Previous Prev Day Next DayNext

Bible in 90 Days

An intensive Bible reading plan that walks through the entire Bible in 90 days.
Duration: 88 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Yakobo 3:13 - 3 Yohana 14

Aina Mbili Za Hekima

13 Ni nani miongoni mwenu aliye na hekima na ufahamu? Basi aonyeshe hayo kwa maisha yake mazuri na kwa matendo yake anayot enda kwa unyenyekevu utokanao na hekima. 14 Lakini ikiwa mna wivu wenye chuki na kufikiria mno maslahi yenu binafsi, msiji sifie hayo wala kuikataa kweli. 15 Hekima ya namna hiyo haishuki kutoka mbinguni bali ni ya kidunia; si hekima ya kiroho bali ni ya shetani. 16 Kwa maana penye wivu na ubinafsi, ndipo penye machafuko na kila tendo ovu.

17 Lakini hekima itokayo mbinguni kwanza ni safi, kisha ni yenye kupenda amani, yenye kufikiria wengine, yenye unyenyekevu, iliyojaa huruma na matunda mema, isiyopendelea mtu, na ya kweli. 18 Wapenda-amani wapandao katika amani huvuna mavuno ya haki.

Jinyenyekezeni Kwa Mungu

Ni kitu gani kinachosababisha vita na ugomvi miongoni mwenu? Je, si tamaa zenu zinazopingana ndani yenu? Mnatamani lakini hampati kwa hiyo mnaua . Na mnatamani kupata lakini ham pati vile mnavyotaka kwa hiyo mnapigana na kuanzisha vita. Mme pungukiwa kwa sababu hamumwombi Mungu. Mnaomba lakini hampokei kwa sababu mnaomba kwa nia mbaya, ili mtumie mtakavyopata kwa kutosheleza tamaa zenu.

Ninyi viumbe wasio waaminifu! Hamfahamu kwamba urafiki na dunia ni uadui na Mungu? Kwa hiyo anayependa kuwa rafiki wa dunia anajitangaza kuwa adui wa Mungu. Au mnadhani Maandiko mataka tifu yanasema bure kuwa, “Anaona wivu juu ya roho aliyemweka aishi ndani yetu”? Lakini yeye anatupatia neema zaidi, ndio maana Maandiko husema, “Mungu huwapinga wenye kiburi lakini huwapa neema wanyenyekevu.”

Kwa hiyo, jinyenyekezeni kwa Mungu . Mpingeni shetani, naye atawakimbia. Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia. Takaseni mikono yenu, ninyi wenye dhambi; na takaseni mioyo yenu, ninyi wenye nia mbili. Huzunikeni, ombolezeni na kulia. Kicheko chenu kiwe kilio na furaha yenu iwe huzuni. 10 Jinyenyekezeni mbele za

Kuhusu Kuhukumiana

11 Ndugu, msilaumiane ninyi kwa ninyi. Mtu anayesema maovu kumhusu ndugu yake au kumhukumu ndugu yake anailaumu sheria na kuihukumu. Unapoihukumu sheria, basi hutii sheria bali umekuwa hakimu wa sheria. 12 Ni Mungu peke yake ambaye ametoa sheria na pia yeye ndiye hakimu; ni yeye tu awezaye kuokoa na kuangamiza.

Usijivunie ya Kesho

13 Sasa nisikilizeni ninyi msemao, “Leo au kesho tutakwenda katika mji huu ama ule tukae mwaka mmoja huko, tufanye biashara na kuchuma fedha.” 14 Kumbe hamjui litakalotokea kesho! Kwani maisha yenu ni kitu gani? Ninyi ni kama ukungu ambao huonekana kwa muda mfupi tu na baadaye hutoweka. 15 Badala yake mnapaswa kusema, “Bwana akipenda, tutaishi na kufanya hili ama lile.” 16 Lakini sasa mnajisifu kwa sababu ya ujinga wenu. Kujisifu kwa jinsi hiyo ni uovu.

17 Mtu ye yote anayefahamu lililo jema kutenda, lakini asilitende, basi mtu huyo anatenda dhambi.

Onyo Kwa Matajiri

Sasa sikilizeni, ninyi matajiri: Lieni na kuomboleza kwa ajili ya huzuni inayowajia. Utajiri wenu umeoza na mavazi yenu yameliwa na nondo. Dhahabu yenu na fedha yenu vimeingia kutu na kutu yake itakuwa ushahidi dhidi yenu na itakula miili yenu kama moto. Mmejilimbikizia utajiri kwa siku za mwisho. Angalieni ule ujira mliowadhulumu vibarua waliovuna mashamba yenu unawalilia; na vilio vya wavunaji hao vimeyafikia masikio ya Bwana wa majeshi. Mmeishi duniani maisha ya anasa na kujistarehesha. Mmejinenepesha tayari kwa siku ya kuchinjwa. Mmemhukumu na kum wua mwenye haki; yeye hakuwapinga.

Subira Na Mateso

Kwa hiyo, ndugu zangu, muwe na subira mpaka Bwana atakapo kuja. Angalieni jinsi mkulima anavyongojea ardhi itoe mavuno mazuri, jinsi anavyongojea kwa subira mvua za mwanzo na za mwisho. Hali kadhalika nanyi muwe na subira. Muwe na mioyo tha biti kwa sababu kuja kwa Bwana kumekaribia. Ndugu zangu, msi nung’unikiane wenyewe kwa wenyewe, ama sivyo mtahukumiwa. Hakimu amesimama mlangoni.

10 Ndugu zangu, kama mfano wa subira wakati wa mateso, waan galieni manabii walionena katika jina la Bwana. 11 Kama mnavy ojua tunawahesabu kuwa wamebarikiwa wale ambao wamevumilia. Mmek wisha kusikia habari za ustahimilivu wa Ayubu na mmeona shabaha ya Bwana, jinsi Bwana alivyo na huruma na rehema.

12 Zaidi ya yote, ndugu zangu, msiape, ama kwa mbingu, au kwa dunia au kwa kiapo kingine cho chote. Bali mkisema ‘Ndio’ iwe ndio, na mkisema ‘Hapana

Maombi Ya Imani

13 Je, kuna mtu ye yote miongoni mwenu aliye na shida? Basi na aombe. Je, yuko mwenye furaha? Basi na aimbe nyimbo za sifa. 14 Je, kuna mtu miongoni mwenu aliye mgonjwa? Basi awaite wazee wa kanisa wamwombee na kumpaka mafuta katika jina la Bwana. 15 Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa huyo na Bwana atamwinua. Kama ametenda dhambi, atasamehewa. 16 Kwa hiyo ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi na kuombeana ili mpate kuponywa. Maombi ya mtu mwenye haki yana nguvu na huleta matokeo.

17 Eliya alikuwa binadamu kama sisi. Aliomba kwa moyo kwamba mvua isinyeshe na mvua haikunyesha juu ya nchi kwa muda wa miaka mitatu na nusu. 18 Kisha akaomba tena na mbingu zikatoa mvua na ardhi ikazaa matunda yake.

19 Ndugu zangu, ikiwa mtu miongoni mwenu anapotoka kutoka katika kweli na mtu mwingine akamrejesha,

Kutoka kwa Petro, mtume wa Yesu Kristo. Kwa wateule wa Mungu ambao wametawanyika, wanaoishi ugenini huko Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithinia. Ninyi mlichaguliwa tangu mwanzo na Mungu Baba na kutakaswa na Roho, mpate kumtii Yesu Kristo na kunyunyiziwa damu yake. Nawatakieni neema na amani tele.

Tumaini Lenye Uzima

Asifiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa rehema yake kuu ametufanya tuzaliwe upya ili tupate tumaini lenye uzima kwa kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo kutoka kwa wafu; na tupokee urithi usioharibika, usiooza na usiochuja, ambao umewekwa mbinguni kwa ajili yenu. Nanyi, kwa imani, mnalindwa na nguvu ya Mungu mpaka utakapofika wokovu ambao uko tayari kufunuliwa wakati wa mwisho.

Furahini sana katika hilo, ingawa sasa kwa kitambo kidogo ni lazima mpate majaribu ya kila aina. Majaribu yataifanya imani yenu, ambayo ina thamani kuliko dhahabu, iwe imepimwa na kuthibitishwa kuwa ya kweli kama vile dhahabu ambayo ingawa ni kitu kiharibikacho, hupimwa kwa moto. Ndipo mtapata sifa, utukufu na heshima siku ile Yesu Kristo atakapofunuliwa. Ingawa hamja pata kumwona, mnampenda. Na ingawa hamumwoni sasa mnamwamini na kujawa na furaha tukufu isiyoelezeka. Maana mnapokea wokovu wa roho zenu, ambao ndio lengo la imani yenu.

10 Manabii waliotabiri kuhusu neema hiyo ambayo ninyi mnge pewa, walitafuta sana na kwa makini habari za wokovu huu. 11 Walijaribu kutafuta kujua ni nani au ni wakati upi uliomaan ishwa na Roho wa Kristo aliyekuwa akisema ndani yao alipotabiri kuhusu mateso ya Kristo na utukufu utakaofuata. 12 Walidhihir ishiwa kuwa kazi waliyokuwa wakifanya si kwa faida yao bali ni kwa ajili yenu. Kwa maana walinena nanyi habari za mambo ambayo sasa mmekwisha elezwa na wale waliowahubiria Injili kwa uwezo wa Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni. Hata malaika wanata mani kufahamu mambo haya.

Mwito Wa Kuishi Maisha Matakatifu

13 Kwa hiyo, ziandaeni nia zenu, muwe na kiasi, wekeni tumaini lenu lote katika neema ile mtakayopewa wakati ule Yesu Kristo atakapodhihirishwa. 14 Kama watoto watiifu, msikubali kutawaliwa na tamaa mbaya mlizokuwa nazo wakati mkiishi katika ujinga. 15 Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, kadhalika ninyi muwe watakatifu katika mwenendo wenu; 16 maana imeandikwa: “Muwe watakatifu kwa sababu mimi ni mtakatifu.”

17 Kwa kuwa mnamwita “Baba” yeye ahukumuye matendo ya kila mtu pasipo upendeleo, ishini maisha yenu hapa duniani kama wageni, kwa kumcha Mungu. 18 Maana mnafahamu kwamba mlikombolewa kutokana na maisha duni yasiyofaa ambayo mlirithi kutoka kwa baba zenu. Hamkukombolewa kwa kutumia vitu viharibikavyo kama fedha na dhahabu, 19 bali mlikombolewa kwa damu ya thamani ya Kristo, Mwana-Kondoo asiye na dosari wala doa. 20 Yeye alichaguliwa kabla ya dunia kuumbwa lakini akadhihirishwa katika siku hizi za mwisho kwa ajili yenu. 21 Kwa ajili yake ninyi mnamwamini Mungu aliyemfufua kutoka kwa wafu akampa utukufu, na kwa hiyo imani yenu na matumaini yenu yako kwa Mungu.

22 Na sasa kwa kuwa mmekwisha kujitakasa kwa kuitii ile kweli na kuwapenda ndugu zenu kwa kweli, pendaneni kwa moyo wote. 23 Maana mmezaliwa upya, si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa mbegu isiyoharibika, kwa neno la Mungu lililo hai na linalodumu hata milele. 24 Maana, “Binadamu wote ni kama nyasi na utukufu wao ni kama ua la mwituni. Nyasi hunyauka na ua huanguka, 25 lakini neno la Mungu hudumu milele.” Na neno hilo ni Habari Njema ambayo mlihubiriwa. Basi, acheni kabisa uovu wote, hila yote, unafiki, wivu na masingizio yote. Kama watoto wachanga, mtamani maziwa safi ya kiroho, ili kwa hayo mpate kukua katika wokovu wenu, kwa maana mmekwisha kuonja fadhili za Bwana.

Jiwe Hai Na Taifa Takatifu

Basi, njooni kwake yeye aliye Jiwe lililo hai, ambalo lili kataliwa na watu bali kwa Mungu ni teule na la thamani kubwa. Ninyi pia, kama mawe hai mjengwe kuwa nyumba ya kiroho, mpate kuwa makuhani watakatifu, mkitoa sadaka za kiroho zinazokubaliwa na Mungu kwa njia ya Yesu Kristo. Kwa maana imeandikwa katika Maandiko: “Tazama, ninaweka jiwe kuu la msingi huko Sayuni; jiwe la pembeni teule na la thamani kubwa, na kila amwaminiye hataaibika.” Kwenu ninyi mnaoamini, yeye ni wa thamani kubwa. Lakini kwao wasioamini, “Lile jiwe walilokataa waashi limekuwa jiwe kuu la msingi,” na, “Jiwe ambalo litawafanya watu wajik wae; mwamba ambao utawafanya waanguke.” Wanajikwaa kwa sababu hawatii lile neno, kama walivyopangiwa tangu mwanzo.

Lakini ninyi ni uzao mteule, ukuhani mtukufu, taifa taka tifu, watu pekee wa Mungu mlioteuliwa kutangaza matendo makuu ya aliyewaita kutoka gizani na kuwaingiza katika nuru yake ya ajabu. 10 Hapo mwanzo ninyi mlikuwa si taifa, lakini sasa ninyi ni watu wa Mungu. Hapo mwanzo mlikuwa hamjapata rehema, lakini sasa mme pata rehema.

11 Rafiki wapendwa, ninawasihi, mkiwa kama wageni na wapi taji njia hapa duniani, epukeni tamaa mbaya za mwili ambazo hupi gana vita na roho zenu. 12 Muwe na mwenendo mwema kati ya watu wasiomjua Mungu, ili kama watawasema kuwa wakosaji, wayaone matendo yenu mema na wamtukuze Mungu siku ile atakapotujia.

Kuwatii Wenye Mamlaka

13 Jinyenyekezeni kwa ajili ya Bwana chini ya mamlaka yote ya wanadamu: ikiwa ni mfalme ambaye ana mamlaka ya mwisho; 14 au ikiwa ni wakuu wengine ambao amewateua kuwaadhibu wahalifu na kuwasifu watendao mema. 15 Kwa maana ni mapenzi ya Mungu kwamba kwa kutenda mema myazime maneno ya kijinga ya watu wapumbavu. 16 Ishini kama watu huru lakini msitumie uhuru wenu kama kisin gizio cha kutenda uovu; bali muishi kama watumishi wa Mungu. 17 Waheshimuni watu wote. Wapendeni ndugu waamini. Mcheni Mungu. Mheshimuni mfalme. 18 Ninyi watumwa, watiini mabwana wenu kwa heshima yote, si wale mabwana walio wapole na wema peke yao, bali hata wale walio wakali. 19 Maana ni jambo jema kwa mtu kuvumilia taabu za maonevu kwa kukumbuka kuwa Mungu yupo. 20 Maana ni sifa gani kwa mtu kustahimili kupigwa kwa kuwa ametenda uovu? Lakini kama mkis tahimili mateso kwa kutenda wema, mnapata kibali mbele za Mungu. 21 Ninyi mmeitwa kwa ajili hiyo, kwa sababu Kristo naye aliteseka kwa ajili yenu akawaachia kielelezo, mzifuate nyayo zake. 22 Yeye hakutenda dhambi wala neno la udanganyifu haliku pita kinywani mwake. 23 Walipomtukana, yeye hakuwarudishia matu kano; alipoteswa, hakuwatishia, bali alimtegemea Mungu ahukumuye kwa haki. 24 Yeye mwenyewe alizibeba juu mtini dhambi zetu mwil ini mwake, ili tuwe wafu kwa mambo ya dhambi na tupate kuishi katika haki. Kwa majeraha yake, ninyi mmeponywa.

25 Kwa maana mlikuwa mmepotea kama kondoo, lakini sasa mmer udi kwa Mchungaji na Mlinzi wa roho zenu.

Mafundisho Kwa Wake Na Waume

Kadhalika ninyi wake, jinyenyekezeni chini ya waume zenu, ili kama wako wasioliamini neno, wapate kuamini kwa kuvutiwa na mwenendo wa wake zao. Hawatahitaji kuambiwa neno kwa sababu wataona maisha yenu safi na ya kumcha Mungu.

Kujipamba kwenu kusiwe kwa nje, yaani: kwa kusuka nywele, kujipamba kwa dhahabu na kuvaa mavazi maridadi. Bali kujipamba kwenu kuwe katika utu wa ndani wa moyoni, kwa uzuri usioharibika, wa roho ya upole na utulivu. Uzuri wa namna hii ni wa thamani sana mbele za Mungu. Maana ndivyo walivyojipamba wanawake wata katifu wa zamani, waliomtumaini Mungu na kuwa wanyenyekevu kwa waume zao. Kama Sara alivyomtii mumewe Ibrahimu, akamwita ‘bwana’. Ninyi sasa ni binti zake Sara kama mkitenda mema pasipo kuogopa tishio lo lote.

Kadhalika ninyi waume, ishini na wake zenu kwa kuwahurumia, mkitambua ya kuwa wao ni dhaifu na hivyo muwape heshima, kwa maana ninyi ni warithi pamoja nao wa neema ya uzima. Fanyeni hivyo ili sala zenu zisizuiliwe.

Msilipe Ovu Kwa Ovu

Hatimaye, ninyi nyote muwe na nia moja, mhurumiane, mpen dane kama ndugu, muwe na mioyo ya upole na ya unyenyekevu. Msi lipe ovu kwa ovu, au tusi kwa tusi; ila barikini kwa maana hili ndilo mliloitiwa na Mungu, mpate kurithi baraka. 10 Kwa maana, “Mtu anayependa kufurahia maisha, na anayetamani kuona siku njema, basi auzuie ulimi wake usinene mabaya na midomo yake isi seme uongo. 11 Mtu huyo aepuke maovu, na atende mema; atafute amani na kuifuatilia sana. 12 Kwa maana macho ya Bwana huwaele kea wenye haki, na masikio yake husikiliza sala zao. Bali Bwana huwapa kisogo watenda maovu.”

Kuvumilia Mateso

13 Basi, ni nani atakayewadhuru ikiwa mna juhudi katika kutenda mema? 14 Lakini hata kama mtateseka kwa ajili ya haki, mtabarikiwa. Msiogope vitisho vyao wala msiwe na wasiwasi, 15 bali mioyoni mwenu mtukuzeni Kristo Bwana. Kila wakati muwe tayari kumjibu mtu ye yote atakayewauliza kuhusu tumaini lililomo ndani yenu. Lakini fanyeni hivyo kwa upole na kwa unyenyekevu.

16 Dhamiri zenu ziwe safi ili mnapotukanwa, hao wanaotukana mwenendo wenu mwema katika Kristo, waone haya. 17 Maana ni afad hali kupata mateso kwa kutenda mema kama hayo ndio mapenzi ya Mungu, kuliko kuteseka kwa kutenda maovu. 18 Maana Kristo pia alikufa mara moja tu kwa wakati wote; mwenye haki kwa ajili ya wasio na haki, ili atulete kwa Mungu. Mwili wake uliuawa lakini akafanywa hai katika roho yake. 19 Naye akiwa katika roho alik wenda kuhubiria roho zilizofungwa kifungoni. 20 Roho hizo zamani hazikutii, siku zile Mungu aliposubiri, wakati Noe alipojenga safina, watu wachache, yaani watu wanane, wakaokolewa katika ile gharika ya maji. 21 Maji hayo ni kielelezo cha ubatizo ambao sasa unawaokoa ninyi, si kwa kuondoa uchafu kwenye miili yenu, bali kama dhamana ya kuwa na dhamiri njema kwa Mungu kwa ajili ya kufufuka kwa Yesu Kristo. 22 Yeye amekwenda mbinguni, na amekaa upande wa kulia wa Mungu pamoja na malaika, mamlaka na nguvu zote zikiwa chini yake.

Maisha Mapya

Basi kwa kuwa Kristo aliteseka katika mwili, ninyi pia jiimarisheni kwa nia hiyo hiyo kwa maana mtu aliyekwisha kuteseka katika mwili hana uhusiano tena na dhambi. Matokeo yake ni kwamba, kwa muda wa maisha yake yaliyobakia hapa duniani, haishi tena kwa kufuata tamaa mbaya za mwili bali anaishi kwa kufuata mapenzi ya Mungu. Maana mmekwisha kutumia muda wa kutosha katika maisha yenu yaliyopita mkifanya yale ambayo watu wasiomjua Mungu hupenda kutenda: uasherati, tamaa mbaya, ulevi, karamu za ulevi na ibada ovu za sanamu. Wanaona ajabu kwamba sasa hamshi riki tena pamoja nao katika ufisadi wao wa kinyama, nao huwatu kana. Lakini itawabidi kujieleza mbele zake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa. Kwa maana hii ndio sababu Injili ilihubiriwa hata kwa hao waliokufa: wahukumiwe kama wana damu wengine kuhusu maisha yao katika mwili, bali wapate kuishi katika roho kama Mungu aishivyo.

Kuja Kwa Kristo Kumekaribia

Mwisho wa mambo yote umekaribia. Kwa hiyo muwe na akili timamu na wenye kiasi ili mweze kuomba. Zaidi ya yote, pen daneni kwa moyo wote, maana upendo hufunika dhambi nyingi sana. Karibishaneni pasipo manung’uniko. 10 Kila mmoja na atumie kipawa alichopewa kuwahudumia wengine, kama mawakili waaminifu wa neema mbalimbali za Mungu. 11 Mtu akisema kitu, basi na awe kama anayesema maneno halisi ya Mungu. Mtu anayetoa huduma na ahudumu kwa nguvu apewayo na Mungu; ili katika mambo yote, Mungu atukuzwe kwa njia ya Yesu Kristo. Yeye ni mwenye utukufu na uweza, milele na milele. Amina.

Kuteseka Kwa Mkristo

12 Wapendwa, msishangae kwa ajili ya mateso makali yanayowa pata kana kwamba ni kitu kigeni kinawatokea. 13 Bali furahini kwamba mnashiriki katika mateso ya Kristo, ili mpate kufurahi na kushangilia wakati utukufu wake utakapofunuliwa. 14 Kama mkilau miwa kwa ajili ya jina la Kristo, mmebarikiwa, kwa sababu Roho wa Utukufu, yaani Roho wa Mungu, anakaa juu yenu. 15 Lakini asiwepo mtu ye yote kati yenu ambaye atateswa kwa kuwa ni mwuaji, au mwizi, au mhalifu au anayejiingiza katika mambo ya watu wengine. 16 Lakini kama mtu akiteseka kwa kuwa ni mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu kwa jina hilo. 17 Kwa maana wakati umefika wa hukumu kuanza katika nyumba ya watu wa Mungu; na kama itaanza na sisi, mwisho wa hao ambao hawatii Injili ya Mungu utakuwaje? 18 Na, “Kama ni vigumu kwa mtu wa haki kuokolewa, itakuwaje kwa mtu asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?” 19 Basi wale wanaoteswa kufuatana na mapenzi ya Mungu, wajikabidhi kwa Muumba wao aliye mwaminifu.

Maagizo Kwa Wazee Na Vijana

Ninawasihi wazee waliomo miongoni mwenu, nikiwa mzee mwenzenu na shahidi wa mateso ya Kristo na mshiriki katika utu kufu utakaofunuliwa. Lichungeni kundi la Mungu mlilokabidhiwa, si kwa kulazimishwa bali kwa hiari, si kwa tamaa ya fedha bali kwa moyo wenu wote. Msijifanye mabwana wakubwa kwa wale mnaowa chunga bali muwe vielelezo kwa kundi hilo. Naye Mchungaji mkuu atakapodhihirishwa mtapokea taji ya utukufu isiyofifia.

Kadhalika ninyi vijana watiini wazee. Jivikeni unyenyekevu, mnyenyekeane kwa maana, “Mungu huwapinga wenye kiburi bali huwapa neema wanyenyekevu.” Basi, nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu wenye nguvu, ili wakati wake ufaao utakapotimia, awainue.

Mwekeeni yeye fadhaa zenu zote kwa maana yeye hujishughul isha sana na mambo yenu.

Kaeni macho. Kesheni, maana adui yenu Ibilisi, huzunguka- zunguka akinguruma kama simba, akitafuta mtu atakayemmeza. Mpingeni, mkiwa thabiti katika imani, mkifahamu kwamba ndugu zenu pote duniani wanapatwa na mateso hayo hayo. 10 Na mkisha kuteseka kitambo kidogo, Mungu wa neema yote ambaye amewaita katika utukufu wake wa milele katika Kristo, yeye mwenyewe atawa kamilisheni na kuwathibitisha na kuwatia nguvu. 11 Uweza ni wake milele na milele. Amina.

Salamu

12 Nimewaandikia kwa kifupi kwa msaada wa Silvano, ndugu ambaye namtambua kuwa mwaminifu, nikiwaonya na kuwashuhudia kuwa hii ndio neema ya kweli ya Mungu. Simameni imara katika neema hiyo. 13 Mwenzenu mteule hapa Babiloni anawasalimu pamoja na mwanangu Marko .

Kutoka kwa Simoni Petro mtumishi na mtume wa Yesu Kristo. Kwa wote ambao wamepokea imani yenye thamani kama yetu kutokana na haki ya Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo.

Nawatakieni neema na amani tele katika kumjua Mungu na Yesu

Wito Wa Kuishi Maisha Ya Kikristo

Uweza wake wa kimungu umetupatia mambo yote yanayohusiana na uzima na utauwa kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake. Kwa njia hiyo ametupatia ahadi zake kuu na za tha mani. Mkishika ahadi hizo mtashiriki asili yake ya kimungu na kuepuka uovu ambao uko duniani kwa sababu ya tamaa mbaya.

Kwa sababu hii, jitahidini sana kuongeza wema katika imani yenu; na katika wema ongezeni maarifa; na katika maarifa ongezeni kiasi; na katika kiasi ongezeni ustahimilivu; na katika ustahimilivu ongezeni kumcha Mungu; na katika kumcha Mungu ongezeni upendano wa kindugu; na katika upendano wa kindugu ongezeni upendo. Maana mkiwa na sifa hizi kwa wingi zitawawe zesha kuwa wenye bidii na wenye kuzaa matunda katika kumfahamu Bwana wetu Yesu Kristo. Lakini mtu asiyekuwa na sifa hizi ni kipofu, haoni mbali, na amesahau kuwa ametakaswa dhambi zake za zamani.

10 Kwa hiyo, ndugu zangu, fanyeni bidii zaidi kuuhakikisha wito wenu na uteule wenu, kwa maana mkifanya hivyo, hamtaanguka kamwe; 11 na mtakaribishwa kwa fahari kubwa katika ufalme wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.

Unabii Wa Maandiko

12 Kwa hiyo ninakusudia kuwakumbusha hayo siku zote, ingawa mnayafahamu na mmekuwa imara katika kweli mliyo nayo. 13 Nadhani ni vema niwahimize kwa kuwakumbusha mambo haya, wakati wote nina poishi katika mwili huu. 14 Kwa maana najua kwamba karibu nitauweka kando mwili wangu, kama Bwana wetu Yesu Kristo alivyon ionyesha wazi. 15 Na nitahakikisha kwamba baada ya kuondoka kwangu mtaendelea kukumbuka mambo haya kila wakati.

16 Tulipowafundisha juu ya uweza na kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo, hatukufuata hadithi zilizotungwa kwa werevu, bali tulish uhudia kwa macho yetu utukufu wake. 17 Maana alipopewa heshima na utukufu kutoka kwa Mungu Baba, na sauti ikamjia katika utukufu mkuu ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa naye’ 18 tuliisikia sauti hii iliyotoka mbinguni, maana tulikuwa naye kwenye ule mlima mtakatifu.

19 Kwa hiyo tuna uhakika zaidi juu ya ujumbe wa manabii. Hivyo itakuwa vema mkizingatia ujumbe huo, kama vile watu wanavy oitegemea taa ing’aayo mahali penye giza, mpaka Siku ile itakapo fika na nyota ya asubuhi itakapoangaza mioyoni mwenu. 20 Kwanza kabisa ni lazima muelewe kwamba hakuna unabii katika Maandiko uliotokana na tafsiri ya nabii mwenyewe. 21 Kwa sababu hakuna unabii uliokuja kwa matakwa ya binadamu, bali watu walinena ujumbe kutoka kwa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu.

Walimu Wa Uongo

Lakini pia walikuwepo manabii wa uongo miongoni mwa watu, kama watakavyotokea walimu wa uongo kati yenu. Kwa siri, watain giza mafundisho ya upotovu hata kumkana Bwana aliyewakomboa, na kwa njia hiyo watajiletea maangamizi ya haraka. Na wengi wata fuata tamaa zao potovu, na kwa ajili ya matendo yao njia ya kweli itadharauliwa. Nao katika tamaa yao watajaribu kuwanunua kwa kuwaambia hadithi walizotunga wenyewe. Lakini hukumu yao imekuwa tayari tangu zamani, wala mwangamizi wao hajalala usingizi.

Maana kama Mungu hakuwahurumia malaika walipotenda dhambi bali aliwatupa kuzimu, katika vifungo vya giza wakae huko mpaka siku ya hukumu; kama hakuuhurumia ulimwengu wa kale alipoleta gharika juu ya ulimwengu wa watu wasiomcha Mungu, akamlinda Noe mjumbe wa haki, pamoja na watu saba wengine; kama aliihukumu miji ya Sodoma na Gomora kwa kuiteketeza ikawa majivu, akaifanya kuwa mfano kwa wote ambao hawatamcha Mungu; na kama alimwokoa Loti, mtu mwenye haki ambaye alihuzunishwa na maisha ya uchafu ya watu wahalifu - kwa sababu yale maasi aliyoona na kusikia huyo mtu wa Mungu alipoishi kati yao yalimhuzunisha usiku na mchana - basi ikiwa ni hivyo, Bwana anajua jinsi ya kuwaokoa watu wa Mungu kutoka katika majaribu na kuwaweka waasi katika hali ya adhabu mpaka siku ya hukumu. 10 Hii ni hakika hasa kwa wale wanaofuata tamaa chafu za mwili na kudharau mamlaka. Watu hawa ni shupavu na katika kiburi chao, hawaogopi kuwatu kana viumbe vitukufu wa mbinguni;

11 ingawa hata malaika, ambao wana nguvu na uwezo zaidi, hawawashtaki au kuwatukana viumbe hao mbele za Bwana. 12 Lakini watu hawa hukufuru katika mambo wasiy oyafahamu. Wao ni kama wanyama wasio na akili, viumbe wanaotawal iwa na hisia za mwili, ambao wamezaliwa ili wakamatwe na kuchinjwa, na kama wanyama, wao pia wataangamizwa.

13 Watalipizwa madhara kwa ajili ya madhara waliyowatendea wengine. Furaha yao ni kufanya karamu za ufisadi mchana, wazi wazi. Wao huleta aibu na fedheha wanaposhiriki katika karamu zenu kwa kuwa wakati wote huo, wanajifurahisha katika upotevu wao. 14 Macho yao yamejaa uzinzi, nao hutenda dhambi bila kikomo. Huwahadaa watu dhaifu. Mioyo yao imezoea kutamani. Hawa ni wana wa laana! 15 Wameiacha njia iliyonyooka, wakapotoka na kuifuata njia ya Balaamu mwana wa Beori aliyependa kupata fedha kwa kufa nya maovu. 16 Balaamu alikaripiwa kwa ajili ya uovu wake. Punda ambaye hasemi alinena kwa sauti ya binadamu akamzuia huyo nabii asiendelee na kichaa chake.

17 Watu hawa ni kama chemchemi zilizokauka na ukungu upeper ushwao na tufani, na lile giza jeusi limewekwa tayari kwa ajili yao. 18 Wao hutamka maneno matupu ya majivuno na kutumia tamaa mbaya za mwili kuwanasa tena wale ambao ndio kwanza wameepukana na watu wanaoishi maisha ya uovu. 19 Huwaahidi hao waliowanasa kuwa watakuwa huru kabisa, lakini wao wenyewe ni watumwa wa upo tovu. Kwa maana mtu huwa mtumwa wa kitu kile kinachomshinda nguvu. 20 Kwa maana wale waliokwisha kuponyoka kutoka katika uchafu wa dunia hii kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo , kisha wakanaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho ni mbaya zaidi kuliko ile ya kwanza. 21 Ingekuwa heri kwao kama hawa kuijua kamwe njia ya haki, kuliko kuifahamu kisha wakaiacha ile amri takatifu waliyopewa. 22 Kama methali moja isemavyo, “Mbwa huyarudia matapishi yake mwenyewe,” na nyingine, “Nguruwe huoshwa na kurudi kugaa-gaa matopeni.”

Siku Ya Bwana

Rafiki wapendwa, hii ni barua ya pili ninayowaandikia. Katika barua zote mbili nimejaribu kuziamsha nia zenu safi kwa kuwakumbusha mambo haya. Napenda mkumbuke maneno yaliyosemwa zamani na manabii watakatifu na ile amri ya Bwana na Mwokozi mli yopewa na mitume wenu. Kwanza kabisa ni lazima muelewe hili: kwamba siku za mwisho watu wenye dhihaka watakuja kuwadhihaki wakiwa wametawaliwa na tamaa zao wenyewe. Watawaambia, “Ali yeahidi atakuja yuko wapi? Tangu baba zetu walipokufa mambo yam eendelea kuwa kama yalivyokuwa tangu kuumbwa kwa dunia.” Wao wameamua kusahau kwamba ni kwa neno la Mungu mbingu zilikuwepo tangu zamani, na kwamba ulimwengu uliumbwa kutokana na maji kwa njia ya maji, na kuwa kwa maji hayo hayo ulimwengu ule uliokuwepo uliangamizwa wakati ule wa gharika. Lakini kwa neno hilo hilo mbingu na dunia, ambazo zipo hivi sasa, zimewekwa akiba kuchomwa moto, zimewekwa mpaka siku ile ya hukumu na ya kuangami zwa kwa watu wasiomcha Mungu.

Lakini wapendwa msisahau neno hili, kwamba kwa Bwana, siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja. Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake kama watu wengine wanavyochukulia kukawia, bali yeye anawavumilia, maana hapendi mtu ye yote aan gamie, bali wote waifikie toba.

10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwizi. Ndipo mbingu zitatoweka kwa kishindo kikuu; na vitu vya asili vitateketezwa kwa moto na dunia na vitu vyote vilivyomo humo vitateketezwa.

11 Kwa kuwa kila kitu kitateketezwa hivyo, ninyi je, mna paswa kuwa watu wa namna gani? Mnapaswa kuishi maisha ya utaka tifu na utauwa, 12 mkingojea na mkiharakisha kuja kwa siku ya Mungu, siku ambayo mbingu zitateketezwa kwa moto na kutoweka, na vitu vyote vilivyomo ndani yake vitayeyushwa kwa moto! 13 Lakini kufuatana na ahadi yake, sisi tunangojea mbingu mpya na dunia mpya ambamo haki huishi.

14 Kwa hiyo wapendwa, kwa kuwa mnatazamia mambo haya, jita hidini ili mkutwe hamna doa wala lawama, mkiwa na amani naye. 15 Hesabuni uvumilivu wa Bwana kuwa ni wokovu, kama ndugu yetu mpendwa Paulo alivyokwisha kuwaandikieni kwa hekima aliyopewa na Mungu. 16 Ameandika hivyo hivyo katika barua zake zote akizun gumzia mambo haya. Barua zake zina mambo mengine ambayo ni magumu kuelewa, ambayo watu wajinga na wasio na msimamo huyapotosha, kama wanavyopotosha sehemu nyingine za Maandiko; na hivyo wana jiletea kuangamia.

17 Basi, ninyi wapendwa mkijua haya, jihadharini msije mka potoshwa na makosa ya hao waasi na kupoteza uthabiti wenu.

Neno La Uzima

Tunawaandikieni kuhusu kile ambacho kimekuwapo tangu mwanzo, ambacho tumekisikia na kukiona kwa macho yetu; ambacho tumekigusa kwa mikono yetu; yaani Neno la uzima. Uzima huo uli tokea, nasi tumeuona na tunaushuhudia, na tunawatangazieni uzima wa milele uliokuwa kwa Baba, nao ukadhihirishwa kwetu. Tunawa tangazia hicho tulichokiona na kukisikia ili nanyi pia mpate kushirikiana nasi. Na ushirika tulio nao ni wetu na Baba na Mwa nae Yesu Kristo. Tunawaandikieni mambo haya ili furaha yetu ikamilike.

Kutembea Nuruni

Huu ndio ujumbe tuliousikia kutoka kwake, ambao tunawatan gazia: Mungu ni nuru na ndani yake hamna giza kamwe. Tukisema tuna ushirika naye huku tunaendelea kuishi gizani tunasema uongo, wala hatutendi yaliyo ya kweli. Bali tukiishi nuruni, kama yeye alivyo nuru, tunakuwa na ushirika sisi kwa sisi na damu ya Mwanae Yesu, inatutakasa dhambi zote. Tukisema kwamba hatuna dhambi tunajidanganya wenyewe wala kweli haimo ndani yetu. Tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwa minifu na wa haki na atatusamehe dhambi zetu na kututakasa na uovu wote. 10 Tukisema hatujatenda dhambi tunamfanya yeye kuwa mwongo, na neno lake halimo ndani yetu.

Upendo Na Utii

Watoto wangu, ninawaandikieni mambo haya, kusudi msitende dhambi. Lakini kama mtu ye yote akitenda dhambi, tunaye mtetezi wetu kwa Baba, yaani Yesu Kristo mwenye haki. Kristo ndiye sadaka iliyotolewa kwa ajili ya dhambi zetu, na wala si dhambi zetu sisi tu, bali pia dhambi za ulimwengu wote.

Na tunaweza kuwa na hakika kwamba tunamjua Kristo ikiwa tunatii amri zake. Mtu ye yote akisema, “Ninamjua’ Lakini mtu ye yote anayetii neno lake, huyo ndiye ambaye upendo wa Mungu umekamilika ndani yake kwa kweli. Hivi ndivyo tunavy ojua kuwa tumo ndani ya Kristo. Mtu anayesema anadumu ndani ya Kristo anapaswa kuishi kama Yesu Kristo mwenyewe alivyoishi.

Wapendwa, siwaandikii amri mpya bali amri ile ambayo mme kuwa nayo tangu mwanzo. Amri hii ya zamani ni lile neno mlilok wisha kusikia. Lakini hata hivyo amri hii ninayowaandikieni ni mpya; ambayo ukweli wake unaonekana kwake na kwenu, kwa sababu giza linatoweka na nuru ya kweli imekwishaanza kuangaza. Mtu anayesema kwamba anaishi nuruni, naye anamchukia ndugu yake, bado yumo gizani. 10 Anayempenda ndugu yake anaishi katika nuru na wala hana kitu cha kumfanya ajikwae. 11 Lakini anayemchukia ndugu yake anaishi gizani na anatembea gizani, wala hajui aen dako, kwa sababu giza limempofusha macho.

Kwa Watoto, Baba Na Vijana

12 Ninawaandikieni ninyi watoto, kwa sababu mmesamehewa dhambi zenu, kwa ajili ya jina lake. 13 Ninawaandikieni ninyi akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliyekuwapo tangu mwanzo. Ninawaandikieni ninyi vijana, kwa sababu mmemshinda yule mwovu. Ninawandikieni ninyi watoto, kwa kuwa mmemjua Baba. 14 Ninawaan dikieni ninyi akina baba, kwa kuwa mmemjua yeye aliyekuwapo tangu mwanzo. Ninawaandikieni ninyi vijana kwa sababu mna nguvu na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.

Msipende Dunia

15 Msiipende dunia wala mambo yaliyomo duniani. Kama mtu akiipenda dunia, hawezi kumpenda Baba. 16 Maana vitu vyote vil ivyomo duniani, yaani, tamaa za mwili, tamaa ya vitu vinavyoone kana kwa macho, na kiburi kiletwacho na mali, vyote hivi havitoki kwa Baba bali hutoka ulimwenguni. 17 Nayo dunia inapita na tamaa zake zote zinapita, lakini mtu anayetimiza mapenzi ya Mungu huishi milele.

Onyo Kuhusu Adui Wa Kristo

18 Watoto wapendwa, huu ni wakati wa mwisho. Na kama mlivy okwisha kusikia kwamba yule mpinga-Kristo anakuja, hata sasa wapinga-Kristo wengi wamekwisha kuja. Kwa hiyo tunajua kuwa huu ni wakati wa mwisho. 19 Watu hao walitoka kati yetu, lakini hawakuwa wa kundi letu. Kama wangekuwa wa kundi letu, wangeende lea kuishi pamoja nasi; lakini waliondoka ili iwe wazi kuwa hakuna hata mmoja wao aliyekuwa wa kundi letu.

20 Lakini ninyi mmemiminiwa Roho Mtakatifu na nyote mnaijua kweli. 21 Siwaandikii hivi kwa kuwa hamuijui kweli bali kwa sababu mnaijua na kwa kuwa hakuna uongo utokao katika kweli. 22 Je, mwongo ni nani? Mwongo ni yule anayekana kwamba Yesu si Kristo. Mtu huyo ndiye mpinga-Kristo, anayemkana Baba na Mwana. 23 Mtu anayemkana Mwana hawezi kumjua Baba; mtu anayemkiri Mwana anamjua na Baba pia.

24 Hakikisheni kwamba ujumbe mliosikia tangu mwanzo unadumu mioyoni mwenu. Ujumbe huo ukikaa mioyoni mwenu, ninyi pia mtadumu ndani ya Mwana na ndani ya Baba. 25 Na yeye ametuahidi uzima wa milele.

26 Ninawaandikia mambo haya kuhusu wale wanaojaribu kuwapo tosha. 27 Lakini yule Roho Mtakatifu mliyempokea anakaa ndani yenu wala hamhitaji mtu kuwafundisha. Lakini kama vile huyo Roho Mtakatifu anavyowafundisha mambo yote, naye ni wa kweli wala si wa uongo; kama alivyowafundisha, dumuni ndani yake.

Watoto Wa Mungu

28 Na sasa, wanangu, kaeni siku zote ndani yake, kusudi ata kapotokea tuwe na ujasiri na wala tusijitenge naye kwa kuona aibu atakapokuja.

29 Kama mnajua kwamba yeye ni wa haki, basi mnajua kwamba kila atendaye haki amezaliwa naye.

Watoto Wa Mungu Wanavyopaswa Kuishi

Tazameni jinsi Baba alivyotupenda mno, hata tukaitwa watoto wa Mungu! Na hivyo ndivyo tulivyo. Watu wa ulimwengu hawatutambui kwa sababu hawakumjua Mungu. Wapendwa, sisi sasa tu wana wa Mungu. Tutakavyokuwa baadaye haijulikani bado, lakini tunajua kwamba Kristo atakapotokea, tutafanana naye, kwa maana tutamwona kama alivyo.

Kujitakasa Na Kuacha Dhambi

Na kila mtu mwenye tumaini hili hujitakasa, kama yeye mwe nyewe alivyo mtakatifu.

Kila atendaye dhambi ana hatia ya kuvunja sheria; maana dhambi ni uvunjaji sheria. Mnajua kwamba Kristo alikuja kuondoa dhambi naye hana dhambi yo yote. Hakuna mtu anayedumu ndani ya Kristo ambaye anatenda dhambi; na mtu ye yote anayetenda dhambi, huyo hajapata kumwona Kristo wala kumjua.

Watoto wadogo, mtu asije akawadanganya. Kila atendaye haki ni mwenye haki, kama Kristo alivyo wa haki. Kila atendaye dhambi ni wa shetani; kwa maana shetani ametenda dhambi tangu mwanzo. Mwana wa Mungu alikuja ili aziangamize kazi za shetani.

Mtu aliyezaliwa na Mungu haendelei na tabia ya kutenda dhambi, kwa maana ana asili ya Mungu; hawezi kuendelea kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa na Mungu.

Kutenda Haki Na Kupendana

10 Na hivi ndivyo tunavyoweza kutambua wazi kati ya walio watoto wa Mungu na walio watoto wa shetani. Mtu ye yote asiyet enda lililo haki si wa Mungu; wala asiyempenda ndugu yake si wa Mungu. 11 Na ujumbe mliosikia tangu mwanzo ndio huu: kwamba tupen dane. 12 Msiwe kama Kaini ambaye alikuwa wa yule mwovu akamwua ndugu yake. Na kwa nini alimwua? Kwa sababu matendo yake yalikuwa maovu lakini matendo ya nduguye yalikuwa ya haki.

13 Ndugu zangu, msishangae watu wa ulimwengu wakiwachukia. 14 Tunajua hakika kwamba tumevuka kutoka kwenye kifo na kuingia kwenye uzima kwa maana tunawapenda ndugu zetu. Asiye na upendo anaishi katika kifo. 15 Kila anayemchukia ndugu yake ni mwuaji, na kama mjuavyo, hakuna mwuaji ambaye ana uzima wa milele ndani yake.

16 Na tumeujua upendo kwa sababu Kristo alitoa maisha yake kwa ajili yetu. Na sisi tunapaswa kuyatoa maisha yetu kwa ajili ya ndugu zetu. 17 Lakini ikiwa mtu ana mali za hapa duniani na akamwona ndugu yake ana shida lakini akawa na moyo mgumu wala asimhurumie, mtu kama huyo anawezaje kusema anao upendo wa Mungu? 18 Wanangu, upendo wetu usiwe wa maneno matupu, bali upendo wetu udhihirishwe kwa vitendo na kweli.

19 Hivi ndivyo tutakavyoweza kuwa na hakika kwamba sisi ni wa kweli na hatutakuwa na wasiwasi mbele ya Mungu 20 hata kama dhamiri zetu zitatuhukumu; kwa maana tunajua kwamba Mungu ni mkuu kuliko dhamiri zetu, naye anajua kila kitu. 21 Wapendwa, ikiwa dhamiri zetu hazituhukumu, tuna ujasiri mbele za Mungu; 22 nasi tunapokea kutoka kwake lo lote tuombalo kwa kuwa tunatii amri zake na kufanya yampendezayo. 23 Na amri yake ndio hii: tuliamini jina la Mwanae Yesu Kristo na kupendana, kama alivyotu agiza. 24 Wote wanaozishika amri zake hukaa ndani yake na yeye ndani yao. Na hivi ndivyo tunavyojua kwamba anaishi ndani yetu: tunajua kwa njia ya yule Roho aliyetupatia.

Kujihadhari Na Maadui Wa Kristo

Wapendwa, msiamini kila roho bali zipimeni roho zote kwa makini muone kama zinatoka kwa Mungu. Kwa maana manabii wengi wa uongo wametokea duniani. Na hivi ndivyo mtakavyomtambua Roho wa Mungu: kila roho inayokiri kuwa Yesu Kristo alikuja kama mwana damu, hiyo inatoka kwa Mungu. Lakini roho yo yote ambayo haim kiri Kristo, si ya Mungu. Hii ndio roho ya mpinga-Kristo, ambayo mmekwisha kusikia kwamba inakuja, na sasa tayari iko duniani.

Lakini ninyi watoto wapendwa, ni wa Mungu, nanyi mmekwisha kuwashinda; kwa maana yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yule aliyeko duniani. Wao ni wa ulimwengu, kwa hiyo wanayoyasema ni ya ulimwengu na watu wa dunia huwasikiliza. Sisi ni wa Mungu. Anayemjua Mungu hutusikiliza, lakini asiye wa Mungu hatusikilizi. Na hivi ndivyo tunaweza kutambua kati ya Roho wa kweli na roho wa uongo.

Mungu Ni Upendo

Wapendwa, tupendane, kwa sababu upendo hutoka kwa Mungu. Mtu mwenye upendo amezaliwa na Mungu na anamjua Mungu. Mtu asiye na upendo hamjui Mungu; kwa maana Mungu ni upendo. Na hivi ndivyo Mungu alivyoonyesha upendo wake kwetu: alimtuma Mwana wake wa pekee ulimwenguni ili kwa ajili yake sisi tupate kwa kupitia kwake. 10 Na huu ndio upendo: si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi hata akamtuma Mwanae awe sadaka ya kulipia dhambi zetu. 11 Wapendwa, kwa kuwa Mungu ali tupenda kiasi hicho, sisi pia tunapaswa kupendana. 12 Hakuna mtu aliyepata kumwona Mungu; lakini tukipendana, Mungu anaishi ndani yetu, na upendo wake unakamilika ndani yetu.

13 Tunajua ya kwamba tunaishi ndani yake na yeye anaishi ndani yetu kwa sababu ametupatia Roho wake. 14 Na sisi tumeona na kushuhudia kwamba Baba amemtuma Mwanae awe mwokozi wa ulim wengu. 15 Kila mtu anayekiri kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu hukaa ndani yake, na yeye hukaa ndani ya Mungu. 16 Kwa hiyo tunajua na kutegemea upendo alio nao Mungu kwetu sisi. Mungu ni upendo, na mtu mwenye upendo hukaa ndani ya Mungu na Mungu hukaa ndani yake. 17 Upendo unakamilishwa ndani yetu ili tuwe na uja siri siku ile ya hukumu; kwa maana hata katika ulimwengu huu sisi tunaishi kama yeye. 18 Katika upendo hakuna woga; upendo ulioka milika hufukuza woga wote, kwa sababu woga hutokana na adhabu. Mtu mwenye woga hajakamilishwa katika upendo. 19 Tunapenda kwa sababu yeye alitupenda kwanza. 20 Mtu akisema, “Nampenda Mungu,” na huku anamchukia ndugu yake, huyo ni mwongo. Kwa maana mtu asipompenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hajamwona. 21 Na Mungu mwenyewe ametupa amri hii kwamba, mtu anayempenda Mungu hana budi kumpenda pia na ndugu yake.

Imani Ndani Ya Kristo

Kila mtu anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo, ni mtoto wa Mungu; na kila ampendaye mzazi wa mtoto, humpenda pia na mtoto wa mzazi huyo. Na hivi ndivyo tunavyojua kwamba tunawapenda watoto wa Mungu: tukimpenda Mungu na kuzitii amri zake. Kwa maana kumpenda Mungu ni kuzitii amri zake. Na amri zake hazitule mei. Kwa maana kila aliyezaliwa na Mungu ameushinda ulimwengu. Nasi tumeushinda ulimwengu kwa imani yetu. Ni nani basi aushin daye ulimwengu isipokuwa yeye aaminiye kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu?

Mashahidi Wa Yesu Kristo

Yesu Kristo ndiye aliyekuja kwa maji na damu; si kwa maji peke yake, bali kwa maji na damu. Roho mwenyewe ndiye anayemshu hudia kwa maana Roho ni kweli. Wapo mashahidi watatu: Roho, maji na damu; na hawa watatu wanakubaliana. Kama tunakubali ushahidi wa wanadamu, ushahidi wa Mungu una uzito zaidi; kwa sababu huu ni ushahidi wa Mungu ambao ameutoa kumhusu Mwanae. 10 Mtu anayemwamini Mwana wa Mungu anao ushuhuda huo ndani yake. Mtu asiyemwamini Mungu, amemfanya Mungu kuwa ni mwongo, kwa sababu hakuamini ushuhuda alioutoa Mungu kuhusu Mwanae. 11 Na ushuhuda wenyewe ndio huu: Mungu ametupatia uzima wa milele, na uzima huu umo kwa Mwanae. 12 Aliye naye Mwana anao uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana uzima.

Uzima Wa Milele

13 Ninawaandikia mambo haya ninyi mnaoliamini jina la Mwana wa Mungu kusudi mjue kuwa mnao uzima wa milele. 14 Na sisi tunao ujasiri huu mbele za Mungu kwamba, tukiomba cho chote sawa na mapenzi yake, atatusikia. 15 Na tukijua kwamba anatusikia kwa lo lote tunaloomba basi tuna hakika kwamba tumekwisha pata yale tuliyomwomba.

Umuhimu Wa Kuonyana

16 Mtu akimwona ndugu yake akitenda dhambi isiyompeleka kwe nye kifo, amwombee kwa Mungu, naye Mungu atampatia uzima. Ninasema kuhusu wale waliotenda dhambi ambazo si za kifo. Lakini ipo dhambi ambayo humpeleka mtu kwenye kifo. Sisemi kwamba ana paswa kuomba kuhusu hiyo. 17 Matendo yote yasiyo ya haki ni dhambi na kuna dhambi isiyompeleka mtu kwenye kifo.

18 Tunafahamu kuwa kila aliyezaliwa na Mungu haendelei kutenda dhambi; kwa sababu Mwana wa Mungu humlinda na yule mwovu hawezi kumgusa. 19 Tunajua kuwa sisi ni wa Mungu na kwamba ulim wengu wote unatawaliwa na yule mwovu. 20 Tunajua pia kwamba Mwana wa Mungu amekuja na ametupa ufahamu ili tumjue yeye aliye wa kweli, nasi tumo ndani yake yeye aliye wa kweli, yaani, ndani ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na uzima wa milele.

Kutoka kwa Mzee. Kwa mama mteule pamoja na watoto wake niwapendao katika kweli. Wala si mimi tu niwapendaye bali wote wanaoifahamu kweli; kwa sababu ya ile kweli ikaayo ndani yetu na ambayo itakuwa nasi hadi milele.

Neema, huruma, na amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo Mwana wake zitakuwa pamoja nasi katika kweli na upendo.

Kweli Na Upendo

Nimefurahi sana kuona kwamba baadhi ya watoto wako wanadumu katika kweli, kama Baba alivyotuamuru. Na sasa, mama mpendwa, sikuandikii amri mpya, bali ile ile ambayo tumekuwa nayo kutoka mwanzo: kwamba tupendane. Na upendo ni huu: kwamba tuishi kwa kuzifuata amri za Mungu. Na kama mlivyosikia tangu mwanzo, amri yake ni kwamba muishi maisha ya upendo.

Kwa maana wadanganyifu wengi wametokea duniani, watu wasiokiri ya kwamba Kristo alikuja kama mwanadamu. Mtu kama huyo ni mdanganyifu na mpinga-Kristo. Jihadharini msije mkapoteza yale mliyoyafanyia kazi, bali mpewe thawabu kamili.

Mtu ye yote anayevuka mpaka wa mafundisho ya Kristo, na kuyaacha, huyo hana Mungu. Na mtu anayedumu katika mafundisho ya Kristo, huyo anaye Baba na Mwana pia. 10 Mtu ye yote akija kwenu bila kuwaletea mafundisho haya, msimkaribishe nyumbani kwenu, wala msimsalimu. 11 Kwa maana mtu anayemsalimu anashiriki kazi zake za uovu.

12 Ninayo mengi ya kuwaandikia, lakini sipendi kutumia kara tasi na wino. Badala yake ninatarajia kuwatembelea na kuongea nanyi uso kwa uso, ili furaha yetu ikamilike.

Kutoka Kwa Mzee. Kwa mpendwa wangu Gayo, nimpendaye katika kweli. Mpendwa, ninakuombea ufanikiwe katika mambo yote na kwamba uwe na afya njema ya mwili; kwa maana najua roho yako ni salama. Nilifurahi sana walipokuja ndugu kadhaa wakashuhudia jinsi ulivyo mwaminifu katika kweli na jinsi unavyoendelea kuishi katika kweli. Hakuna kitu kinachonifurahisha zaidi kuliko kusi kia kwamba watoto wangu wanafuata kweli.

Uaminifu Wa Gayo

Mpendwa, wewe umekuwa mwaminifu kwa yote unayowatendea hao ndugu, ingawaje wao ni wageni kwako. Wamelishuhudia kanisa kuhusu upendo wako. Tafadhali wasaidie waendelee na safari yao kwa namna itakayompendeza Mungu. Kwa maana wanasafiri kwa ajili ya Bwana na wamekataa kupokea cho chote kutoka kwa watu wasiomjua Mungu . Kwa hiyo tunawajibu wa kuwasaidia watu wa namna hiyo ili tuwe watenda kazi pamoja nao kwa ajili ya kweli.

Diotrefe Na Demetrio

Niliandika barua kwa hilo kanisa; lakini Diotrefe apendaye kujiweka mbele kama kiongozi wao, hatambui mamlaka yangu. 10 Kwa hiyo nitakapokuja nitaeleza mambo anayofanya; na kuhusu maneno maovu anayosema juu yangu. Wala hatosheki na hayo bali anakataa kuwakaribisha ndugu. Pia anawazuia wale ambao wanataka kuwakarib isha na anawafukuza kutoka katika kanisa. 11 Mpendwa, usiige ubaya bali iga wema. Atendaye mema ni wa Mungu. Atendaye uovu hajapata kumwona Mungu. 12 Demetrio anashuhudiwa wema na kila mtu na hata kweli yenyewe inamshuhudia. Mimi pia ninamshuhudia wema, na wewe unajua kwamba ushuhuda wangu ni wa kweli.

Salamu Za Mwisho

13 Ninayo mengi ya kukuandikia, lakini afadhali nisitumie kalamu na wino. 14 Natarajia kukuona karibuni na tutaongea uso kwa uso.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica