wala zabibu hazichumwi kwenye majani mwitu. 45 Hali kadhalika mtu mwema hutambulikana kwa matendo yake mazuri yatokayo katika moyo mwema. Mtu mwovu pia hutenda maovu yatokanayo na uovu uliojaa ndani ya moyo wake. Mtu hunena yale yaliyojaa moyoni mwake.

46 “Kwa nini mnaniita, ‘Bwana, Bwana’ nanyi hamfanyi ninay owaambia?

47 Nitawaambieni alivyo mtu anayesikia na kufanya ninay osema. 48 Yeye ni kama mtu aliyejenga nyumba akachimba chini na kujenga msingi kwenye mwamba. Mafuriko yalipotokea, yakaikumba ile nyumba wala haikutikisika, kwani ilikuwa na msingi imara. 49 Lakini yeye ayasikiaye maneno yangu na asiyafuate, ni kama mtu aliyejenga nyumba juu ya mchanga bila kuweka msingi. Mafuriko yalipoikumba nyumba ile, ilianguka mara, na kuporomoka kabisa.”

Yesu alipomaliza kuwaambia watu mambo haya alikwenda Kaper naumu. Huko mtumishi wa jemadari mmoja wa Kirumi ambaye bwana wake alimpenda, alikuwa mgonjwa sana, karibu ya kufa. Jemadari huyo aliposikia habari za Yesu aliwatuma wazee wa Kiyahudi wakam wombe aje kumponya mtumishi wake. Wale wazee walipofika kwa Yesu walimsihi sana amsaidie yule jemadari wakisema, “Mtu huyu anastahili msaada wako kwani yeye analipenda taifa letu, tena ametujengea sinagogi.”

Hivyo Yesu akaongozana nao. Hata alipoikaribia nyumba yake, yule jemadari aliwatuma rafiki zake, kumwambia Yesu, “Bwana, usijisumbue kuingia nyumbani kwangu. Sistahili heshima kubwa kiasi hicho, wala sikuona ninastahili mimi kuja kukuona binafsi. Sema neno moja tu na mtumishi wangu atapona. Katika nafasi yangu ya kazi nina wakubwa wangu na wapo askari wengine chini ya mamlaka yangu. Nikitoa amri kwa askari, ‘Nenda!’ huenda; nikimwambia mwingine, ‘Njoo!’ huja; na nikimwambia mtumishi wangu, ‘Fanya hiki,’ hufanya.” Yesu aliposikia maneno haya alishangaa sana. Akawageukia wale watu walioongozana naye aka waambia, “Hata katika Israeli yote sijakutana na mtu mwenye imani kama hii.” 10 Na wale waliotumwa kwa Yesu waliporudi nyumbani kwa yule jemadari walikuta yule mtumishi amepona kabisa.

Yesu Amfufua Mtoto Wa Mjane

11 Baada ya siku hiyo, Yesu alikwenda mji mmoja uitwao Naini. Wanafunzi wake na umati wa watu waliongozana naye. 12 Alipokaribia njia ya kuingia mjini alikutana na watu wal iobeba maiti wakitoka nje ya mji. Marehemu alikuwa mtoto wa kiume wa pekee wa mama mmoja mjane na umati wa watu wa mji ule ulikuwa pamoja na huyo mama. 13 Bwana Yesu alipomwona yule mjane moyo wake ulijaa huruma, akamwambia, “Usilie.” 14 Kisha akalisoge lea lile jeneza akaligusa na wale waliolibeba wakasimama. Ndipo akasema: “Kijana nakuambia, amka!” 15 Yule aliyekuwa marehemu akaamka, akakaa na akaanza kusema! Yesu akamkabidhi kwa mama yake.

16 Watu wote wakajawa na hofu. Wakamtukuza Mungu wakisema, “Nabii mkuu ametokea kati yetu. Mungu amekuja kutuokoa sisi watu wake.” 17 Habari hizi za mambo aliyofanya Yesu zikaenea Uyahudi nzima na sehemu za jirani.

Hakuna Aliye Mkuu Kuliko Yohana

18 Wanafunzi wa Yohana Mbatizaji walipomweleza Yohana habari hizi zote aliwaita wawili kati yao 19 akawatuma wakamwulize Bwana Yesu, “Wewe ndiye yule ajaye, au tumtazamie mwingine?”

201 Walipofika kwa Yesu wakamwambia, “Yohana Mbatizaji ametutuma tukuulize, ‘Wewe ndiye yule ajaye au tumtazamie mwin gine?”’

21 Wakati huo huo, Yesu aliwaponya wengi waliokuwa na magonjwa, maumivu na pepo wachafu. Pia akawawezesha vipofu wengi kuona. 22 Ndipo akawajibu wale wanafunzi waliotumwa, “Nendeni mkamwambie Yohana yote mliyoyaona na kusikia: vipofu wanapata kuona, vilema wanatembea, wenye ukoma wanapona, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa na maskini wanasikia Habari Njema. 23 Amebari kiwa mtu asiyepoteza imani yake kwangu.” 24 Wanafunzi wa Yohana walipoondoka, Yesu akaanza kuwaeleza watu juu ya Yohana: “Hivi mlipokwenda nyikani mlikwenda kuona nini? Nyasi zikipeperushwa na upepo? 25 Kama sivyo, mlikwenda kuona nini basi? Mtu aliyevaa nguo za fahari? Sidhani! Watu wanaovaa nguo za fahari na kuishi maisha ya anasa hukaa katika majumba makubwa. 26 Sasa mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kuona nabii? Naam! Tena aliye mkuu kuliko nabii. 27 Huyu Yohana ndiye anayezungumzwa katika Maandiko yase mayo: ‘Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie, ili akuandalie njia.’ 28 Nawaambia, kati ya binadamu wote, hakuna aliye mkuu kumzidi Yohana. Hata hivyo aliye mdogo kabisa katika Ufalme wa Mungu ni mkuu kuliko Yohana. 29 Watu wote waliosikia maneno hayo, ikiwa ni pamoja na watoza ushuru, walimtukuza Mungu kwa kuwa wao waliukubali ubatizo wa Yohana. 30 Bali Mafarisayo na wanasheria walikataa mpango wa Mungu kwao kwa kutokukubali kubatizwa na Yohana. 31 Yesu akawau liza, “Niseme nini juu ya watu wa kizazi hiki? Niwafananishe na nini? 32 Wao wamefanana na watoto waliokaa sokoni wakijibizana na wenzao wakisema: ‘Tuliwaimbia nyimbo za shangwe, hamkucheza. Tuliwaimbia nyimbo za msiba, hamkuomboleza.’ 33 Yohana Mbatizaji alikuwa akifunga na hakuonja divai maishani mwake, ninyi mkasema, ‘Ana wazimu!’ 34 Lakini mimi nakula na kunywa, nanyi mnasema: ‘Mtazameni mlafi na mlevi! Rafiki wa watoza kodi na wenye dhambi.’ 35 Lakini hekima ya Mungu inadhihirishwa kuwa kweli na wote wanaoipokea.”

Mwanamke Aliyempaka Yesu Manukato

36 Farisayo mmoja alimwalika Yesu nyumbani kwake kwa chak ula. Naye akaenda akakaa ale chakula. 37 Katika mji ule palikuwa na mwanamke mmoja kahaba. Naye aliposikia kuwa Yesu atakula nyum bani kwa yule Farisayo, alichukua chupa ya alabasta iliyojaa man ukato 38 akaenda, akakaa nyuma ya Yesu, karibu na miguu yake. Kisha akaanza kulia, machozi yake yakidondokea miguuni mwa Yesu, akayafuta kwa nywele zake. Huku akimbusu miguu na kuimiminia yale manukato.

39 Yule Farisayo aliyemwalika Yesu alipoona yanayotendeka, akawaza moyoni mwake, “Huyu mtu hawezi kuwa ni nabii. Kama ange kuwa nabii angetambua kuwa huyu mwanamke ni kahaba.” 40 Kisha Yesu akijua mawazo ya yule Farisayo akamwambia, “Simoni, kuna jambo nataka kukuambia.” Simoni akajibu “Sema, mwalimu.” 41 “Palikuwa na mtu mmoja aliyewakopesha watu wawili fedha: mmoja shillingi elfu tano na mwingine shillingi mia tano. 42 Wote wawili wakashindwa kulipa madeni yao, kwa hiyo akaamua kuwasamehe. Unadhani kati yao, ni yupi aliyempenda zaidi yule aliyewasamehe?” 43 Simoni akajibu, “Nadhani ni yule aliyesame hewa deni kubwa zaidi.” Yesu akamwambia, “Umejibu sawa.” 44 Ndipo akamgeukia yule mwanamke akamwambia Simoni, “Unamwona mwanamke huyu? Niliingia nyumbani kwako hukunipa maji ya kunawa miguu, lakini huyu ameniosha miguu kwa machozi yake na kunifuta kwa nywele zake. 45 Hukunisalimu kwa busu, lakini huyu mwanamke amekuwa akiibusu miguu yangu tangu niingie hapa. 46 Hukunipaka mafuta kichwani kama ilivyo desturi lakini huyu mwanamke ameipaka miguu yangu manukato. 47 Kwa hiyo nakuambia, upendo mkubwa aliouonyesha huyu mama unathibitisha kuwa dhambi zake ambazo ni nyingi zimesamehewa. Lakini ye yote asamehewaye kidogo, huonyesha upendo kidogo.”

48 Akamwambia yule mwanamke, “Dhambi zako zimesamehewa.” 49 Ndipo wale wageni wengine waliokuwepo wakaanza kuulizana, “Hivi huyu ni nani, hata aweze kusamehe dhambi?” 50 Yesu akam wambia yule mwanamke, “Imani yako imekuokoa; nenda kwa amani.”

Baada ya haya Yesu alikwenda katika miji na vijiji akifu atana na wanafunzi wake. Kila alipokwenda alihubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu.

Baadhi ya wanawake aliokuwa amewatoa pepo wachafu na kuwa ponya walifuatana naye. Miongoni mwao alikuwepo Mariamu ambaye aliitwa Magdalena, aliyetolewa pepo saba; Yohana mke wa Chuza -msimamizi wa ikulu ya Herode; Susana, na wengine wengi. Wana wake hawa walimhudumia Yesu na wanafunzi wake kutokana na mapato yao wenyewe.

Watu wengi walimiminika kutoka katika kila mji na umati mkubwa ulipokusanyika, Yesu akawaambia mfano huu: “Mkulima mmoja alikwenda shambani kwake kupanda mbegu. Alipokuwa akitawa nya mbegu, nyingine zilianguka njiani zikakanyagwa kanyagwa; na ndege wakazila. Na mbegu nyingine zilianguka penye miamba na zilipomea zikakauka kwa kukosa unyevu. Na mbegu nyingine zil ianguka kwenye miiba, ikazisonga zikafa. Mbegu nyingine zilian guka penye udongo mzuri, nazo zikamea na kutoa mazao mara mia zaidi ya mbegu alizopanda.” Baada ya kutoa mfano huu akasema: “Mwenye nia ya kusikia na asikie!”

Wanafunzi wake wakamwuliza maana ya mfano huu. 10 Naye akawajibu, “Ninyi mmejaliwa kufahamu siri za Ufalme wa Mungu, lakini kwa wengine nazungumza kwa mifano ili, ‘Kuangalia waan galie lakini wasione, kusikia wasikie, lakini wasielewe.’ 11 Maana ya mfano huu ni hii: Mbegu ni neno la Mungu. 12 Ile njia zilipoanguka baadhi ya mbegu, ni mfano wa watu wanaolisikia neno la Mungu lakini shetani huja akalichukua kutoka katika mioyo yao, ili wasiamini na kuokolewa. 13 Ile miamba ambamo mbegu nyingine zilianguka ni sawa na watu ambao hufurahia kusikia mahu biri lakini neno la Mungu halipenyi ndani ya mioyo yao. Hawa huamini kwa muda mfupi lakini wanapojaribiwa hupoteza imani yao. 14 Na ile miiba ambamo mbegu nyingine zilianguka ni sawa na wale wanaosikia neno la Mungu lakini baadaye imani yao inasongwa na mahangaiko ya maisha, utajiri, shughuli na anasa; wasiweze kukua. 15 Bali ule udongo mzuri ambamo mbegu nyingine zilianguka ni sawa na wale ambao hulisikia neno la Mungu na kulishika kwa moyo mwema na wa utii, wakavumilia na kuzaa matunda.”

Mfano Wa Taa

16 “Ni nani anayewasha taa kisha akaifunika, au akaiweka uvunguni, badala ya kuiweka mahali ambapo mwanga wake utaonekana? 17 Hakuna siri ambayo haitafichuliwa, wala hakuna jambo lililo fichika ambalo halitajulikana na kuwekwa wazi. 18 Kwa hiyo muwe waangalifu mnaposikiliza, kwa sababu, yeye aliye na kitu ataonge zewa, naye ambaye hana, atanyang’anywa hata kile anachodhania anacho.”

Ndugu Wa Kweli

19 Wakati mmoja mama yake Yesu na ndugu zake walikuja kum wona lakini hawakuweza kumfikia kwa sababu ya msongamano wa watu. 20 Mtu mmoja akamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje wanataka kukuona.” 21 Yesu akamjibu, “Mama yangu na ndugu zangu ni wale wote wanaolisikia neno la Mungu na kulitii.”

Bwana Yesu Atuliza Dhoruba

22 Siku moja Yesu alipanda mashua na wanafunzi wake akawaam bia, “Twendeni ng’ambo ya pili ya ziwa.” Kwa hiyo wakaanza kuvuka. Walipokuwa wakivuka, akalala usingizi. Upepo mkali ukawa unavuma na mashua yao ikaanza kujaa maji; wakawa katika hatari ya kuzama.

24 Wale wanafunzi wakamkimbilia Yesu wakamwamsha wakisema, “Bwana, Bwana, tunazama!” Ndipo akaamka akaukemea ule upepo na yale mawimbi vikakoma, pakawa shwari. 25 Kisha akawauliza, “Imani yenu iko wapi?” Wakashangaa na kuogopa. Wakaulizana, “Ni mtu wa namna gani huyu ambaye anaamuru upepo na mawimbi navyo vikamtii?”

Yesu Amponya Mtu Mwenye Pepo

26 Basi wakawasili ng’ambo ya pili katika jimbo la Wagerasi. 27 Na aliposhuka katika mashua alikutana na mtu mmoja wa mji ule aliyepagawa na pepo. Kwa muda mrefu mtu huyu alikuwa havai nguo wala kuishi nyumbani, bali aliishi makaburini. 28 Alipomwona Yesu alipiga kelele, akajitupa chini mbele yake, na kusema kwa sauti kuu, “Unataka nini kwangu, Yesu Mwana wa Mungu Aliye Juu?

Nakuomba, tafadhali usinitese!”

29 Wakati huo Yesu alikuwa ameanza kumwamuru yule pepo mchafu amtoke. Mara nyingi pepo huyo alimwingia na hata alipo fungwa na minyororo na kuwekwa chini ya ulinzi aliivunjilia mbali minyororo hiyo na kukimbilia jangwani akiwa ametawaliwa kabisa na pepo huyo. 30 Yesu akamwuliza, “Jina lako ni nani?” Akamjibu, “Jeshi’ 31 Wale pepo wachafu wakamsihi sana asiwaamuru kwenda shimoni kwenye kifungo cha mashetani.

32 Palikuwa na kundi kubwa la nguruwe hapo karibu wakilisha kando kando ya mlima. Wale pepo wakamsihi Yesu awaruhusu wawaingie hao nguruwe. Akawaruhusu.

33 Kwa hiyo wakamtoka yule mtu wakawaingia wale nguruwe. Kundi lote la nguruwe likatimka mbio katika ule mteremko mkali wakatumbukia ziwani na kuzama. 34 Watu waliokuwa wakichunga lile kundi la nguruwe waliona yaliyotokea, wakakimbia wakaeneza habari hizi mjini na mashambani.

35 Watu wakatoka kwenda kujionea wenyewe yaliyotokea. Wali pofika hapo alipokuwa Yesu wakamwona yule mtu aliyetokwa na pepo amekaa karibu na Yesu, akiwa amevaa nguo na mwenye akili timamu! Wakaogopa sana. 36 Wale walioona mambo yalivyotokea wakawasimu lia wenzao jinsi yule mtu alivyoponywa. 37 Watu wote wa jimbo hilo la Wagerasi wakamwomba Yesu aondoke kwao, kwa sababu wali kuwa wamejawa na woga. Basi akaingia katika mtumbwi akaondoka.

38 Yule mtu aliyetolewa pepo akamsihi Yesu afuatane naye. Lakini Yesu akakataa, akamwambia: 39 “Rudi nyumbani ukawaeleze mambo makuu aliyokufanyia Mungu.” Kwa hiyo yule mtu akaenda, akatangaza mji mzima mambo makuu Yesu aliyomfanyia.

Yesu Amfufua Binti Wa Yairo

40 Yesu aliporudi ng’ambo ya pili umati mkubwa wa watu ukam pokea kwa furaha, kwani walikuwa wakimngojea.

41 Wakati huo akaja mtu mmoja jina lake Yairo, kiongozi wa sinagogi. Akapiga magoti mbele ya Yesu akamwomba afike nyumbani kwake, 42 kwa kuwa binti yake mwenye umri wa miaka kumi na mbili, aliyekuwa mtoto wake wa pekee, alikuwa mgonjwa mahututi, karibu ya kufa. Yesu alipokuwa akienda, umati ulimsonga sana.

43 Katika umati huo alikuwepo mama mmoja ambaye alikuwa na ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, wala hakuna mganga aliyeweza kumponya. 44 Akaja nyuma ya Yesu, akam gusa pindo la vazi lake. Mara damu iliyokuwa ikimtoka ikakauka, akapona. 45 Yesu akauliza: “Nani amenigusa?” Kila mtu alipo kana Petro akasema, “Bwana, watu ni wengi mno wanaokusonga kila upande.” 46 Yesu akasema: “Kuna mtu aliyenigusa maana naona ya kuwa nguvu za kuponya zimenitoka.” 47 Yule mama alipofahamu ya kuwa amegundulika akaja huku akitetemeka akapiga magoti mbele ya Yesu. Akamweleza Yesu mbele ya watu wote kilichomfanya amguse, na jinsi alivyoponywa mara. 48 Basi Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani.” 49 Wakati Yesu alipo kuwa bado anasema, akaja mtumishi kutoka nyumbani kwa Yairo kum wambia, “Binti yako amefariki. Hakuna sababu ya kuendelea kum sumbua Mwalimu.” 50 Lakini Yesu aliposikia haya alimwambia Yairo, “Usiogope. Uwe na imani na binti yako atapona.” 51 Wal ipofika kwa Yairo akawazuia watu wote wasiingie ndani isipokuwa Petro, Yakobo na Yohana, na baba na mama wa yule binti. 52 Watu waliokuwepo walikuwa wakilia na kuomboleza lakini Yesu akawaam bia, “Acheni kulia! Huyu binti hajafa ila amelala!” 53 Wao wakamcheka kwa dharau maana walijua amekwisha kufa. 54 Yesu akamshika yule binti mkono akamwita: “Binti, amka!” 55 Uhai ukamrudia, naye akasimama mara moja. Yesu akaamuru apewe chakula. 56 Wazazi wake wakastaajabu sana lakini Yesu akawakataza wasim wambie mtu alivyomfufua binti yao.

Yesu Awatuma Wanafunzi Kumi Na wawili

Yesu akawaita pamoja wanafunzi wake kumi na wawili na kuwapa mamlaka na uwezo wa kufukuza pepo wote na kuponya magonjwa yote. Kisha akawatuma waende wakautangaze Ufalme wa Mungu na kuponya wagonjwa.

Akawaagiza akisema, “Msichukue cho chote safarini, wala fimbo, wala mkoba, wala chakula, wala fedha; na msichukue nguo za kubadili. Mkikaribishwa katika nyumba yo yote muwe wageni wa nyumba hiyo hadi mtakapoondoka katika kijiji hicho. Po pote ambapo hamtakaribishwa, mnapoondoka kung’uteni mavumbi miguuni mwenu kama ishara ya hukumu ya Mungu juu yao.”

Wale wanafunzi wakaondoka wakaenda kutoka kijiji hadi kijiji wakihubiri Habari Njema na kuponya wagonjwa. Habari zil imfikia Herode mtawala wa Galilaya kuhusu miujiza iliyokuwa iki fanyika, naye akafadhaika kwa kuwa baadhi ya watu walikuwa wakisema, “Yohana Mbatizaji amefufuka!” Wengine wakasema, “Ni Eliya ametutokea” na wengine kwamba, “Mmoja wa manabii wa kale amefufuka.” Herode akasema, “Yohana nilimkata kichwa, ni nani huyu anayefanya maajabu haya ninayoambiwa?” Akajaribu sana amwone Yesu.

Yesu Awalisha Watu Elfu Tano

10 Wanafunzi waliporudi walimweleza Yesu yote waliyofanya. Akawachukua wakaenda peke yao mpaka mji mmoja uitwao Bethsaida. 11 Lakini watu wengi wakafahamu alipokwenda, wakamfuata. Akawa karibisha, akawafundisha tena kuhusu Ufalme wa mbinguni na akapo nya wangonjwa. 12 Ilipokaribia jioni, wale wanafunzi kumi na wawili wakamwambia Yesu, “Waruhusu watu hawa waondoke ili waweze kujitafutia chakula na mahali pa kulala katika vijiji na mashamba ya jirani kwa maana hapa tuko nyikani.” 13 Akawajibu, “Wapeni chakula.” Wakasema, “Tunayo mikate mitano tu na samaki wawili. Unataka tukanunue chakula cha kuwatosha watu wote hawa?” 14 Kwa kuwa walikuwapo wanaume wapatao elfu tano! Lakini Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Waketisheni katika makundi ya watu hamsini-hamsini.” 15 Wakawaketisha wote. 16 Yesu akaichukua mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama mbinguni, akavi bariki na kuvimega. Kisha akawapa wanafunzi wake wawagawie wale watu. 17 Kila mtu akala na kutosheka na vilipokusanywa vipande vilivyobaki, vilijaa vikapu kumi na viwili.

Petro Amkiri Bwana Yesu Kuwa Ndiye Kristo

18 Siku moja Yesu alipokuwa akisali faraghani akiwa na wana funzi wake aliwauliza, “Watu husema mimi ni nani?” 19 Wakam wambia, “Watu husema wewe ni Yohana Mbatizaji, wengine husema ni Eliya na wengine husema wewe ni nabii wa kale aliyefufuka kutoka kwa wafu.”

20 Kisha akawauliza, “Ninyi je, mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, “Wewe ndiye Kristo wa Mungu.” 21 Yesu akawaka taza wasimwambie mtu jambo hilo 22 akisema, “Imenipasa mimi Mwana wa Adamu kupata mateso mengi na kukataliwa na wazee, maku hani wakuu na walimu wa sheria. Nitauawa na siku ya tatu nitafuf uliwa.” 23 Kisha akawaambia wote, “Ye yote anayetaka kunifuata ni lazima ajikane nafsi yake, achukue msalaba wake kila siku, anifuate. 24 Kwa maana ye yote atakayeshughulikia zaidi usalama wa nafsi yake ataipoteza. Lakini ye yote atakayeipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataisalimisha. 25 Je, kuna faida gani kwa mtu kuupata ulimwengu mzima ambapo kwa kufanya hivyo ataipoteza nafsi yake? 26 Mtu ye yote atakayenionea aibu mimi na maneno yangu, na mimi Mwana wa Adamu nitamwonea aibu mtu huyo nitakapo kuja katika utukufu wangu na wa Baba na wa malaika watakatifu. 27 Ninawaambia kweli, baadhi ya watu waliosimama hapa hawatakufa mpaka watakapouona Ufalme wa Mungu.”

Bwana Yesu Abadilika Sura

28 Yapata siku nane baada ya kusema hayo, Yesu alikwenda kusali mlimani pamoja na Petro, Yakobo na Yohana. 29 Alipokuwa akiomba, sura yake ili badilika, mavazi yake yakawa meupe, yakimetameta na kung’aa. 30 Ghafla wakawepo watu wawili wakaanza kuzungumza naye. Walikuwa ni Musa na Eliya! 31 Nao walionekana katika utukufu wakizungumza na Yesu kuhusu kifo chake ambacho kingetokea Yerusalemu.

32 Petro na wenzake ambao walikuwa wamelala usingizi mzito waliamka wakaona utukufu wa Yesu na wale watu wawili waliokuwa wamesimama pamoja naye. 33 Musa na Eliya walipoanza kuondoka, Petro akamwambia Yesu, “Bwana ni vizuri mno kwamba tuko hapa! Tutajenga vibanda vitatu - kimoja chako, kingine cha Musa na kin gine cha Eliya.” Lakini Petro hakujua anasema nini. 34 Petro alipokuwa bado anazungumza, pakatokea wingu kubwa na kivuli chake kikawafunika, na wale wanafunzi wakashikwa na hofu lile wingu lilipowafikia. 35 Sauti ikatoka kwenye wingu ikisema, “Huyu ni Mwanangu niliyemchagua, msikilizeni yeye.” 36 Baada ya sauti hiyo kusema, alionekana Yesu peke yake. Wale wanafunzi wakakaa kimya na kwa wakati huo hawakumwambia mtu ye yote yale waliyoy aona.

37 Kesho yake aliposhuka kutoka mlimani alikutana na umati mkubwa wa watu. 38 Ghafla, mtu mmoja kati yao akapiga kelele akasema, “Mwalimu, tafadhali nakuomba umwangalie mtoto wangu, ni mwanangu wa pekee. 39 Mara kwa mara pepo humshika na kumfanya apige kelele kisha humwangusha na kumtia kifafa akatokwa na povu mdomoni. Anamtesa sana na hamwachii ila kwa shida. 40 Nimewaomba wanafunzi wako wamwondoe huyo pepo lakini wameshindwa.” 41 Yesu akajibu, “Enyi watu mliopotoka, msio na imani, nitakaa nanyi na kuwavumilia mpaka lini? Mlete mwanao hapa.”

42 Yule mtoto alipokuwa akija, yule pepo akamwangusha, akam tia kifafa. Lakini Yesu akamwamuru yule pepo amtoke. Akamponya yule mtoto akamkabidhi kwa baba yake. 43 Watu wote walishangaa walipoona huo uweza mkuu wa Mungu. Wakati watu walipokuwa wanas taajabia hayo yote aliyokuwa akiyafanya Yesu, yeye aliwaambia wanafunzi wake: 44 “ Sikilizeni kwa makini haya nitakayowaambia sasa: mimi Mwana wa Adamu nitasalitiwa na kuwekwa mikononi mwa wanadamu.” 45 Lakini wanafunzi wake hawakuyaelewa maneno hayo. Maana ya maneno hayo ilikuwa imefichwa ili wasiweze kuelewa, nao waliogopa kumwuliza.

Yesu Afundisha Kuhusu Ukubwa

46 Wanafunzi wakaanza kubishana wao kwa wao kuhusu nani kati yao alikuwa mkuu zaidi. 47 Lakini Yesu aliyatambua mawazo yao, akamsimamisha mtoto mdogo karibu naye 48 kisha akawaambia, “Ye yote atakayemkaribisha mtoto huyu mdogo kwa jina langu atakuwa amenikaribisha; na ye yote atakayenikaribisha mimi atakuwa amem karibisha yeye aliyenituma; kwa maana yeye aliye mdogo kati yenu, ndiye aliye mkubwa kuliko wote.” 49 Yohana akasema, “Bwana, tumemwona mtu akifukuza pepo kwa jina lako tukamzuia kwa maana yeye si mmoja wetu.” 50 Yesu akasema, “Msimzuie kwa sababu ye yote ambaye hapingani nanyi, yuko upande wenu.”

Yesu Akataliwa Samaria

51 Siku zake za kurudi mbinguni zilipokaribia, Yesu aliamua kwamba lazima aende Yerusalemu na akaanza safari kuelekea huko. 52 Akatuma watu wamtangulie, nao wakaenda katika kijiji kimoja cha Samaria kumwandalia kila kitu. 53 Lakini watu wa kijiji hicho walikataa kumpokea kwa sababu ilikuwa dhahiri kwamba ali kuwa anakwenda Yerusalemu. 54 Basi wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, wakasema: “Bwana, unataka tuamuru moto kutoka mbinguni uwaangamize?” 55 Yesu akageuka, akawakemea. 56 Wakaenda kijiji kingine.

Gharama Ya Kumfuata Yesu

57 Walipokuwa wakienda, mtu mmoja akamwambia Yesu, “Nitakufu ata po pote utakapokwenda.” 58 Yesu akamwambia, “Mbweha wanaishi kwenye mapango yao na ndege kwenye viota vyao lakini mimi Mwana wa Adamu sina mahali pa kulala na kupumzika.”

59 Yesu alimwambia mtu mwingine, “Nifuate.” Mtu huyo akamjibu, “Bwana, niache kwanza nikamzike baba yangu.” 60 Yesu akamwam bia, “Waache wafu wawazike wafu wao. Bali wewe nenda ukautan gaze Ufalme wa Mungu.” 61 Mtu mwingine akamwambia, “Bwana nitakufuata lakini naomba kwanza nikaage jamaa yangu.” 62 Yesu akamwambia, “Mtu ye yote ashikaye jembe kuanza kulima kisha akawa anageuka kutazama nyuma, hafai kwa Ufalme wa Mungu.” Yesu Awatuma Wafuasi Sabini na Wawili

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica